Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 19.2
Bible en Swahili de l’est


Conclusion de l’alliance

Alliance au mont Sinaï

1 Mwezi wa tatu baada ya kutoka Waisraeli katika nchi ya Misri, siku iyo hiyo wakafika jangwa la Sinai.
Exode 12.6 Nombres 33.15 Exode 16.1 Lévitique 23.16-23.18 Exode 12.2
2 Nao walipokuwa wameondoka Refidimu na kufika jangwa la Sinai, wakatua katika lile jangwa; Israeli wakapiga kambi huko wakiukabili mlima.
Exode 3.1 Exode 17.1 Exode 18.5 Exode 17.8 Exode 3.12
3 Musa akapanda kwa Mungu, na Bwana akamwita toka mlima ule, akisema, Utawaambia nyumba ya Yakobo, na kuwaarifu wana wa Israeli, maneno haya;
Exode 3.4 Actes 7.38 Exode 20.21 Exode 24.15-24.18 Deutéronome 5.5-5.31
4 Mmeona jinsi nilivyowatendea Wamisri, na jinsi nilivyowachukua ninyi juu ya mbawa za tai, nikawaleta ninyi kwangu mimi.
Esaïe 63.9 Deutéronome 29.2 Deutéronome 32.11-32.12 Apocalypse 12.14 Exode 7.1-7.14
5 Sasa basi ikiwa mtaitii sauti yangu kweli kweli, na kulishika agano langu, hapo ndipo mtakapokuwa tunu kwangu kuliko makabila yote ya watu; maana dunia yote pia ni mali yangu,
Deutéronome 14.2 Deutéronome 7.6 Deutéronome 5.2 Deutéronome 26.18 Job 41.11
6 nanyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu. Hayo ndiyo maneno utakayowaambia wana wa Israeli.
1 Pierre 2.9 Deutéronome 7.6 1 Pierre 2.5 Deutéronome 26.19 Esaïe 62.12
7 Musa akaenda akawaita wazee wa watu, akawafunulia maneno hayo yote, Bwana aliyokuwa amemwagiza.
Exode 4.29-4.30 1 Corinthiens 15.1 Exode 3.16
8 Watu wote wakaitika pamoja wakisema, Hayo yote aliyoyasema Bwana tutayatenda. Naye Musa akamwambia Bwana maneno ya hao watu.
Exode 24.3 Exode 24.7 Deutéronome 5.27-5.29 Néhémie 10.29 Exode 20.19
9 Bwana akamwambia Musa, Tazama, mimi naja kwako katika wingu zito ili watu hawa wasikie nitakaposema nawe, nao wapate kukuamini wewe nawe hata milele. Musa akamwambia Bwana hayo maneno ya watu.
Deutéronome 4.36 Deutéronome 4.11-4.12 Exode 24.15-24.16 Exode 19.16 Exode 14.31
10 Bwana akamwambia Musa, Enenda kwa watu hawa, ukawatakase leo na kesho, wakazifue nguo zao,
Genèse 35.2 Lévitique 15.5 Lévitique 11.44-11.45 Nombres 8.7 Josué 3.5
11 wawe tayari kwa siku ya tatu; maana siku ya tatu Bwana atashuka katika mlima wa Sinai machoni pa watu hawa wote.
Exode 19.16 Deutéronome 33.2 Exode 34.5 Psaumes 18.9 Exode 3.8
12 Nawe utawawekea mipaka watu hawa pande zote, ukisema, Jihadharini, msipande mlima huu, wala msiuguse, hata mapambizo yake; kila mtu atakayeugusa mlima huu, bila shaka atauawa.
Hébreux 12.20-12.21 Exode 34.12 Deutéronome 2.4 Exode 10.28 Exode 19.21
13 Mkono wa mtu awaye yote usimguse mtu huyo, ila hakika yake atapigwa kwa mawe, au kupigwa kwa mkuki; kwamba ni mnyama au kwamba ni mwanadamu, hataishi. Hapo panda itakapotoa sauti kwa kufuliza ndipo watakapoukaribia mlima.
Exode 19.16 Hébreux 12.20 Exode 19.19 1 Corinthiens 15.52 Lévitique 20.15-20.16
14 Musa akatelemka mlimani akawaendea watu akawatakasa, nao wakafua nguo zao.
Exode 19.10
15 Akawaambia watu; Mwe tayari siku ya tatu; msimkaribie mwanamke.
1 Samuel 21.4-21.5 Exode 19.11 1 Corinthiens 7.5 Malachie 3.2 2 Pierre 3.11-3.12
16 Ikawa siku ya tatu, wakati wa asubuhi, palikuwa na ngurumo na umeme, na wingu zito juu ya mlima, na sauti ya baragumu iliyolia sana. Watu wote waliokuwa kituoni wakatetemeka.
Hébreux 12.21 Hébreux 12.18-12.19 Apocalypse 4.1 Exode 20.18 Apocalypse 4.5
17 Musa akawatoa hao watu katika kituo, akawaleta ili waonane na Mungu; wakasimama pande za chini za kile kilima.
Deutéronome 4.10 Deutéronome 5.5
18 Mlima wa Sinai wote pia ukatoa moshi, kwa sababu Bwana alishuka katika moto; na ule moshi wake ukapanda juu kama moshi wa tanuu, mlima wote ukatetemeka sana.
Psaumes 144.5 Apocalypse 15.8 Juges 5.5 Exode 24.17 Psaumes 104.32
19 Na hapo sauti ya baragumu ilipozidi kulia sana, Musa akanena, naye Mungu akamwitikia kwa sauti.
Psaumes 81.7 Exode 19.16 Hébreux 12.21 Néhémie 9.13 Exode 19.13
20 Bwana akaushukia mlima, juu ya kilele cha mlima; Bwana akamwita Musa aende hata kilele cha mlima; Musa akapanda juu.
Néhémie 9.13 Exode 24.12-24.13 Exode 24.18 Exode 34.2 Exode 34.4
21 Ndipo Bwana akamwambia Musa, Shuka chini, uwaonye watu wasije wakapasua njia waje kwa Bwana kutazama, kisha wengi miongoni mwao wakaangamia.
1 Samuel 6.19 Exode 3.5 Hébreux 12.28-12.29 Exode 19.12-19.13 Ecclésiaste 5.1
22 Makuhani nao, wamkaribiao Bwana, na wajitakase, Bwana asije akawafurikia.
Exode 24.5 2 Chroniques 30.3 2 Chroniques 30.18-30.19 1 Chroniques 15.13 1 Corinthiens 11.30-11.32
23 Musa akamwambia Bwana, Watu hawa hawawezi kuukaribia mlima wa Sinai; kwa kuwa wewe ulituusia, ukisema, Wekeni mipaka kando-kando ya mlima, na kuutenga.
Exode 19.12 Josué 3.4-3.5
24 Bwana akamwambia, Nenda, ushuke wewe; nawe utakwea, wewe, na Haruni pamoja nawe; lakini wale makuhani na watu wasipenye kumkaribia Bwana, asije yeye akawafurikia juu yao.
Exode 19.12 Galates 3.10-3.11 Romains 4.15 Luc 16.16 Exode 24.9
25 Basi Musa akawatelemkia hao watu na kuwaambia hayo.

Cette Bible est dans le domaine public.