Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 12.7
Bible en Swahili de l’est


Perplexité de Jérémie et réponse de Dieu

1 Wewe u mwenye haki, Ee Bwana, nitetapo nawe, lakini nitasema nawe katika habari ya haki. Mbona njia ya wabaya inasitawi? Mbona wote watendao hila wanakaa salama?
Malachie 3.15 Job 12.6 Psaumes 92.7 Psaumes 37.1 Psaumes 51.4
2 Umewapanda, naam, wametia mizizi, wanakua, naam, wanazaa matunda; katika vinywa vyao u karibu, bali katika mioyo yao u mbali.
Esaïe 29.13 Jérémie 11.17 Tite 1.16 Ezéchiel 33.31 Jérémie 45.4
3 Lakini wewe, Bwana, wanijua; umeniona, umeujaribu moyo wangu, jinsi unavyokuelekea; uwakokote kama kondoo waendao kuchinjwa, ukawaweke tayari kwa siku ya kuchinjwa.
2 Rois 20.3 Jérémie 17.18 Psaumes 17.3 Jacques 5.5 Psaumes 139.1-139.4
4 Hata lini itaomboleza nchi, na kukauka majani ya nchi yote? Kwa ajili ya mabaya yao wakaao ndani yake, wanyama wameangamia na ndege pia; kwa sababu walisema, Hatauona mwisho wetu.
Jérémie 9.10 Jérémie 4.25 Jérémie 23.10 Jérémie 7.20 Osée 4.3
5 Ikiwa umepiga mbio pamoja na hao waendao kwa miguu, nao wamekuchosha, basi wawezaje kushindana na farasi? Na ujapokuwa katika nchi ya amani u salama, lakini utafanyaje hapo katika kiburi cha Yordani?
Jérémie 50.44 Jérémie 49.19 1 Pierre 4.12 Hébreux 12.3-12.4 Josué 3.15
6 Kwa maana hata ndugu zako, na nyumba ya baba yako, wamekutenda mambo ya hila; naam, wamepiga kelele nyuma yako; usiwasadiki, wajapokuambia maneno mazuri.
Jérémie 9.4 Proverbes 26.25 Psaumes 69.8 Psaumes 12.2 Job 6.15
7 Nimeiacha nyumba yangu, nimeutupa urithi wangu; nimemtia mpenzi wangu katika mikono ya adui zake.
Esaïe 2.6 Jérémie 11.15 Psaumes 78.59-78.60 Osée 9.15 Ezéchiel 7.20-7.21
8 Urithi wangu umekuwa kwangu kama simba msituni; ameinua sauti yake juu yangu; kwa sababu hiyo nimemchukia.
Osée 9.15 Amos 6.8 Zacharie 11.8 Jérémie 51.38 Jérémie 2.15
9 Je! Urithi wangu umekuwa kwangu kama ndege mwenye madoadoa? Ndege wakali wanamtulia pande zote? Enendeni, wakusanyeni pamoja wanyama wote wa mwituni, waleteni ili wale.
Esaïe 56.9 Jérémie 7.33 2 Rois 24.2 Ezéchiel 23.22-23.25 Jérémie 2.15
10 Wachungaji wengi wameliharibu shamba langu la mizabibu, wamelikanyaga fungu langu chini ya miguu yao, wamefanya fungu langu zuri kuwa jangwa la ukiwa.
Esaïe 63.18 Esaïe 5.1-5.7 Jérémie 3.19 Jérémie 6.3 Psaumes 80.8-80.16
11 Wamelifanya kuwa ukiwa, na kwa kuwa ni ukiwa linanililia; nchi yote imefanywa kuwa ukiwa, kwa sababu hapana mtu aliyeweka haya moyoni mwake.
Esaïe 42.25 Jérémie 23.10 Jérémie 14.2 Jérémie 10.25 Ecclésiaste 7.2
12 Watekao nyara wamepanda juu ya vilele vya milima katika nyika; kwa maana upanga wa Bwana utakula toka upande mmoja wa nchi hata upande wa pili wa nchi; hapana mwenye mwili atakayekuwa na amani.
Jérémie 47.6 Amos 9.4 Ezéchiel 14.17 Esaïe 34.6 Jérémie 34.17
13 Wamepanda ngano, lakini watavuna miiba; wamejiumiza nafsi zao, lakini hawatakuwa na faida; naam, tahayarini kwa ajili ya matunda yenu, kwa sababu ya hasira kali ya Bwana.
Aggée 1.6 Michée 6.15 Deutéronome 28.38 Esaïe 55.2 Lévitique 26.16
14 Bwana asema hivi juu ya jirani zangu wote walio wabaya, waugusao urithi wangu niliowarithisha watu wangu Israeli, Tazama, nitawang’oa katika nchi yao, nami nitaing’oa nyumba ya Yuda isiwe kati yao.
Zacharie 2.8 Esaïe 11.11-11.16 Jérémie 49.7 Deutéronome 30.3 Sophonie 2.8-2.10
15 Tena itakuwa, baada ya kuwang’oa, nitarudi na kuwahurumia; nami nitawaleta tena, kila mtu aingie katika urithi wake, na kila mtu aingie katika nchi yake.
Jérémie 49.6 Jérémie 48.47 Jérémie 49.39 Deutéronome 30.3 Amos 9.14
16 Kisha itakuwa, ikiwa watajifunza kwa bidii njia za watu wangu, kuapa kwa jina langu, Kama Bwana aishivyo, vile vile kama walivyowafundisha watu wangu kuapa kwa Baali, ndipo watakapojengwa kati ya watu wangu.
Jérémie 4.2 Josué 23.7 Sophonie 1.5 Ephésiens 2.19-2.22 Esaïe 9.18-9.21
17 Bali, kama hawataki kusikia, kung’oa nitaling’oa taifa lile, na kuliangamiza kabisa, asema Bwana.
Esaïe 60.12 Psaumes 2.8-2.12 Zacharie 14.16-14.19 Daniel 11.4 Jérémie 18.7

Cette Bible est dans le domaine public.