Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 65.12
Bible en Swahili de l’est


Réponse de Dieu

1 Watu wasionitaka wanauliza habari zangu; nimeonekana na hao wasionitafuta; naliliambia taifa lisiloitwa kwa jina langu,
Romains 10.20 Ephésiens 2.12-2.13 Romains 9.24-9.26 Osée 1.10 Esaïe 2.2-2.3
2 Nitazameni, nitazameni. Mchana kutwa nimewanyoshea mikono yangu watu walioasi, watu waendao katika njia isiyo njema, wakifuata mawazo yao wenyewe;
Romains 10.21 Esaïe 1.2 Proverbes 1.24 Esaïe 55.7 Psaumes 81.11-81.12
3 watu wanikasirishao mbele za uso wangu daima, wakitoa dhabihu katika bustani zao, na kufukiza uvumba juu ya matofali;
Esaïe 1.29 Esaïe 66.17 Job 1.11 Job 2.5 Esaïe 3.8
4 waketio kati ya makaburi, na kulala katika mahali pao pa siri; walao nyama ya nguruwe, na mchuzi wa vitu vinichukizavyo u katika vyombo vyao;
Lévitique 11.7 Esaïe 66.17 Esaïe 66.3 Marc 5.2-5.5 Ezéchiel 4.14
5 watu wasemao, Simama peke yako, usinikaribie mimi, kwa maana mimi ni mtakatifu kuliko wewe; watu hao ni moshi puani mwangu, moto uwakao mchana kutwa.
Luc 18.9-18.12 Luc 7.39 Proverbes 16.5 Matthieu 9.11 Luc 5.30
6 Tazama, neno hili limeandikwa mbele zangu. Sitanyamaza, lakini nitalipa, naam, mimi nitawalipa ujira wao vifuani mwao;
Jérémie 16.18 Psaumes 50.3 Psaumes 79.12 Psaumes 50.21 Esaïe 42.14
7 maovu yenu na maovu ya baba zenu pamoja, asema Bwana, ninyi mliofukiza uvumba juu ya milima, na kunitukana juu ya vilima; basi, kwa ajili ya hayo nitawapimia kwanza kazi yao vifuani mwao.
Esaïe 57.7 Ezéchiel 20.27-20.28 Exode 20.5 Jérémie 13.25 Jérémie 5.29
8 Bwana asema hivi, Kama vile divai mpya ipatikanavyo katika kichala, na mtu mmoja husema, Usikiharibu kwa maana mna baraka ndani yake; ndivyo nitakavyotenda kwa ajili ya watumishi wangu, ili nisiwaharibu wote.
Esaïe 6.13 Romains 9.27-9.29 Romains 11.24-11.26 Matthieu 24.22 Joël 2.14
9 Nami nitaleta uzao toka Yakobo, na mrithi wa milima yangu toka Yuda, na mteule wangu atairithi, na watumishi wangu watakaa huko.
Amos 9.11-9.15 Esaïe 27.6 Ezéchiel 36.24 Esaïe 45.19 Esaïe 10.20-10.22
10 Na Sharoni itakuwa zizi la makundi ya kondoo, na bonde la Akori mahali pa kulala makundi ya ng’ombe, kwa ajili ya watu wangu walionitafuta.
Esaïe 35.2 Osée 2.15 Esaïe 33.9 Esaïe 51.1 Ezéchiel 34.13-34.14
11 Bali ninyi mmwachao Bwana, na kuusahau mlima wangu mtakatifu, na kuandika meza kwa ajili ya Bahati, na kuijazia Ajali vyombo vya divai iliyochanganyika;
Esaïe 1.28 Esaïe 2.2 Esaïe 65.25 1 Chroniques 28.9 1 Corinthiens 10.20-10.21
12 mimi nitawaandikia kuuawa kwa upanga, na ninyi nyote mtainama ili kuchinjwa; kwa sababu nilipoita hamkuitika; niliponena, hamkusikia; bali mlitenda yaliyo mabaya machoni pangu, mlichagua mambo nisiyoyafurahia.
Jérémie 7.13 2 Chroniques 36.15-36.16 Esaïe 50.2 Matthieu 21.34-21.43 Esaïe 3.25
