Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 59.11
Bible en Swahili de l’est


Prière pour le jugement des impies

1 Ee Mungu wangu, uniponye na adui zangu, Uniinue juu yao wanaoshindana nami.
1 Samuel 19.11-19.24 Psaumes 18.48 Psaumes 57.1 Psaumes 91.14 Juges 16.2-16.3
2 Uniponye nao wafanyao maovu, Uniokoe na watu wa damu.
Psaumes 139.19 Psaumes 26.9 Psaumes 27.2 Psaumes 55.23
3 Kwa maana wanaiotea nafsi yangu; Wenye nguvu wamenikusanyikia; Ee Bwana, si kwa kosa langu, Wala si kwa hatia yangu.
Psaumes 56.6 1 Samuel 24.11 Psaumes 69.4 1 Samuel 26.18 Michée 7.2
4 Bila kosa langu huenda mbio, hujiweka tayari; Uamke uonane nami, na kutazama.
Psaumes 35.23 Esaïe 51.9 Esaïe 59.7 1 Samuel 19.12-19.24 Psaumes 35.19
5 Na Wewe, Bwana, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, uamke. Uwapatilize mataifa yote; Usiwarehemu waovu wafanyao uovu hata mmoja.
Psaumes 7.12-7.13 Genèse 33.20 Ezéchiel 18.27-18.28 Romains 9.6 Exode 20.5
6 Wakati wa jioni hurudi, hulia kama mbwa, Na kuzunguka-zunguka mjini.
Psaumes 59.14 Psaumes 22.16 1 Samuel 19.11
7 Tazama, kwa vinywa vyao huteuka, Midomoni mwao mna panga, Kwa maana ni nani asikiaye?
Psaumes 57.4 Proverbes 15.2 Psaumes 10.11 Proverbes 12.18 Psaumes 73.11
8 Na Wewe, Bwana, utawacheka, Utawadhihaki mataifa yote.
Psaumes 2.4 Psaumes 37.13 Proverbes 1.26 1 Samuel 19.15-19.16 Matthieu 18.17
9 Ee nguvu zangu, nitakungoja Wewe, Maana Mungu ndiye aliye ngome yangu
Psaumes 9.9 Psaumes 62.2 Habakuk 3.19 Psaumes 20.1 Psaumes 27.14
10 Mungu wa fadhili zangu atanitangulia, Mungu atanijalia kuwatazama adui zangu.
Psaumes 54.7 Psaumes 21.3 Psaumes 59.17 1 Thessaloniciens 4.15 Romains 10.2-10.3
11 Usiwaue, watu wangu wasije wakasahau; Uwatawanye kwa uweza wako, Na kuwaangamiza, Ee Bwana, ngao yetu.
Psaumes 3.3 Deutéronome 30.3-30.4 Genèse 4.12-4.15 Apocalypse 9.6 Ezéchiel 12.15-12.16
12 Kwa dhambi ya kinywa chao, Na kwa neno la midomo yao, Wanaswe kwa kiburi chao, Kwa ajili ya kulaani na uongo wasemao.
Proverbes 12.13 Osée 4.2 Psaumes 10.2 Matthieu 12.36-12.37 Psaumes 120.3-120.4
13 Uwakomeshe kwa hasira, Uwakomeshe watoweke, Wajue ya kuwa Mungu atawala katika Yakobo, Na hata miisho ya dunia.
Psaumes 83.18 Psaumes 7.9 Daniel 4.25 1 Samuel 17.46-17.47 1 Rois 18.36-18.37
14 Wakati wa jioni hurudi, hulia kama mbwa, Na kuzunguka-zunguka mjini.
Psaumes 59.6 Psaumes 22.16
15 Watatanga-tanga hao wakitafuta chakula; Wasiposhiba watakesha usiku kucha.
Job 15.23 Psaumes 109.10 Esaïe 8.21 Lamentations 4.4-4.5 Job 30.1-30.7
16 Nami nitaziimba nguvu zako asubuhi, Nitaziimba fadhili zako kwa furaha. Kwa kuwa ndiwe uliyekuwa ngome yangu, Na makimbilio siku ya shida yangu.
Psaumes 21.13 Psaumes 101.1 Psaumes 143.8 Romains 15.9 Psaumes 5.3
17 Ee nguvu zangu, nitakuimbia kwa furaha, Maana Mungu ndiye aliye ngome yangu, Mungu wa fadhili zangu.
Psaumes 59.9-59.10 Psaumes 46.1 Psaumes 18.1

Cette Bible est dans le domaine public.