Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 2.12
Bible en Swahili de l’est


Consécration et règne du divin roi

1 Mbona mataifa wanafanya ghasia, Na makabila wanatafakari ubatili?
Psaumes 46.6 Psaumes 21.11 Apocalypse 17.14 Psaumes 83.4-83.8 Jean 11.49-11.50
2 Wafalme wa dunia wanajipanga, Na wakuu wanafanya shauri pamoja, Juu ya Bwana, Na juu ya masihi wake.
Jean 1.41 Matthieu 27.1 Luc 23.11-23.12 Psaumes 45.7 Apocalypse 17.12-17.14
3 Na tuvipasue vifungo vyao, Na kuzitupia mbali nasi kamba zao.
Jérémie 5.5 Luc 19.14 1 Pierre 2.7-2.8 Luc 19.27
4 Yeye aketiye mbinguni anacheka, Bwana anawafanyia dhihaka.
Psaumes 59.8 Psaumes 37.13 Esaïe 40.22 Psaumes 11.4 Proverbes 1.26
5 Ndipo atakaposema nao kwa hasira yake, Na kuwafadhaisha kwa ghadhabu yake.
Esaïe 11.4 Psaumes 110.5-110.6 Matthieu 23.33-23.36 Psaumes 50.16-50.22 Zacharie 1.15
6 Nami nimemweka mfalme wangu Juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.
Psaumes 45.6 Psaumes 48.1-48.2 Matthieu 28.18 Apocalypse 14.1 Esaïe 9.6-9.7
7 Nitaihubiri amri; Bwana aliniambia, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa.
Actes 13.33 Matthieu 3.17 Hébreux 5.5 Hébreux 1.5-1.6 Jean 3.16
8 Uniombe, nami nitakupa mataifa kuwa urithi wako, Na miisho ya dunia kuwa milki yako.
Psaumes 22.27 Daniel 7.13 Psaumes 72.8 Psaumes 89.27 Jean 17.4-17.5
9 Utawaponda kwa fimbo ya chuma, Na kuwavunja kama chombo cha mfinyanzi.
Apocalypse 12.5 Apocalypse 2.26-2.27 Psaumes 89.23 Esaïe 30.14 Apocalypse 19.15
10 Na sasa, enyi wafalme, fanyeni akili, Enyi waamuzi wa dunia, mwadibiwe.
Osée 14.9 Esaïe 52.15 Psaumes 72.10-72.11 Esaïe 49.23 Psaumes 45.12
11 Mtumikieni Bwana kwa kicho, Shangilieni kwa kutetemeka.
Philippiens 2.12 Hébreux 12.28-12.29 Hébreux 12.25 Psaumes 119.119-119.120 Psaumes 97.1
12 Shikeni yaliyo bora asije akafanya hasira, Nanyi mkapotea njiani,Kwa kuwa hasira yake itawaka upesi,Heri wote wanaomkimbilia.
Apocalypse 6.16-6.17 Jean 5.23 Romains 9.33 Jérémie 17.7 1 Samuel 10.1

Cette Bible est dans le domaine public.