Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 16.7
Bible en Swahili de l’est


1 Pelekeni wana-kondoo, kodi yake aitawalaye nchi toka Sela kuelekea jangwani, mpaka mlima wa binti Sayuni.
2 Rois 3.4 Esaïe 10.32 2 Rois 14.7 Esdras 7.17 Michée 4.8
2 Na binti za Moabu watakuwa kama ndege warukao huko na huko, kama kioto cha ndege waliotiwa hofu, kwenye vivuko vya Arnoni.
Proverbes 27.8 Juges 11.18 Esaïe 13.14 Deutéronome 2.36 Jérémie 48.20
3 Lete shauri; kata neno; fanya kivuli chako kuwa kama usiku kati ya mchana; wafiche waliofukuzwa; usiwachongee waliopotea.
Esaïe 32.2 Esaïe 25.4 1 Rois 18.4 Juges 9.15 Esaïe 1.17
4 Watu wangu waliofukuzwa waache wakae pamoja nawe; katika habari za Moabu, uwe sitara kwake mbele ya uso wake anayeharibu; maana yeye atozaye kwa nguvu amekoma; afanyaye ukiwa ametoweka; waliokanyaga watu wametoka katika nchi.
Esaïe 51.13 Esaïe 14.4 Malachie 4.3 Jérémie 21.12 Esaïe 33.1
5 Na kiti cha enzi kitafanywa imara kwa rehema; na mmoja ataketi juu yake katika kweli, katika hema ya Daudi; akifanya hukumu, akitaka sana yaliyo haki, mwepesi wa kutenda haki.
Daniel 7.14 Michée 4.7 Esaïe 32.1-32.2 Esaïe 9.6-9.7 Daniel 7.27
6 Tumesikia habari za kiburi cha Moabu, ya kwamba ni mwenye kiburi kingi; habari za majivuno yake, na kiburi chake, na ghadhabu yake; majivuno yake si kitu.
Amos 2.1 Jérémie 48.29-48.30 Abdias 1.3-1.4 Esaïe 28.15 1 Pierre 5.5
7 Kwa sababu hiyo Moabu atalia kwa ajili ya Moabu, kila mmoja atalia, maana mtaiombolezea mikate ya zabibu ya Kir-Haresethi, mkipigwa sana.
2 Rois 3.25 Jérémie 48.20 1 Chroniques 16.3 Esaïe 16.11 Esaïe 8.19
8 Maana makonde ya Heshboni yamenyauka, na mzabibu wa Sibma; mabwana wa mataifa wameyavunja matawi yake mateule; yamefika hata Yazeri, yalitanga-tanga hata nyikani; matawi yake yalitapakaa, yaliivuka bahari.
Nombres 32.38 Esaïe 15.4 Esaïe 10.7 2 Samuel 1.21 Jérémie 27.6-27.7
9 Basi, naililia mizabibu ya Sibma kwa kilio cha Yazeri, nitawanyeshea machozi yangu, Ee Heshboni na Eleale, kwa kuwa kelele za vita zimeyaangukia mavuno ya matunda yako, na mavuno ya mizabibu yako.
Jérémie 40.12 Jérémie 40.10 Esaïe 15.4-15.5 Esaïe 9.3 Jérémie 48.32-48.34
10 Na furaha imeondolewa, na shangwe toka mashamba yaliyozaa sana; hapana kuimba katika mashamba ya mizabibu, wala sauti za furaha; akanyagaye hakanyagi divai katika mashinikizo; nimeikomesha sauti ya furaha yake akanyagaye.
Jérémie 48.33 Juges 9.27 Amos 5.11 Amos 5.17 Esaïe 24.7-24.9
11 Kwa sababu hiyo mtima wangu unamlilia Moabu kama kinubi, na matumbo yangu kwa ajili ya Kir-Heresi.
Esaïe 15.5 Jérémie 48.36 Esaïe 63.15 Osée 11.8 Philippiens 2.1
12 Tena itakuwa, Moabu akionekana, na kujichosha kwa kulia juu ya mahali pa juu, na kuingia katika patakatifu pake aombe, hatapata kushinda.
Esaïe 15.2 Nombres 23.14 1 Rois 18.29 Nombres 23.28 Nombres 22.39
13 Hilo ndilo neno lile alilolisema Bwana juu ya Moabu zamani.
Esaïe 44.8
14 Lakini sasa Bwana asema hivi, Katika muda wa miaka mitatu, kama miaka ya mtu wa mshahara, utukufu wa Moabu utadharauliwa, pamoja na wingi wake wote; mabaki yake yatakuwa machache sana, kama si kitu kabisa.
Esaïe 21.16 Esaïe 17.4 Esaïe 23.9 Jérémie 48.42 Esaïe 15.5

Cette Bible est dans le domaine public.