Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 11.2
Bible en Swahili de l’est


Le pharaon averti de la mort des premiers-nés

1 Bwana akamwambia Musa, Liko pigo moja bado, nitakaloleta juu ya Farao na juu ya Misri; baadaye atawapa ninyi ruhusa mtoke huku; naye hapo atakapowapa ruhusa, atawafukuza mtoke huku kabisa kabisa.
Exode 12.31-12.39 Genèse 15.14 Exode 3.20 Deutéronome 4.34 Lévitique 26.21
2 Basi nena wewe masikioni mwa watu hawa, na kila mtu mume na atake kwa jirani yake, na kila mwanamke atake kwa jirani yake, vyombo vya fedha, na vyombo vya dhahabu.
Exode 3.22 Exode 12.35-12.36 Ezéchiel 16.10-16.13 Matthieu 20.15 Genèse 31.9
3 Bwana akawapa watu hao kibali machoni pa Wamisri. Zaidi ya hayo, huyo Musa alikuwa ni mkuu sana katika nchi ya Misri, machoni pa watumishi wa Farao, na machoni pa watu wake.
Exode 3.21 Exode 12.36 Psaumes 106.46 Genèse 12.2 2 Samuel 7.9
4 Musa akasema, Bwana asema hivi, Kama usiku wa manane mimi nitatoka nipite kati ya Misri;
Exode 12.29 Amos 4.10 Job 34.20 Exode 12.23 Amos 5.17
5 na wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri watakufa, tangu yule mzaliwa wa kwanza wa Farao aketiye katika kiti chake cha enzi, hata mzaliwa wa kwanza wa huyo kijakazi aliye pale nyuma ya jiwe la kusagia; na wazaliwa wa kwanza wote wa wanyama.
Psaumes 78.51 Exode 4.23 Psaumes 135.8 Matthieu 24.41 Exode 12.12
6 Ndipo kutakuwa na kilio kikuu katika nchi yote ya Misri, ambacho mfano wake haujakuwa bado majira yo yote, wala hautakuwako mfano wake tena kabisa.
Exode 12.30 Amos 5.17 Proverbes 21.13 Exode 3.7 Apocalypse 18.18-18.19
7 Lakini katika wana wa Israeli hapana hata mbwa atakayetoa ulimi juu yao, juu ya mtu wala juu ya mnyama; ili kwamba mpate kujua jinsi Bwana anavyowatenga Wamisri na Waisraeli.
Exode 8.22 Josué 10.21 Malachie 3.18 Exode 10.23 Exode 9.4
8 Tena hao watumishi wako wote watanitelemkia kwangu mimi, nao watanisujudia, wakisema, Toka wewe, na hawa watu wote wakufuatao; na baada ya hayo nitatoka. Basi akatoka kwa Farao na hasira kuu.
Exode 12.31-12.33 Psaumes 6.1 Esaïe 49.23 Juges 4.10 Ezéchiel 3.14
9 Bwana akamwambia Musa, Farao hatawasikiza ninyi; kusudi ajabu zangu ziongezeke katika nchi ya Misri.
Exode 7.3-7.4 Exode 3.19 Exode 10.1 Romains 9.16-9.18
10 Musa na Haruni walifanya ajabu hizo zote mbele ya Farao; Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, asiwape wana wa Israeli ruhusa watoke nchi yake.
Exode 4.21 Exode 10.20 Exode 10.27 Deutéronome 2.30 Romains 9.22

Cette Bible est dans le domaine public.