Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 6.4
Bible en Swahili de l’est


Appel et mission d’Ésaïe

1 Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu.
Jean 12.41 Apocalypse 15.8 Jean 1.18 Daniel 7.9 Apocalypse 7.15-7.17
2 Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka.
Apocalypse 4.8 Psaumes 103.20 Esaïe 6.6 Apocalypse 7.11 Ezéchiel 1.11
3 Wakaitana, kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni Bwana wa majeshi; dunia yote imejaa utukufu wake.
Apocalypse 4.8-4.9 Psaumes 72.19 Esaïe 40.5 Exode 15.11 Nombres 14.21
4 Na misingi ya vizingiti ikatikisika kwa sababu ya sauti yake aliyelia, nayo nyumba ikajaa moshi.
Apocalypse 15.8 Amos 9.1 Psaumes 18.8 Ezéchiel 10.5 Exode 40.34
5 Ndipo niliposema, Ole wangu! Kwa maana nimepotea; kwa sababu mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninakaa kati ya watu wenye midomo michafu; na macho yangu yamemwona Mfalme, Bwana wa majeshi.
Exode 6.30 Exode 6.12 Jérémie 9.3-9.8 Ezéchiel 2.6-2.8 Jérémie 1.6
6 Kisha mmoja wa maserafi wale akaruka akanikaribia; naye alikuwa na kaa la moto mkononi mwake, ambalo alikuwa amelitwaa kwa makoleo toka juu ya madhabahu;
Apocalypse 8.3-8.5 Ezéchiel 10.2 Hébreux 13.10 Hébreux 9.22-9.26 Daniel 9.21-9.23
7 akanigusa kinywa changu kwa kaa hilo, akaniambia, Tazama, hili limekugusa midomo yako, na uovu wako umeondolewa, na dhambi yako imefunikwa.
Jérémie 1.9 Daniel 10.16 Esaïe 53.5 1 Jean 1.7 Esaïe 43.25
8 Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa, nitume mimi.
Exode 4.10-4.13 Ephésiens 3.8 Genèse 1.26 Deutéronome 4.33-4.36 Esaïe 65.1
9 Naye akaniambia, Enenda, ukawaambie watu hawa, Fulizeni kusikia, lakini msifahamu; fulizeni kutazama, lakini msione.
Matthieu 13.14-13.15 Luc 8.10 Marc 4.12 Jean 12.40 Esaïe 29.13
10 Uunoneshe moyo wa watu hawa, ukayatie uzito masikio yao, ukayafumbe macho yao; wasije wakaona kwa macho yao, na kusikia kwa masikio yao, na kufahamu kwa mioyo yao, na kurejea na kuponywa.
Matthieu 13.15 Jérémie 5.21 Actes 28.27 Deutéronome 32.15 Psaumes 17.10
11 Ndipo nilipouliza, Ee Bwana, hata lini? Naye akanijibu, Hata miji itakapokuwa ukiwa, haina wenyeji, na nyumba zitakapokuwa hazina watu, na nchi hii itakapokuwa ganjo kabisa;
Esaïe 1.7 Esaïe 3.26 Esaïe 24.1-24.12 Psaumes 79.5 Psaumes 94.3
12 hata Bwana atakapowahamisha watu waende mbali sana, na mahame yatakapokuwa mengi ndani ya nchi.
Jérémie 4.29 Esaïe 26.15 Jérémie 15.4 Jérémie 12.7 2 Rois 25.11
13 Na ijapokuwa imebaki sehemu moja katika sehemu kumi ndani yake, italiwa hii nayo; kama mvinje na kama mwaloni, ambao shina lake limebaki, ingawa imekatwa; kadhalika mbegu takatifu ndiyo shina lake.
Job 14.7-14.9 Romains 11.5-11.6 Romains 11.16-11.29 Esaïe 1.9 Esdras 9.2

Cette Bible est dans le domaine public.