Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 24.4
Bible en Swahili de l’est


Moïse sur le mont Sinaï

1 Kisha Bwana akamwambia Musa, Kweeni wewe, na Haruni, na Nadabu, na Abihu, na watu sabini wa wazee wa Israeli, mkamfikilie Bwana; mkasujudie kwa mbali;
Nombres 11.16 Exode 6.23 Exode 28.1 Lévitique 10.1-10.2 Exode 19.24
2 na Musa peke yake ndiye atakayekaribia karibu na Bwana; lakini hao hawatakaribia karibu; wala hao watu hawatakwea pamoja naye.
Exode 24.13 Exode 24.15 Exode 24.18 Jérémie 49.19 Nombres 16.5
3 Musa akaenda akawaambia watu maneno yote ya Bwana, na hukumu zake zote; watu wote wakajibu kwa sauti moja, wakasema, Maneno yote aliyoyanena Bwana tutayatenda.
Exode 19.8 Exode 24.7 Deutéronome 4.5 Galates 3.19-3.20 Josué 24.22
4 Basi Musa akayaandika maneno yote ya Bwana, akaondoka asubuhi na mapema, akajenga madhabahu chini ya mlima, na nguzo kumi na mbili, kwa hesabu ya kabila kumi na mbili za Israeli,
Deutéronome 31.9 Genèse 28.18 Genèse 31.45 1 Rois 11.30 Exode 20.24-20.26
5 akapeleka vijana wa wana wa Israeli, waliotoa sadaka za kuteketezwa, wakamchinjia Bwana sadaka za amani za ng’ombe.
Exode 18.12 Exode 19.22 Lévitique 7.11-7.21 Lévitique 1.1-1.17 Lévitique 3.1-3.17
6 Musa akatwaa nusu ya ile damu, akaitia katika mabakuli; na nusu ya ile damu akainyunyiza juu ya madhabahu.
Hébreux 9.18 Exode 29.16 Colossiens 1.20 Lévitique 3.8 1 Pierre 1.2
7 Kisha akakitwaa kitabu cha agano akakisoma masikioni mwa watu; wakasema, Hayo yote aliyoyanena Bwana tutayatenda, nasi tutatii.
Exode 24.3-24.4 1 Thessaloniciens 5.27 Hébreux 9.18-9.23 Jérémie 7.23-7.24 Actes 13.15
8 Musa akaitwaa ile damu, akawanyunyizia watu, akasema, Hii ndiyo damu ya agano alilolifanya Bwana pamoja nanyi katika maneno haya yote.
Hébreux 13.20 1 Pierre 1.2 Matthieu 26.28 Zacharie 9.11 Luc 22.20
9 Ndipo akakwea juu, Musa, na haruni, na Nadabu, na Abihu, na watu sabini miongoni mwa wazee wa Israeli;
Exode 24.1
10 wakamwona Mungu wa Israeli; chini ya miguu yake palikuwa na kama sakafu iliyofanyizwa kwa yakuti samawi, kama zile mbingu zenyewe kwa usafi wake.
Jean 1.18 Ezéchiel 10.1 Apocalypse 4.3 Exode 33.20 Matthieu 17.2
11 Naye hakuweka mkono wake juu ya hao wakuu wa wana wa Israeli; nao wakamwona Mungu, wakala na kunywa.
Exode 18.12 Genèse 16.13 Exode 19.21 Genèse 31.54 Exode 24.1
12 Bwana akamwambia Musa, Njoo huku juu kwangu mlimani, uwe huku; nami nitakupa mbao za mawe na ile sheria na hiyo amri niliyoiandika ili uwafundishe.
Exode 32.15-32.16 Deutéronome 5.22 Exode 31.18 Exode 24.18 Exode 24.15
13 Musa akaondoka na Yoshua, mtumishi wake, Musa akapanda mlimani kwa Mungu.
Exode 33.11 Exode 3.1 Exode 17.9-17.14 Exode 32.17 Nombres 11.28
14 Akawaambia hao wazee, Tungojeeni hapa, mpaka tutakaporudi kwenu; na tazameni, Haruni na Huri wapo pamoja nanyi; kila mtu aliye na neno na awaendee.
Exode 17.10 Exode 17.12 Genèse 22.5 1 Samuel 10.8 Exode 18.25-18.26
15 Musa akapanda mlimani, lile wingu likaufunikiza mlima.
Exode 19.9 Matthieu 17.5 Exode 19.16 2 Chroniques 6.1
16 Na huo utukufu wa Bwana ukakaa juu ya mlima wa Sinai; lile wingu likaufunikiza siku sita; na siku ya saba akamwita Musa toka kati ya lile wingu.
Exode 16.10 Nombres 14.10 Lévitique 9.23 Nombres 16.42 Psaumes 99.7
17 Na kuonekana kwake ule utukufu wa Bwana kulikuwa kama moto uteketezao, juu ya mlima machoni pa wana wa Israeli.
Exode 3.2 Hébreux 12.29 Deutéronome 4.36 Hébreux 12.18 Deutéronome 4.24
18 Musa akaingia ndani ya lile wingu, akapanda mlimani; Musa akawa humo katika ule mlima siku arobaini, mchana na usiku.
Deutéronome 9.9 Exode 34.28 Deutéronome 10.10 Deutéronome 9.25 Deutéronome 9.18

Cette Bible est dans le domaine public.