Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 30
Bible en Swahili de l’est


Louange après la délivrance

1 Ee Bwana, nitakutukuza kwa maana umeniinua, Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu.
Psaumes 25.2 Psaumes 35.19 Psaumes 13.4 Daniel 4.37 2 Samuel 5.11
2 Ee Bwana, Mungu wangu, Nalikulilia ukaniponya.
Psaumes 6.2 Psaumes 88.13 Exode 15.26 Psaumes 103.3-103.4 Psaumes 107.17-107.22
3 Umeniinua nafsi yangu, Ee Bwana, kutoka kuzimu. Umenihuisha na kunitoa Miongoni mwao washukao shimoni.
Psaumes 28.1 Psaumes 16.10 Psaumes 86.13 Psaumes 71.20 Psaumes 40.1-40.2
4 Mwimbieni Bwana zaburi, Enyi watauwa wake. Na kufanya shukrani. Kwa kumbukumbu la utakatifu wake.
Psaumes 97.12 1 Chroniques 16.4 Apocalypse 19.5-19.6 Psaumes 132.9 Esaïe 6.3
5 Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo, Katika radhi yake mna uhai. Huenda kilio huja kukaa usiku, Lakini asubuhi huwa furaha.
Esaïe 54.7-54.8 2 Corinthiens 4.17 Psaumes 103.9 Esaïe 26.20 Psaumes 6.6-6.9
6 Nami nilipofanikiwa nalisema, Sitaondoshwa milele.
Esaïe 56.12 Luc 12.19 2 Corinthiens 12.7 Psaumes 15.5 Esaïe 47.7
7 Bwana, kwa radhi yako Wewe uliuimarisha mlima wangu. Uliuficha uso wako, Nami nikafadhaika.
Psaumes 104.29 Psaumes 143.7 Deutéronome 31.17 Psaumes 89.17 Psaumes 5.12
8 Ee Bwana, nalikulilia Wewe, Naam, kwa Bwana naliomba dua.
Psaumes 34.6 Psaumes 130.1-130.2 Philippiens 4.6-4.7 1 Corinthiens 12.8-12.9 Psaumes 77.1-77.2
9 Mna faida gani katika damu yangu Nishukapo shimoni? Mavumbi yatakusifu? Yataitangaza kweli yako?
Psaumes 6.5 Esaïe 38.18 Ecclésiaste 9.10 Psaumes 88.10-88.12 Psaumes 115.17-115.18
10 Ee Bwana, usikie, unirehemu, Bwana, uwe msaidizi wangu.
Psaumes 54.4 Psaumes 27.7 Psaumes 143.7-143.9 Psaumes 51.1-51.2 Psaumes 28.7
11 Uligeuza matanga yangu kuwa machezo; Ulinivua gunia, ukanivika furaha.
Jérémie 31.4 Apocalypse 21.4 Psaumes 149.3 Ecclésiaste 3.4 Psaumes 150.4
12 Ili utukufu wangu ukusifu, Wala usinyamaze. Ee Bwana, Mungu wangu, Nitakushukuru milele.
Psaumes 16.9 Psaumes 57.8 Psaumes 146.1-146.2 Actes 4.20 Psaumes 13.6

Cette Bible est dans le domaine public.