Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Cantique 2.8
Bible en Swahili de l’est


1 Mimi ni ua la uwandani, Ni nyinyoro ya mabondeni.
Cantique 5.13 Osée 14.5 Esaïe 35.1-35.2 Cantique 2.16 Psaumes 85.11

Le jeune homme

2 Kama nyinyoro kati ya miiba, Kadhalika mpenzi wangu kati ya binti.
Matthieu 10.16 Esaïe 55.13 Matthieu 6.28-6.29 1 Pierre 2.12 Philippiens 2.15-2.16

La jeune femme

3 Kama mpera kati ya miti ya msituni, Kadhalika mpendwa wangu kati ya vijana. Naliketi kivulini mwake kwa furaha, Na matunda yake naliyaonja kuwa matamu.
Cantique 8.5 Esaïe 32.2 Hébreux 1.1-1.6 Esaïe 25.4 Psaumes 89.6
4 Akanileta mpaka nyumba ya karamu, Na bendera yake juu yangu ni mapenzi.
Cantique 1.4 Psaumes 63.2-63.5 Cantique 6.4 Jean 15.9-15.15 Romains 8.28-8.39
5 Nishibisheni zabibu, niburudisheni kwa mapera, Kwa maana nimezimia kwa mapenzi.
Cantique 5.8 2 Samuel 6.19 Osée 3.1 Luc 24.32 Cantique 7.8
6 Mkono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu, Nao wa kuume unanikumbatia!
Sophonie 3.17 Esaïe 54.5-54.10 Jérémie 32.41 Jean 3.29 Ephésiens 5.25-5.29

Le jeune homme

7 Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe.
Cantique 3.5 Cantique 8.4 Cantique 1.5 Cantique 5.8-5.9 Matthieu 26.63

La jeune femme

8 Sikiliza! Ni mpendwa wangu! Tazama, anakuja, Akiruka milimani, akichachawa vilimani.
Cantique 2.17 Apocalypse 3.20 Esaïe 40.3-40.4 Esaïe 55.12-55.13 Jean 10.4-10.5
9 Mpendwa wangu ni kama paa, au ayala. Tazama, asimama nyuma ya ukuta wetu, Achungulia dirishani, atazama kimiani.
Cantique 8.14 Cantique 2.17 Colossiens 2.17 Luc 24.35 1 Pierre 1.10-1.12
10 Mpendwa wangu alinena, akaniambia, Ondoka, mpenzi wangu, mzuri wangu, uje zako,
Cantique 2.13 Apocalypse 19.7-19.9 Apocalypse 22.17 2 Samuel 23.3 Psaumes 45.10-45.11
11 Maana tazama, kaskazi imepita, Masika imekwisha, imekwenda zake;
Ecclésiaste 3.4 Ephésiens 5.8 Esaïe 60.1-60.2 Esaïe 12.1-12.2 Matthieu 5.4
12 Maua yatokea katika nchi, Wakati wa kupelea umefika, Na sauti ya mwigo husikiwa kwetu.
Ephésiens 5.18-5.20 Cantique 6.11 Romains 15.9-15.13 Colossiens 3.16 Cantique 6.2
13 Mtini wapevusha tini zake, Na mizabibu inachanua, Inatoa harufu yake nzuri; Ondoka, mpenzi wangu, mzuri wangu, uje zako.
Cantique 2.10 Cantique 7.8 Luc 19.42 Esaïe 55.10-55.11 Cantique 7.11-7.13
14 Hua wangu, mafichoni mwa jabali, Katika sitara za magenge, Nitazame uso wako, nisikie sauti yako, Maana sauti yako ni tamu na uso wako mzuri.
Cantique 8.13 Cantique 1.5 Cantique 5.2 Exode 3.6 Exode 33.22-33.23
15 Tukamatie mbweha, Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu, Maana mizabibu yetu yachanua.
Luc 13.32 Cantique 7.12 Ezéchiel 13.4-13.16 Apocalypse 2.2 2 Pierre 2.1-2.3
16 Mpendwa wangu ni wangu, na mimi ni wake; Hulisha kundi lake penye nyinyoro.
Cantique 6.3 Cantique 7.10 Cantique 4.5 Psaumes 63.1 1 Corinthiens 3.21-3.23
17 Hata jua lipunge, na vivuli vikimbie, Unigeukie, mpendwa wangu, Nawe uwe kama paa, au ayala, Juu ya milima ya Betheri.
Cantique 4.6 Hébreux 10.1 Hébreux 8.5 Luc 1.78 Cantique 2.8-2.9

Cette Bible est dans le domaine public.