Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ecclésiaste 1.18
Bible en Swahili de l’est


Examen de la réalité

Le cycle de la vie

1 Maneno ya Mhubiri mwana wa Daudi,mfalme katika Yerusalemu.
Ecclésiaste 1.12 Ecclésiaste 7.27 Ecclésiaste 12.8-12.10 Psaumes 40.9 Néhémie 6.7
2 Mhubiri asema, Ubatili mtupu, ubatili mtupu, mambo yote ni ubatili.
Romains 8.20 Ecclésiaste 12.8 Psaumes 144.4 Psaumes 39.5-39.6 Psaumes 62.9-62.10
3 Mtu ana faida gani ya kazi yake yote aifanyayo chini ya jua?
Ecclésiaste 2.22 Ecclésiaste 3.9 Ecclésiaste 5.16 Ecclésiaste 2.11 Jean 6.27
4 Kizazi huenda, kizazi huja; nayo dunia hudumu daima.
Psaumes 104.5 Matthieu 24.35 Zacharie 1.5 2 Pierre 3.10-3.13 Ecclésiaste 6.12
5 Jua lachomoza, na jua lashuka, na kufanya haraka kwenda mahali pa maawio yake.
Habakuk 3.11 Psaumes 19.4-19.6 Genèse 8.22 Psaumes 42.1 Jérémie 33.20
6 Upepo huvuma kusi, hugeuka kuwa kaskazi; hugeuka daima katika mwendo wake, na upepo huyarudia mazunguko yake.
Jean 3.8 Matthieu 7.24 Psaumes 107.25 Psaumes 107.29 Actes 27.13-27.15
7 Mito yote huingia baharini, walakini bahari haijai; huko iendako mito, ndiko irudiko tena.
Job 38.10-38.11 Psaumes 104.6-104.9
8 Mambo yote yamejaa uchovu usioneneka, jicho halishibi kuona, wala sikio halikinai kusikia.
Proverbes 27.20 Ecclésiaste 4.8 Matthieu 11.28 Apocalypse 7.16-7.17 Ecclésiaste 4.1-4.4
9 Yaliyokuwako ndiyo yatakayokuwako; na yaliyotendeka ndiyo yatakayotendeka; wala jambo jipya hakuna chini ya jua.
Ecclésiaste 3.15 Jérémie 31.22 Apocalypse 21.1 Ecclésiaste 7.10 2 Pierre 2.1
10 Je! Kuna jambo lo lote ambalo watu husema juu yake, Tazama, ni jambo jipya? Limekwisha kuwako, tangu zamani za kale zilizokuwa kabla yetu sisi.
Matthieu 23.30-23.32 Matthieu 5.12 Luc 17.26-17.30 Actes 7.51 1 Thessaloniciens 2.14-2.16
11 Hakuna kumbukumbu lo lote la vizazi vilivyotangulia; wala hakutakuwa na kumbukumbu lo lote la vizazi vitakavyokuja, miongoni mwao wale watakaofuata baadaye.
Ecclésiaste 2.16 Esaïe 42.9 Ecclésiaste 9.5 Psaumes 9.6 Esaïe 41.22-41.26

La sagesse humaine

12 Mimi, Mhubiri, nalikuwa Mfalme wa Israeli katika Yerusalemu.
Ecclésiaste 1.1 1 Rois 4.1-4.19
13 Nikatia moyo wangu ili kuyatafuta yote yanayotendeka chini ya mbingu, na kuyavumbua kwa hekima; ni taabu kubwa ambayo Mungu amewapa wanadamu, ili kutaabika ndani yake.
Ecclésiaste 3.10 Genèse 3.19 Ecclésiaste 1.17 Ecclésiaste 8.16-8.17 Ecclésiaste 7.25
14 Nimeziona kazi zote zifanywazo chini ya jua; na, tazama, mambo yote ni ubatili na kujilisha upepo.
Ecclésiaste 2.17 Ecclésiaste 2.11 Ecclésiaste 2.26 Ecclésiaste 6.9 Ecclésiaste 1.17-1.18
15 Yaliyopotoka hayawezi kunyoshwa, Wala yasiyokuwapo hayahesabiki.
Ecclésiaste 7.12-7.13 Esaïe 40.4 Ecclésiaste 3.14 Job 11.6 Matthieu 6.27
16 Nikatafakari nikisema, Nimejipatia hekima nyingi kupita wote walionitangulia katika Yerusalemu; naam, moyo wangu umeona kwa wingi hekima na maarifa.
Ecclésiaste 2.9 1 Rois 4.30 1 Rois 10.7 1 Rois 3.12-3.13 2 Chroniques 9.22-9.23
17 Nikatia moyo wangu ili kuijua hekima, na kujua wazimu na upumbavu; nikatambua ya kwamba hayo yote nayo ni kujilisha upepo.
Ecclésiaste 2.3 1 Thessaloniciens 5.21 Ecclésiaste 2.10-2.12 Ecclésiaste 1.13-1.14 Ecclésiaste 7.23-7.25
18 Yaani, Katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni,Naye aongezaye maarifa huongeza masikitiko.
1 Corinthiens 3.18-3.20 Ecclésiaste 12.12-12.13 Ecclésiaste 7.16 Ecclésiaste 2.15 Job 28.28

Cette Bible est dans le domaine public.