Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 27
Bible en Swahili de l’est


Le triomphe de la foi

1 Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani?
Psaumes 118.6 Hébreux 13.6 Exode 15.2 2 Corinthiens 12.9 Esaïe 60.19-60.20
2 Watenda mabaya waliponikaribia, Wanile nyama yangu, Watesi wangu na adui zangu, Walijikwaa wakaanguka.
Psaumes 14.4 Jean 18.3-18.6 Job 19.22 Psaumes 118.12 Psaumes 53.4
3 Jeshi lijapojipanga kupigana nami, Moyo wangu hautaogopa. Vita vijaponitokea, Hata hapo nitatumaini.
Psaumes 3.6 Philippiens 1.28 Esaïe 41.11-41.12 1 Samuel 28.15-28.16 Apocalypse 12.7-12.11
4 Neno Moja nimelitaka kwa Bwana, Nalo ndilo nitakalolitafuta, Nikae nyumbani mwa Bwana Siku zote za maisha yangu, Niutazame uzuri wa Bwana, Na kutafakari hekaluni mwake.
Psaumes 26.8 Psaumes 23.6 Psaumes 65.4 Psaumes 84.10 Psaumes 84.4
5 Mradi atanisitiri bandani mwake siku ya mabaya, Atanisitiri katika sitara ya hema yake, Na kuniinua juu ya mwamba.
Psaumes 31.20 Psaumes 40.2 Psaumes 91.1 Psaumes 138.7 Psaumes 50.15
6 Na sasa kichwa changu kitainuka Juu ya adui zangu wanaonizunguka. Nami nitatoa dhabihu za shangwe hemani mwake; Nitaimba, naam, nitamhimidi Bwana.
Psaumes 3.3 Psaumes 107.22 Esaïe 12.6 Hébreux 13.15 Zacharie 9.9
7 Ee Bwana, usikie, kwa sauti yangu ninalia, Unifadhili, unijibu.
Psaumes 13.3 Psaumes 130.2-130.4 Psaumes 5.2 Psaumes 4.1 Psaumes 143.1-143.2
8 Uliposema, Nitafuteni uso wangu, Moyo wangu umekuambia, Bwana, uso wako nitautafuta.
Psaumes 105.4 Jérémie 29.12-29.13 Psaumes 119.58 Psaumes 63.1-63.2 Psaumes 24.6
9 Usinifiche uso wako, Usijiepushe na mtumishi wako kwa hasira. Umekuwa msaada wangu, usinitupe, Wala usiniache, Ee Mungu wa wokovu wangu.
Psaumes 69.17 Psaumes 102.2 Psaumes 143.7 Psaumes 24.5 Psaumes 44.24
10 Baba yangu na mama yangu wameniacha, Bali Bwana atanikaribisha kwake.
Esaïe 49.15 Esaïe 40.11 2 Timothée 4.16 Jean 16.32 Matthieu 10.36
11 Ee Bwana, unifundishe njia yako, Na kuniongoza katika njia iliyonyoka; Kwa sababu yao wanaoniotea;
Psaumes 5.8 Psaumes 86.11 Psaumes 26.12 Psaumes 25.4-25.5 Psaumes 64.6
12 Usinitie katika nia ya watesi wangu; Maana mashahidi wa uongo wameniondokea, Nao watoao jeuri kama pumzi.
Psaumes 35.11 Actes 9.1 1 Samuel 22.9-22.10 1 Samuel 26.19 Psaumes 38.16
13 Naamini ya kuwa nitauona wema wa Bwana Katika nchi ya walio hai.
Psaumes 142.5 2 Corinthiens 4.8-4.14 Ezéchiel 26.20 2 Corinthiens 4.16 Psaumes 56.13
14 Umngoje Bwana, uwe hodari, Upige moyo konde, naam, umngoje Bwana.
Psaumes 31.24 Psaumes 37.34 Esaïe 40.31 Esaïe 30.18 Habakuk 2.3

Cette Bible est dans le domaine public.