Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 54.14
Bible en Swahili de l’est


Prospérité future d’Israël

1 Imba, wewe uliye tasa, wewe usiyezaa; paza sauti yako kwa kuimba, piga kelele, wewe usiyekuwa na utungu; maana watoto wake aliyeachwa ni wengi kuliko watoto wake yeye aliyeolewa, asema Bwana.
Galates 4.27 1 Samuel 2.5 Esaïe 62.4 Hébreux 11.11-11.12 Psaumes 67.3-67.5
2 Panua mahali pa hema yako, na wayatandaze mapazia ya maskani yako; usiwakataze; ongeza urefu wa kamba zako; vikaze vigingi vya hema yako.
Esaïe 49.19-49.20 Esaïe 33.20 Jérémie 10.20 Exode 39.40 Exode 35.18
3 Kwa maana utaenea upande wa kuume na upande wa kushoto; na wazao wako watawamiliki mataifa; wataifanya miji iliyokuwa ukiwa kukaliwa na watu.
Esaïe 43.5-43.6 Esaïe 60.3-60.13 Esaïe 61.5-61.9 Esaïe 55.5 Romains 9.25-9.26
4 Usiogope; maana hutatahayarika; wala usifadhaike; maana hutaaibishwa; kwa kuwa utaisahau aibu ya ujana wako, pia mashutumu ya ujane wako hutayakumbuka tena.
Jérémie 31.19 Esaïe 41.10 Esaïe 45.16-45.17 1 Pierre 2.6 Osée 3.1-3.5
5 Kwa sababu Muumba wako ni mume wako; Bwana wa majeshi ndilo jina lake; na Mtakatifu wa Israeli ndiye Mkombozi wako; Yeye ataitwa Mungu wa dunia yote.
Esaïe 48.17 Osée 2.19-2.20 Ephésiens 5.25-5.27 Ezéchiel 16.8 Jean 3.29
6 Maana Bwana amekuita kama mke aliyeachwa na kuhuzunishwa rohoni, kama mke wakati wa ujana, atupwapo, asema Mungu wako.
Esaïe 62.4 2 Corinthiens 7.6 Malachie 2.14 Osée 2.1-2.2 Ecclésiaste 9.9
7 Kwa kitambo kidogo nimekuacha; lakini kwa rehema nyingi nitakukusanya.
Esaïe 26.20 Michée 4.6 Ezéchiel 36.24 2 Pierre 3.8 2 Corinthiens 4.17
8 Kwa ghadhabu ifurikayo nalikuficha uso wangu dakika moja; lakini kwa fadhili za milele nitakurehemu, asema Bwana, Mkombozi wako.
Esaïe 54.5 Esaïe 55.3 Jérémie 31.3 Psaumes 27.9 Psaumes 13.1
9 Kwa maana jambo hili limekuwa kama maji ya Nuhu kwangu; maana kama nilivyoapa ya kwamba maji ya Nuhu hayatapita juu ya dunia tena, kadhalika nimeapa ya kwamba sitakuonea hasira, wala kukukemea.
Genèse 8.21 Esaïe 12.1 Genèse 9.11-9.16 Jérémie 33.20-33.26 Psaumes 104.9
10 Maana milima itaondoka, na vilima vitaondolewa; bali wema wangu hautaondoka kwako, wala agano langu la amani halitaondolewa; asema Bwana akurehemuye.
Malachie 2.5 Psaumes 46.2 Matthieu 24.35 Ephésiens 2.4-2.5 Romains 11.29
11 Ewe uliyeteswa, uliyerushwa na tufani, usiyetulizwa, tazama, nitaweka mawe yako kwa rangi nzuri, nitaweka misingi yako kwa yakuti samawi.
1 Chroniques 29.2 Esaïe 51.23-52.5 Psaumes 129.1-129.3 Ezéchiel 10.1 Apocalypse 12.13-12.17
12 Nami nitaifanya minara yako ya akiki nyekundu, na malango yako ya almasi, na mipaka yako yote ya mawe yapendezayo.
13 Na watoto wako wote watafundishwa na Bwana; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi.
Jean 6.45 Psaumes 119.165 Esaïe 48.18 Romains 5.1 Philippiens 4.7
14 Utathibitika katika haki; utakuwa mbali na kuonewa, kwa maana hutaogopa; na mbali na hofu, kwa maana haitakukaribia.
Proverbes 3.25-3.26 Zacharie 9.8 Esaïe 1.26 2 Pierre 3.13 Jérémie 30.10
15 Tazama, yamkini watakusanyana; lakini si kwa shauri langu. Watu wo wote watakaokusanyana juu yako wataanguka kwa ajili yako.
Apocalypse 19.19-19.21 Apocalypse 20.8-20.9 Zacharie 14.2-14.3 Apocalypse 16.14 Zacharie 2.8
16 Tazama, nimemwumba mhunzi avukutaye moto wa makaa, akatoa silaha kwa kazi yake; nami nimemwumba mharibu ili aharibu.
Proverbes 16.4 Exode 9.16 Jean 19.11 Esaïe 10.15 Daniel 4.34-4.35
17 Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema Bwana.
Esaïe 50.8 Romains 8.28-8.39 Jean 10.28-10.30 Romains 8.1 Apocalypse 12.10

Cette Bible est dans le domaine public.