Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 18.20
Bible en Swahili de l’est


Visite de Jéthro, le beau-père de Moïse

1 Basi Yethro, kuhani wa Midiani, mkwewe Musa, alisikia habari ya mambo hayo yote Mungu aliyokuwa amemtendea Musa, na Waisraeli watu wake, jinsi Bwana alivyowaleta Israeli watoke Misri.
Exode 2.16 Exode 3.1 Psaumes 77.14-77.15 Josué 2.10 Jérémie 33.9
2 Ndipo Yethro mkwewe Musa akamtwaa Sipora, mke wa Musa, baada ya yeye kumrudisha,
Exode 2.21 Exode 4.25-4.26
3 pamoja na wanawe wawili; katika hao, jina la mmoja ni Gershomu, maana alisema, Mimi nimekuwa mgeni katika nchi ya ugenini;
Exode 2.22 Actes 7.29 Psaumes 39.12 Hébreux 11.13 Exode 4.20
4 na jina la wa pili ni Eliezeri, kwa kuwa alisema, Yeye Mungu wa baba yangu alikuwa msaada wangu, akaniokoa na upanga wa Farao.
1 Chroniques 23.15 2 Timothée 4.17 Esaïe 50.7-50.9 2 Corinthiens 1.8-1.10 Psaumes 46.1
5 Basi Yethro, mkwewe Musa, pamoja na mke wa Musa na wanawe wawili wakamwendea Musa huko nyikani, hapo alipokuwa amepanga, kwenye mlima wa Mungu;
Exode 3.1 Exode 3.12 Exode 19.11 1 Rois 19.8 Exode 24.16-24.17
6 naye akamwambia Musa, Mimi Yethro mkweo nimekuja kwako, na mkeo, na wanawe wawili pamoja naye.
7 Basi Musa akatoka nje ili amlaki mkwewe, akasujudia na kumbusu; nao wakaulizana habari; kisha wakaingia hemani.
Genèse 29.13 2 Samuel 11.7 Genèse 14.17 Genèse 19.1 Genèse 18.2
8 Musa akamwambia mkwewe mambo hayo yote Bwana aliyomtenda Farao na Wamisri kwa ajili ya Israeli, na mambo mazito yote yaliyowapata njiani, na jinsi Bwana alivyowaokoa.
Psaumes 78.42-78.43 Psaumes 106.10 Psaumes 81.7 Nombres 20.14 Néhémie 9.9-9.15
9 Yethro alifurahi kwa ajili ya wema wote Bwana aliowatendea Israeli, kwa alivyo waokoa mikononi mwa Wamisri.
Esaïe 66.10 Romains 12.15 Esaïe 44.23 1 Corinthiens 12.26 Romains 12.10
10 Kisha Yethro akasema, Na ahimidiwe Bwana aliyewaokoa na mikono ya Wamisri, na mkono wa Farao; aliyewaokoa watu hao watoke mikononi mwa Wamisri.
Genèse 14.20 2 Samuel 18.28 Luc 1.68 Psaumes 68.19-68.20 Apocalypse 5.11-5.13
11 Sasa najua ya kuwa Bwana ni mkuu kuliko miungu yote; naam, katika jambo hilo walilowatenda kwa unyeti.
2 Chroniques 2.5 Exode 15.11 Psaumes 95.3 Luc 1.51 Daniel 4.37
12 Yethro mkwewe Musa akamletea Mungu sadaka ya kuteketezwa na dhabihu; na Haruni akaja, na wazee wote wa Israeli, wale chakula pamoja na mkwewe Musa mbele za Mungu.
Genèse 31.54 Deutéronome 12.7 Exode 24.5 Exode 24.11 Lévitique 7.11-7.17
13 Asubuhi yake Musa akaketi ili awapishie hukumu watu; na hao watu wakasimama kumzunguka Musa tangu asubuhi hata jioni.
Romains 12.8 Romains 13.6 Matthieu 23.2 Job 29.7 Esaïe 16.5
