Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 28.25
Bible en Swahili de l’est


Prophétie sur Éphraïm

1 Ole wa taji ya kiburi ya walevi wa Efraimu, na ua la uzuri wa fahari yake linalonyauka, lililo kichwani mwa bonde linalositawi, la hao walioshindwa na divai!
Osée 7.5 Esaïe 28.7 Esaïe 28.3-28.4 Amos 6.6 Amos 2.8
2 Tazama, Bwana ana mmoja aliye hodari, mwenye nguvu; kama dhoruba ya mvua ya mawe, tufani iharibuyo, kama dhoruba ya maji mengi yafurikayo, ndivyo atakavyotupa chini kwa mkono.
Esaïe 30.30 Ezéchiel 13.11 Nahum 1.8 Esaïe 29.6 Matthieu 7.25-7.27
3 Taji ya kiburi ya walevi wa Efraimu itakanyagwa kwa miguu;
Esaïe 26.6 Daniel 8.13 2 Rois 9.33 Esaïe 25.10 Apocalypse 11.2
4 na ua la uzuri wa fahari yake linalonyauka, lililo kichwani mwa bonde linalositawi, litakuwa kama tini iliyotangulia kuiva kabla ya wakati wa hari, ambayo, aionapo yeye aiangaliaye, huila mara anapoishika mkononi mwake.
Michée 7.1 Nahum 3.12 Esaïe 28.1 Osée 9.10-9.11 Osée 13.15
5 Katika siku ile Bwana wa majeshi atakuwa ni taji ya fahari, na kilemba cha uzuri, kwa mabaki ya watu wake.
Esaïe 60.19 Esaïe 62.3 Esaïe 41.16 Esaïe 45.25 Job 29.14
6 Naye atakuwa roho ya hukumu kwake yeye aketiye ili ahukumu; naye atakuwa nguvu kwao wageuzao nyuma vita langoni.
1 Rois 3.28 Jean 5.30 Esaïe 32.15-32.16 Esaïe 11.2-11.4 Psaumes 18.32-18.34
7 Lakini hawa nao wamekosa kwa divai, wamepotea kwa kileo; kuhani na nabii wamekosa kwa kileo, wamemezwa kwa divai, wamepotea kwa kileo; hukosa katika maono, hujikwaa katika hukumu.
Esaïe 56.10-56.12 Esaïe 19.14 Luc 21.34 Matthieu 24.29 Proverbes 20.1
8 Maana meza zote zimejaa matapiko na uchafu, hapana mahali palipo safi.
Jérémie 48.26 Proverbes 26.11 Habakuk 2.15-2.16
9 Atamfundisha nani maarifa? Atamfahamisha nani habari hii? Je! Ni wale walioachishwa maziwa, walioondolewa matitini?
Psaumes 131.2 Jérémie 6.10 Matthieu 21.15-21.16 Matthieu 11.25 Jean 12.38
10 Kwa maana ni amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo.
Jérémie 25.3-25.7 2 Chroniques 36.15-36.16 Esaïe 28.13 2 Timothée 3.7 Néhémie 9.29-9.30
11 La, bali kwa midomo ya watu wageni, na kwa lugha nyingine atasema na watu hawa;
1 Corinthiens 14.21 Esaïe 33.19 Deutéronome 28.49 Jérémie 5.15
12 ambao aliwaambia, Hii ndiyo raha yenu, mpeni raha yeye aliyechoka; huku ndiko kuburudika; lakini hawakutaka kusikia.
Matthieu 11.28-11.29 Esaïe 30.15 Jérémie 6.16 Jérémie 44.16 Esaïe 11.10
13 Kwa sababu hiyo neno la Bwana kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo; ili waende na kuanguka nyuma, na kuvunjwa, na kunaswa, na kuchukuliwa.
Matthieu 21.44 2 Pierre 3.16 Esaïe 8.14-8.15 2 Corinthiens 2.16 Osée 6.5
14 Basi, lisikieni neno la Bwana, enyi watu wenye dharau, mnaowatawala watu hawa walio ndani ya Yerusalemu.
Esaïe 1.10 Esaïe 29.20 Esaïe 28.22 Osée 7.5 Esaïe 5.9
15 Kwa sababu mmesema, Tumefanya agano na mauti, tumepatana na kuzimu; pigo lifurikalo litakapopita, halitatufikia sisi; kwa maana tumefanya maneno ya uongo kuwa kimbilio letu, tumejificha chini ya maneno yasiyo kweli;
Esaïe 8.7-8.8 Esaïe 28.2 Ezéchiel 13.22 Esaïe 28.18 Amos 2.4
16 kwa ajili ya hayo Bwana, MUNGU, asema hivi, Tazama, naweka jiwe katika Sayuni, liwe msingi, jiwe lililojaribiwa, jiwe la pembeni lenye thamani, msingi ulio imara; yeye aaminiye hatafanya haraka.
Psaumes 118.22 Actes 4.11-4.12 Romains 9.33 1 Pierre 2.6-2.8 Luc 20.17-20.18
17 Nami nitafanya hukumu kuwa ndiyo kanuni, na haki kuwa ndiyo timazi; na mvua ya mawe itachukulia mbali hilo kimbilio la maneno ya uongo, na maji yatapagharikisha mahali pa kujisitiri.
2 Rois 21.13 Amos 7.7-7.9 Esaïe 28.2 Apocalypse 16.21 Josué 10.11
18 Na agano lenu mliloagana na mauti litabatilika, tena mapatano yenu mliyopatana na kuzimu hayatasimama; pigo lifurikalo litakapopita, ndipo ninyi mtakapokanyagwa nalo.
Esaïe 28.15 Esaïe 7.7 Esaïe 8.10 Esaïe 28.3 Jérémie 44.28
19 Kila wakati litakapopita litawachukueni. Maana litapita asubuhi baada ya asubuhi, wakati wa mchana na wakati wa usiku; na kuifahamu habari ile kutakuwa kitisho tu.
2 Rois 24.2 Ezéchiel 21.19-21.23 Job 18.11 Habakuk 3.16 Esaïe 37.3
20 Maana kitanda kile ni kifupi asiweze mtu kujinyosha juu yake, na nguo ile ya kujifunika ni nyembamba asipate mtu kujizingisha.
Esaïe 64.6 Esaïe 59.5-59.6 Esaïe 57.12-57.13 Esaïe 66.3-66.6 1 Corinthiens 1.18-1.31
21 Maana Bwana ataondoka kama vile katika mlima Perasimu, ataghadhibika kama vile katika bonde la Gibeoni; apate kufanya kazi yake, kazi yake ya ajabu; na kulitimiza tendo lake, tendo lake la ajabu.
1 Chroniques 14.16 2 Samuel 5.20 Josué 10.12 Josué 10.10 1 Chroniques 14.11
22 Basi sasa msiwe watu wenye kudharau, vifungo vyenu msije vikakazwa; maana nimesikia kwa Bwana, Bwana wa majeshi, habari ya hukumu itakayotimizwa, nayo imekusudiwa, itakayoipata dunia yote pia.
Esaïe 10.22-10.23 Esaïe 28.14-28.15 Daniel 9.26-9.27 Actes 17.32 Lamentations 1.14

