Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 60.18
Bible en Swahili de l’est


Gloire future de Jérusalem

1 Ondoka, uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja, Na utukufu wa Bwana umekuzukia.
Ephésiens 5.14 Ephésiens 5.8 Esaïe 52.1-52.2 Esaïe 60.19-60.20 Malachie 4.2
2 Maana, tazama, giza litaifunika dunia, Na giza kuu litazifunika kabila za watu; Bali Bwana atakuzukia wewe, Na utukufu wake utaonekana juu yako.
1 Pierre 2.9 Hébreux 1.2-1.3 Jean 8.55 Malachie 4.2 1 Rois 8.11
3 Na mataifa wataijilia nuru yako, Na wafalme kuujia mwanga wa kuzuka kwako.
Esaïe 49.23 Apocalypse 21.24 Esaïe 45.14 Esaïe 60.16 Esaïe 54.1-54.3
4 Inua macho yako, utazame pande zote; Wote wanakusanyana; wanakujia wewe; Wana wako watakuja kutoka mbali. Na binti zako watabebwa nyongani.
Esaïe 49.20-49.22 Esaïe 49.18 Esaïe 11.12 Esaïe 43.6 Galates 3.28-3.29
5 Ndipo utakapoona na kutiwa nuru, Na moyo wako utatetemeka na kukunjuka; Kwa kuwa wingi wa bahari utageuzwa kukujia, Utajiri wa mataifa utakuwasilia.
Esaïe 61.6 Esaïe 23.18 Psaumes 96.7-96.9 Actes 24.17 Romains 11.25
6 Wingi wa ngamia utakufunika, Ngamia vijana wa Midiani na Efa; Wote watakuja kutoka Sheba; Wataleta dhahabu na uvumba; Na kuzitangaza sifa za Bwana.
Matthieu 2.11 Psaumes 72.10 Juges 6.5 Genèse 25.3-25.4 Romains 15.9
7 Makundi yote ya Kedari yatakusanyika kwako, Kondoo waume wa Nebayothi watakutumikia; Watapanda juu ya madhabahu yangu kwa kibali, Nami nitaitukuza nyumba ya utukufu wangu.
Esaïe 56.7 Genèse 25.13 Job 42.8 Esaïe 42.11 Romains 15.16
8 Ni nani hawa warukao kama wingu, Na kama njiwa waendao madirishani kwao?
Luc 13.29 Genèse 8.8-8.11 Esaïe 60.4 Apocalypse 7.9 Esaïe 45.22
9 Hakika yake visiwa vitaningojea, Na merikebu za Tarshishi kwanza, Ili kuleta wana wako kutoka mbali, Na fedha yao na dhahabu yao pamoja nao, Kwa ajili ya jina la Bwana, Mungu wako, Kwa ajili yake Mtakatifu wa Israeli, Kwa kuwa amekutukuza wewe.
Esaïe 55.5 Esaïe 11.11 Esaïe 2.16 Esaïe 51.5 Esaïe 49.1
10 Na wageni watajenga kuta zako, Na wafalme wao watakuhudumu; Maana katika ghadhabu yangu nalikupiga, Lakini katika upendeleo wangu nimekurehemu.
Apocalypse 21.24 Esaïe 49.23 Zacharie 6.15 Esaïe 61.5 Esdras 7.12-7.28
11 Malango yako nayo yatakuwa wazi daima; Hayatafungwa mchana wala usiku; Ili watu wapate kukuletea utajiri wa mataifa, Na wafalme wao wakiongozwa pamoja nao.
Esaïe 60.5 Apocalypse 21.25-21.26 Esaïe 60.18 Esaïe 62.10 Néhémie 13.19
12 Kwa maana kila taifa na ufalme wa watu Wasiotaka kukutumikia wataangamia; Naam, mataifa hayo wataharibiwa kabisa.
Zacharie 14.12-14.19 Daniel 2.35 Psaumes 2.12 Zacharie 12.2-12.4 Esaïe 54.15
13 Utukufu wa Lebanoni utakujia wewe, Mberoshi na mtidhari na mteashuri pamoja; Ili kupapamba mahali pangu patakatifu, Nami nitapatukuza mahali pa miguu yangu.
Esaïe 35.2 1 Chroniques 28.2 Psaumes 132.7 Osée 14.6-14.7 Esaïe 55.13
14 Na wana wa watu wale waliokutesa Watakuja kwako na kukuinamia; Nao wote waliokudharau Watajiinamisha hata nyayo za miguu yako; Nao watakuita, Mji wa Bwana, Sayuni wa Mtakatifu wa Israeli.
Esaïe 49.23 Apocalypse 3.9 Esaïe 14.1-14.2 Hébreux 12.22 Esaïe 45.14
15 Na kwa kuwa umeachwa na kuchukiwa, Hata ikawa hapana mtu aliyepita ndani yako, Nitakufanya kuwa fahari ya milele, Furaha ya vizazi vingi.
Esaïe 61.7 Jérémie 30.17 Esaïe 65.18 Esaïe 35.10 Esaïe 4.2
16 Utanyonya maziwa ya mataifa, Utanyonya matiti ya wafalme; Nawe utajua ya kuwa mimi, Bwana, ni mwokozi wako, Na mkombozi wako, Mwenye enzi wa Yakobo.
Esaïe 66.11-66.12 Esaïe 49.23 Ezéchiel 34.30 Esaïe 66.14 Esaïe 59.20
17 Badala ya shaba nitaleta dhahabu, Na badala; ya chuma nitaleta fedha, Na badala ya mti, shaba, Na badala ya mawe, chuma; Tena nitawafanya wasimamizi wako wawe amani, Na hao wakutozao fedha kuwa haki.
2 Pierre 3.13 Esaïe 30.26 Hébreux 11.40 Esaïe 1.26 Zacharie 12.8
18 Jeuri haitasikiwa tena katika nchi yako, Ukiwa na uharibifu hazitakuwa mipakani mwako; Bali utaziita kuta zako, Wokovu, Na malango yako, Sifa.
Esaïe 26.1 Esaïe 11.9 Psaumes 72.3-72.7 Esaïe 2.4 Michée 4.3
19 Jua halitakuwa nuru yako tena wakati wa mchana, Wala mwezi hautakupa nuru kwa mwangaza wake; Bali Bwana atakuwa nuru ya milele kwako, Na Mungu wako atakuwa utukufu wako.
Apocalypse 22.5 Apocalypse 21.23 Zacharie 2.5 Psaumes 36.9 Psaumes 4.2
20 Jua lako halitashuka tena, Wala mwezi wako hautajitenga; Kwa kuwa Bwana mwenyewe atakuwa nuru yako ya milele; Na siku za kuomboleza kwako zitakoma.
Apocalypse 21.4 Esaïe 35.10 Psaumes 84.11 Malachie 4.2 Esaïe 65.19
21 Watu wako nao watakuwa wenye haki wote, Nao watairithi nchi milele;
Matthieu 15.13 Psaumes 37.22 Esaïe 61.3 Esaïe 29.23 Psaumes 37.11
22 Mdogo atakuwa elfu, Na mnyonge atakuwa taifa hodari; Mimi, Bwana, nitayahimiza hayo wakati wake.
Habakuk 2.3 Esaïe 5.19 Actes 2.41 Matthieu 13.31-13.32 Daniel 2.44

Cette Bible est dans le domaine public.