13 Kwa hiyo Bwana MUNGU asema hivi, Tazama, watumishi wangu watakula, bali ninyi mtaona njaa; tazama, watumishi wangu watakunywa, bali ninyi mtaona kiu; tazama, watumishi wangu watafurahi, bali ninyi mtatahayarika;
Malachie 3.18 Esaïe 66.14 Esaïe 61.7 Luc 16.24-16.25 Esaïe 66.5
14 tazama, watumishi wangu wataimba kwa furaha ya moyo, bali ninyi mtalia kwa huzuni ya moyo; mtapiga kelele kwa sababu ya uchungu wa roho zenu.
Matthieu 8.12 Luc 13.28 Jacques 5.13 Psaumes 66.4 Esaïe 24.14
15 Nanyi mtaliacha jina lenu kuwa laana kwa wateule wangu. Na Bwana MUNGU atakuua; naye atawaita watumishi wake kwa jina lingine.
Zacharie 8.13 Esaïe 62.2 Romains 9.26 Jérémie 29.22 Esaïe 65.9
16 Hata itakuwa yeye atakayejibariki duniani, atajibariki kwa Mungu wa kweli; naye atakayeapa duniani, ataapa kwa Mungu wa kweli. Kwa kuwa taabu za kwanza zimesahauliwa, na kwa kuwa zimefichwa machoni pangu.
Psaumes 31.5 Esaïe 19.18 Jérémie 4.2 Deutéronome 32.4 Jérémie 12.16
17 Maana, tazama, mimi naumba mbingu mpya na nchi mpya, na mambo ya kwanza hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni.
2 Pierre 3.13 Esaïe 66.22 Apocalypse 21.1-21.5 Jérémie 3.16 Esaïe 43.18
18 Lakini furahini, mkashangilie daima, kwa ajili ya hivi niviumbavyo; maana, tazama, naumba Yerusalemu uwe shangwe, na watu wake wawe furaha.
Psaumes 98.1-98.9 Esaïe 66.10-66.14 Apocalypse 11.15-11.18 Esaïe 44.23 Psaumes 96.10-96.13
19 Nami nitaufurahia Yerusalemu, nitawaonea shangwe watu wangu; sauti ya kulia haitasikiwa ndani yake tena, wala sauti ya kuomboleza.
Esaïe 35.10 Apocalypse 7.17 Esaïe 25.8 Apocalypse 21.4 Esaïe 62.4-62.5
20 Hatakuwapo tena mtoto wa siku chache, wala mzee asiyetimia siku zake; kwa maana mtoto atakufa mwenye umri wa miaka mia; bali mtenda dhambi mwenye umri wa miaka mia atalaaniwa.
Deutéronome 4.40 Job 5.26 Psaumes 34.12 Esaïe 3.11 Ecclésiaste 8.12-8.13
21 Nao watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake.
Amos 9.14 Esaïe 32.18 Esaïe 62.8-62.9 Jérémie 31.4-31.5 Esaïe 37.30
22 Hawatajenga, akakaa mtu mwingine ndani yake; hawatapanda, akala mtu mwingine; maana kama siku za mti ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, na wateule wangu wataifurahia kazi ya mikono yao muda wa siku nyingi.
Psaumes 92.12-92.14 Psaumes 91.16 Esaïe 65.15 Esaïe 65.9 Psaumes 21.4
23 Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa kwa taabu; kwa sababu wao ni wazao wa hao waliobarikiwa na Bwana, na watoto wao pamoja nao.
Esaïe 61.9 Actes 2.39 Jérémie 32.38-32.39 Esaïe 49.4 Deutéronome 28.3-28.12
24 Na itakuwa ya kwamba, kabla hawajaomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia.
Daniel 10.12 1 Jean 5.14-5.15 Marc 11.24 Esaïe 58.9 Psaumes 91.15
25 Mbwa-mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, na simba atakula majani kama ng’ombe; na mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote, asema Bwana.
Esaïe 65.11 Michée 7.17 Esaïe 11.6-11.9 Michée 4.3 Esaïe 2.4

Cette Bible est dans le domaine public.