Parabole du cultivateur

23 Tegeni masikio, sikieni sauti yangu, sikilizeni mkasikie neno langu.
Apocalypse 2.29 Apocalypse 2.11 Apocalypse 2.7 Apocalypse 2.14 Esaïe 1.2
24 Je! Mwenye kulima alima daima, ili apande? Afunua daima madongoa ya nchi yake, na kuyavunja?
Jérémie 4.3 Osée 10.11-10.12
25 Akiisha kuulainisha uso wa nchi yake, je! Hamwagi huko na huko kunde, na kutupa-tupa jira, na kuitia ngano safu safu, na shayiri mahali pake palipochaguliwa, na kusemethi karibu na mipaka yake?
Exode 9.31-9.32 Ezéchiel 4.9 Matthieu 23.23
26 Kwa maana Mungu wake anamwagiza vizuri na kumfundisha.
Daniel 1.17 Psaumes 144.1 Jacques 1.17 Job 39.17 Exode 36.2
27 Kwa maana kunde zile hazipurwi kwa chombo kikali, wala gurudumu la gari halipitishwi huko na huko juu ya jira ile, bali kunde zile hupurwa kwa fimbo, na jira ile kwa ufito.
Amos 1.3 Esaïe 27.7-27.8 Jérémie 46.28 Esaïe 41.15 Jérémie 10.24
28 Ngano ya mkate husagwa; kwa maana haipuri siku zote bila kukoma; na ingawa gurudumu la gari lake na farasi wake huitawanya ngano ile, haisagi.
Jean 12.24 Esaïe 21.10 1 Corinthiens 9.9-9.10 1 Corinthiens 3.9 Matthieu 13.37-13.43
29 Hayo nayo yatoka kwa Bwana wa majeshi, mwenye shauri la ajabu, apitaye wote kwa hekima yake.
Esaïe 9.6 Romains 11.33 Jérémie 32.19 Job 37.23 Daniel 4.2-4.3

Cette Bible est dans le domaine public.