Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Cantique 2.4
Bible en Swahili de l’est


1 Mimi ni ua la uwandani, Ni nyinyoro ya mabondeni.
Esaïe 35.1-35.2 Cantique 5.13 Osée 14.5 Cantique 6.3 Cantique 2.16

Le jeune homme

2 Kama nyinyoro kati ya miiba, Kadhalika mpenzi wangu kati ya binti.
Matthieu 10.16 Esaïe 55.13 Matthieu 6.28-6.29 1 Pierre 2.12 Philippiens 2.15-2.16

La jeune femme

3 Kama mpera kati ya miti ya msituni, Kadhalika mpendwa wangu kati ya vijana. Naliketi kivulini mwake kwa furaha, Na matunda yake naliyaonja kuwa matamu.
Cantique 8.5 Esaïe 25.4 Esaïe 32.2 Hébreux 1.1-1.6 Ezéchiel 47.12
4 Akanileta mpaka nyumba ya karamu, Na bendera yake juu yangu ni mapenzi.
Cantique 1.4 Esaïe 11.10 Apocalypse 3.20 Cantique 1.1 Job 1.10
5 Nishibisheni zabibu, niburudisheni kwa mapera, Kwa maana nimezimia kwa mapenzi.
Cantique 5.8 Osée 3.1 2 Samuel 6.19 1 Chroniques 16.3 Esaïe 26.8-26.9
6 Mkono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu, Nao wa kuume unanikumbatia!
Sophonie 3.17 Esaïe 54.5-54.10 Jérémie 32.41 Esaïe 62.4-62.5 Jean 3.29

Le jeune homme

7 Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe.
Cantique 3.5 Cantique 8.4 Cantique 1.5 Cantique 5.8-5.9 Cantique 5.16

La jeune femme

8 Sikiliza! Ni mpendwa wangu! Tazama, anakuja, Akiruka milimani, akichachawa vilimani.
Esaïe 49.11-49.13 Jean 10.27 Luc 3.4-3.6 Jean 3.29 Actes 3.8
9 Mpendwa wangu ni kama paa, au ayala. Tazama, asimama nyuma ya ukuta wetu, Achungulia dirishani, atazama kimiani.
Cantique 8.14 Cantique 2.17 Apocalypse 19.10 2 Corinthiens 3.13-3.18 Jean 5.39
10 Mpendwa wangu alinena, akaniambia, Ondoka, mpenzi wangu, mzuri wangu, uje zako,
Cantique 2.13 Matthieu 4.19-4.22 Psaumes 85.8 Cantique 5.2 Matthieu 9.9
11 Maana tazama, kaskazi imepita, Masika imekwisha, imekwenda zake;
Esaïe 40.2 Ecclésiaste 3.11 Esaïe 54.6-54.8 Ecclésiaste 3.4 Ephésiens 5.8
12 Maua yatokea katika nchi, Wakati wa kupelea umefika, Na sauti ya mwigo husikiwa kwetu.
Esaïe 35.1-35.2 Esaïe 55.12 Esaïe 42.10-42.12 Ephésiens 1.13-1.14 Osée 14.5-14.7
13 Mtini wapevusha tini zake, Na mizabibu inachanua, Inatoa harufu yake nzuri; Ondoka, mpenzi wangu, mzuri wangu, uje zako.
Cantique 2.10 2 Corinthiens 5.20 Esaïe 18.5 Luc 13.6-13.7 Aggée 2.19
14 Hua wangu, mafichoni mwa jabali, Katika sitara za magenge, Nitazame uso wako, nisikie sauti yako, Maana sauti yako ni tamu na uso wako mzuri.
Cantique 8.13 Cantique 1.5 Esdras 9.5-9.6 Jérémie 49.16 Cantique 5.2
15 Tukamatie mbweha, Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu, Maana mizabibu yetu yachanua.
Cantique 2.13 Luc 13.32 Cantique 7.12 Ezéchiel 13.4-13.16 Apocalypse 2.2
16 Mpendwa wangu ni wangu, na mimi ni wake; Hulisha kundi lake penye nyinyoro.
Cantique 6.3 Cantique 7.10 Cantique 4.5 Galates 2.20 Jérémie 31.33
17 Hata jua lipunge, na vivuli vikimbie, Unigeukie, mpendwa wangu, Nawe uwe kama paa, au ayala, Juu ya milima ya Betheri.
Cantique 4.6 Cantique 8.14 Romains 13.12 Hébreux 10.1 Hébreux 8.5

Cette Bible est dans le domaine public.