Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 8.4
Bible en Swahili de l’est


Ruine des royaumes de Syrie et d’Israël

1 Bwana akaniambia, Ujipatie ubao mkubwa ukaandike juu yake kwa kalamu ya binadamu, Kwa Maher-shalal-hash-bazi;
Esaïe 30.8 Apocalypse 21.17 Jérémie 36.32 Jérémie 36.28 Habakuk 2.2-2.3
2 nami nitajipatia mashahidi waaminifu ili kuandika habari, yaani, Uria, kuhani, na Zekaria, mwana wa Yeberekia.
2 Rois 16.10-16.11 2 Rois 18.2 2 Corinthiens 13.1 2 Rois 16.15-16.16 Ruth 4.10-4.11
3 Nami nikamwendea huyo nabii mke, naye akapata mimba, akazaa mtoto mwanamume. Kisha Bwana akaniambia, Mwite jina lake Maher-shalal-hash-bazi.
Juges 4.4 2 Rois 22.14 Osée 1.3-1.9 Esaïe 7.13-7.14
4 Kwa maana kabla mtoto huyo hajapata kujua kusema, Baba yangu, na Mama yangu, hazina za Dameski na mateka ya Samaria yatachukuliwa mbele ya mfalme wa Ashuru.
Romains 9.11 2 Rois 17.3 Deutéronome 1.39 2 Rois 15.29 2 Rois 17.5-17.6
5 Kisha Bwana akasema nami mara ya pili, akaniambia,
Esaïe 7.10
6 Kwa sababu watu hawa wameyakataa maji ya Shiloa yapitayo polepole, na kufurahi kwa ajili ya Resini na huyo mwana wa Remalia,
Jean 9.7 Néhémie 3.15 Jérémie 2.13 Juges 9.16-9.20 Jérémie 18.14
7 basi sasa angalia; Bwana aleta juu yao maji ya huo Mto, yenye nguvu, mengi sana, nayo ni mfalme wa Ashuru na utukufu wake wote; naye atakuja, na kupita juu ya mifereji yake yote, atafurika juu ya kingo zake zote;
Esaïe 17.12-17.13 Esaïe 7.17 Genèse 6.17 Esaïe 7.20 Amos 8.8
8 naye atapita, atapita kwa kasi na kuingia Yuda; atafurika na kupita katikati, atafika hata shingoni; na kule kuyanyosha mabawa yake kutaujaza upana wa nchi yako, Ee Imanueli.
Esaïe 7.14 Esaïe 30.28 Matthieu 1.23 Esaïe 28.14-28.22 Esaïe 22.1-22.7
9 Fanyeni ghasia, enyi kabila za watu, Nanyi mtavunjwa vipande vipande; Tegeni masikio, ninyi nyote wa nchi zilizo mbali; Jikazeni viuno, nanyi mtavunjwa vipande vipande; Jikazeni viuno, nanyi mtavunjwa vipande vipande.
Esaïe 14.5-14.6 1 Rois 20.11 Esaïe 7.1-7.2 Proverbes 11.21 Psaumes 37.14-37.15
10 Fanyeni shauri pamoja, nalo litabatilika; Semeni neno, lakini halitasimama; Kwa maana Mungu yu pamoja nasi.
Romains 8.31 Job 5.12 Lamentations 3.37 2 Samuel 17.23 Esaïe 7.5-7.7
11 Maana Bwana aliniambia hivi, kwa mkono hodari, akanifundisha nisiende katika njia ya watu hawa, akisema,
Ezéchiel 3.14 Psaumes 32.8 Jérémie 20.7 Jérémie 20.9 Proverbes 1.15
12 Msiseme, Ni fitina, katika habari za mambo yote ambayo watu hawa watasema, Ni fitina; msihofu kwa hofu yao, wala msiogope.
1 Pierre 3.14-3.15 Luc 21.9 Luc 12.4-12.5 Psaumes 53.5 2 Rois 16.5-16.7
13 Bwana wa majeshi ndiye mtakayemtakasa; na awe yeye hofu yenu, na awe yeye utisho wenu.
Psaumes 76.7 Luc 12.5 Romains 4.20 Esaïe 26.3-26.4 Esaïe 29.23
14 Naye atakuwa ni mahali patakatifu; bali ni jiwe la kujikwaza na mwamba wa kujikwaa kwa nyumba za Israeli zote mbili, na mtego na tanzi kwa wenyeji wa Yerusalemu.
1 Pierre 2.8 Luc 2.34 Romains 9.32-9.33 Esaïe 28.16 Ezéchiel 11.16
15 Na wengi watajikwaa juu yake, na kuanguka na kuvunjika, na kunaswa na kukamatwa.
Matthieu 21.44 Esaïe 28.13 Jean 6.66 Luc 20.17-20.18 Matthieu 11.6
16 Ufunge huo ushuhuda, ukaitie muhuri sheria kati ya wanafunzi wangu.
Daniel 12.4 Apocalypse 19.10 1 Jean 5.9-5.12 Apocalypse 5.5 Apocalypse 10.4
17 Nami nitamngojea Bwana, awafichaye uso wake nyumba ya Yakobo, nami nitamtazamia.
Esaïe 54.8 Habakuk 2.3 Psaumes 27.14 Deutéronome 31.17-31.18 Michée 3.4
18 Angalieni, mimi na watoto hawa niliopewa na Bwana tu ishara na ajabu katika Israeli, zitokazo kwa Bwana wa majeshi, yeye akaaye katika mlima Sayuni.
Luc 2.34 Hébreux 2.13-2.14 Esaïe 7.3 Psaumes 9.11 Zacharie 8.3
19 Na wakati watakapokuambia, Tafuta habari kwa watu wenye pepo na kwa wachawi; waliao kama ndege na kunong’ona; je! Haiwapasi watu kutafuta habari kwa Mungu wao? Je! Waende kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu walio hai?
Esaïe 19.3 Lévitique 20.6 1 Samuel 28.8 2 Chroniques 33.6 Esaïe 29.4
20 Na waende kwa sheria na ushuhuda; ikiwa hawasemi sawasawa na neno hili, bila shaka kwa hao hapana asubuhi.
2 Pierre 1.19 Michée 3.6 Esaïe 30.8-30.11 Esaïe 8.16 Jean 5.39
21 Nao watapita katikati yake, wamedhikika sana na kuwa na njaa; na itakuwa watakapoona njaa, watalalamika na kuapa kwa mfalme wao, na kwa Mungu wao, na kuelekeza nyuso zao juu;
Esaïe 9.20 Lamentations 4.4-4.5 Job 2.9 Job 1.11 2 Rois 6.33
22 nao wataiangalia nchi, na, tazama, shida na giza; hapana changamko kwa sababu ya dhiki; nao watafukuzwa na kuingia katika giza kubwa.
Esaïe 5.30 Sophonie 1.14-1.15 Jérémie 13.16 Amos 5.18-5.20 Esaïe 8.20

Cette Bible est dans le domaine public.