14 Mkwewe Musa alipoyaona yote aliyowafanyia watu, akasema, Ni jambo gani hili uwatendealo hao watu? Kwani wewe kuketi hapo peke yako, na watu wote kusimama kwako tangu asubuhi hata jioni?
15 Musa akamwambia mkwewe, Ni kwa sababu watu hunijilia mimi wapate kumwuliza Mungu;
Nombres 15.34 Nombres 27.5 Exode 18.19-18.20 Nombres 9.6 Nombres 9.8
16 wakiwa na neno, hunijilia; nami naamua kati ya mtu na mwenziwe, nami nawajuvisha amri za Mungu, na sheria zake.
Exode 24.14 2 Samuel 15.3 Deutéronome 5.1 Deutéronome 4.5 1 Corinthiens 6.1
17 Mkwewe Musa akamwambia, Jambo hili ufanyalo si jema.
18 Huna budi utadhoofika wewe, na hawa watu walio pamoja nawe pia; maana jambo hili ni zito mno kwako; huwezi wewe kulitenda peke yako.
Actes 6.1-6.4 Nombres 11.14-11.17 1 Thessaloniciens 2.8-2.9 Philippiens 2.30 2 Corinthiens 12.15
19 Sikiza sasa neno langu, nitakupa shauri, na Mungu na awe pamoja nawe; uwe wewe kwa ajili ya watu mbele ya Mungu, nawe umletee Mungu maneno yao;
Nombres 27.5 Genèse 39.2 Deutéronome 5.5 Exode 3.12 Exode 20.19
20 nawe utawafundisha zile amri na sheria, nawe utawaonyesha njia ambayo inawapasa kuiendea, na kazi ambayo inawapasa kuifanya.
Deutéronome 5.1 Psaumes 143.8 Deutéronome 1.18 Deutéronome 4.1 Deutéronome 4.5
21 Zaidi ya hayo utajipatia katika watu hawa watu walio na uwezo, wenye kumcha Mungu, watu wa kweli, wenye kuchukia mapato ya udhalimu; ukawaweka juu yao, wawe wakuu wa maelfu, na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi;
Actes 6.3 2 Chroniques 19.5-19.10 Deutéronome 16.18-16.19 Genèse 42.18 Exode 18.25
22 nao wawaamue watu hawa sikuzote; kisha, kila neno lililo kubwa watakuletea wewe, lakini kila neno dogo wataliamua wenyewe; basi kwako wewe mwenyewe utapata nafasi zaidi, nao watauchukua huo mzigo pamoja nawe.
Nombres 11.17 Nombres 36.1 Nombres 27.2 Lévitique 24.11 Exode 18.26
23 Kwamba utafanya jambo hili, na Mungu akikuagiza hivyo, basi utaweza kusimama wewe, na watu hawa wote nao watakwenda mahali pao kwa amani.
Exode 18.18 Philippiens 1.24-1.25 2 Samuel 21.17 Galates 2.2 Genèse 18.33
24 Basi Musa akasikiza neno la mkwewe, akayafanya yote aliyokuwa amemwambia.
Esdras 10.2 Exode 18.2-18.5 Exode 18.19 1 Corinthiens 12.21 Proverbes 1.5
25 Musa akawachagua watu wenye uwezo katika Israeli yote, akawaweka wawe vichwa juu ya watu, wakuu wa maelfu, na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi.
Deutéronome 1.15 Exode 18.21 Actes 6.5
26 Nao wakawaamua watu sikuzote; mashauri magumu wakamletea Musa, lakini kila neno dogo wakaliamua wenyewe.
Exode 18.22 Exode 18.14-18.15 Deutéronome 17.8 1 Rois 3.16-3.28 Job 29.16
27 Kisha Musa akaagana na mkwewe; naye akaenda zake, mpaka nchi yake mwenyewe.
Nombres 10.29-10.30 Juges 19.9 Genèse 31.55 Genèse 24.59

Cette Bible est dans le domaine public.