Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ecclésiaste 1.10
Bible en Swahili de l’est


Examen de la réalité

Le cycle de la vie

1 Maneno ya Mhubiri mwana wa Daudi,mfalme katika Yerusalemu.
Ecclésiaste 1.12 Ecclésiaste 7.27 Ecclésiaste 12.8-12.10 Néhémie 6.7 2 Chroniques 9.30
2 Mhubiri asema, Ubatili mtupu, ubatili mtupu, mambo yote ni ubatili.
Romains 8.20 Ecclésiaste 12.8 Psaumes 39.5-39.6 Psaumes 144.4 Psaumes 62.9-62.10
3 Mtu ana faida gani ya kazi yake yote aifanyayo chini ya jua?
Ecclésiaste 3.9 Ecclésiaste 5.16 Ecclésiaste 2.22 Ecclésiaste 2.11 Proverbes 23.4-23.5
4 Kizazi huenda, kizazi huja; nayo dunia hudumu daima.
Psaumes 104.5 Matthieu 24.35 Zacharie 1.5 Ecclésiaste 6.12 2 Pierre 3.10-3.13
5 Jua lachomoza, na jua lashuka, na kufanya haraka kwenda mahali pa maawio yake.
Habakuk 3.11 Psaumes 19.4-19.6 Jérémie 33.20 Josué 10.13-10.14 Psaumes 104.19-104.23
6 Upepo huvuma kusi, hugeuka kuwa kaskazi; hugeuka daima katika mwendo wake, na upepo huyarudia mazunguko yake.
Jean 3.8 Psaumes 107.29 Actes 27.13-27.15 Ecclésiaste 11.5 Jonas 1.4
7 Mito yote huingia baharini, walakini bahari haijai; huko iendako mito, ndiko irudiko tena.
Job 38.10-38.11 Psaumes 104.6-104.9
8 Mambo yote yamejaa uchovu usioneneka, jicho halishibi kuona, wala sikio halikinai kusikia.
Proverbes 27.20 Ecclésiaste 4.8 Matthieu 11.28 Ecclésiaste 4.1-4.4 Apocalypse 7.16-7.17
9 Yaliyokuwako ndiyo yatakayokuwako; na yaliyotendeka ndiyo yatakayotendeka; wala jambo jipya hakuna chini ya jua.
Ecclésiaste 3.15 Jérémie 31.22 Apocalypse 21.1 Ecclésiaste 2.12 Ecclésiaste 6.10
10 Je! Kuna jambo lo lote ambalo watu husema juu yake, Tazama, ni jambo jipya? Limekwisha kuwako, tangu zamani za kale zilizokuwa kabla yetu sisi.
Luc 17.26-17.30 Actes 7.51 Matthieu 23.30-23.32 Matthieu 5.12 1 Thessaloniciens 2.14-2.16
11 Hakuna kumbukumbu lo lote la vizazi vilivyotangulia; wala hakutakuwa na kumbukumbu lo lote la vizazi vitakavyokuja, miongoni mwao wale watakaofuata baadaye.
Ecclésiaste 2.16 Ecclésiaste 9.5 Psaumes 9.6 Esaïe 41.22-41.26 Esaïe 42.9

La sagesse humaine

12 Mimi, Mhubiri, nalikuwa Mfalme wa Israeli katika Yerusalemu.
Ecclésiaste 1.1 1 Rois 4.1-4.19
13 Nikatia moyo wangu ili kuyatafuta yote yanayotendeka chini ya mbingu, na kuyavumbua kwa hekima; ni taabu kubwa ambayo Mungu amewapa wanadamu, ili kutaabika ndani yake.
Ecclésiaste 3.10 Genèse 3.19 Ecclésiaste 1.17 Ecclésiaste 8.16-8.17 Ecclésiaste 7.25
14 Nimeziona kazi zote zifanywazo chini ya jua; na, tazama, mambo yote ni ubatili na kujilisha upepo.
Ecclésiaste 2.11 Ecclésiaste 2.17 Ecclésiaste 2.26 Ecclésiaste 1.17-1.18 Ecclésiaste 4.4
15 Yaliyopotoka hayawezi kunyoshwa, Wala yasiyokuwapo hayahesabiki.
Esaïe 40.4 Ecclésiaste 7.12-7.13 Ecclésiaste 3.14 Matthieu 6.27 Daniel 4.35
16 Nikatafakari nikisema, Nimejipatia hekima nyingi kupita wote walionitangulia katika Yerusalemu; naam, moyo wangu umeona kwa wingi hekima na maarifa.
Ecclésiaste 2.9 1 Rois 4.30 1 Rois 10.7 1 Rois 3.12-3.13 Psaumes 77.6
17 Nikatia moyo wangu ili kuijua hekima, na kujua wazimu na upumbavu; nikatambua ya kwamba hayo yote nayo ni kujilisha upepo.
Ecclésiaste 2.3 Ecclésiaste 2.10-2.12 1 Thessaloniciens 5.21 Ecclésiaste 7.23-7.25 Ecclésiaste 1.13-1.14
18 Yaani, Katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni,Naye aongezaye maarifa huongeza masikitiko.
1 Corinthiens 3.18-3.20 Ecclésiaste 12.12-12.13 Job 28.28 Ecclésiaste 2.23 Ecclésiaste 7.16

Cette Bible est dans le domaine public.