Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 143.4
Bible en Swahili de l’est


Prière pour la délivrance

1 Ee Bwana, uisikie sala yangu, uzisikilize dua zangu, Kwa uaminifu wako unijibu kwa haki yako.
Psaumes 71.2 Psaumes 140.6 Psaumes 31.1 1 Jean 1.9 Daniel 9.16
2 Wala usimhukumu mtumishi wako, Maana kwako hakuna aliye hai mwenye haki.
Ecclésiaste 7.20 Psaumes 130.3 Romains 3.20 Job 14.3 Job 25.4
3 Maana adui ameifuatia nafsi yangu, Ameutupa chini uzima wangu. Amenikalisha mahali penye giza, Kama watu waliokufa zamani.
Psaumes 88.4-88.6 Psaumes 31.12-31.13 Psaumes 35.4 2 Samuel 18.11 Lamentations 3.6
4 Na roho yangu imezimia ndani yangu, Moyo wangu ndani yangu umesituka.
Psaumes 142.3 Psaumes 77.3 Luc 22.44 Psaumes 124.4 Psaumes 102.1
5 Nimezikumbuka siku za kale, Nimeyatafakari matendo yako yote, Naziwaza kazi za mikono yako.
Psaumes 77.5-77.6 Michée 6.5 1 Samuel 17.34-17.37 1 Samuel 17.45-17.50 Psaumes 77.10-77.12
6 Nakunyoshea mikono yangu; Nafsi yangu inakuonea kiu kama nchi kame.
Psaumes 63.1 Psaumes 88.9 Job 11.13 Psaumes 84.2 Esaïe 26.8-26.9
7 Ee Bwana, unijibu hima, roho yangu imelegea; Usinifiche uso wako, Nisifanane nao washukao shimoni
Psaumes 69.17 Psaumes 27.9 Psaumes 28.1 Psaumes 84.2 Esaïe 38.18
8 Unifanye kusikia fadhili zako asubuhi, Kwa maana nimekutumaini Wewe. Unijulishe njia nitakayoiendea, Kwa maana nakuinulia nafsi yangu.
Psaumes 25.4-25.5 Psaumes 46.5 Esaïe 48.17 Esaïe 30.21 Psaumes 86.4
9 Ee Bwana, uniponye na adui zangu; Nimekukimbilia Wewe, unifiche.
Psaumes 59.1 Psaumes 142.5 Hébreux 6.18 Psaumes 34.2-34.4 Psaumes 31.15
10 Unifundishe kuyatenda mapenzi yako, Kwa maana ndiwe Mungu wangu; Roho yako mwema aniongoze kwenye nchi sawa,
Néhémie 9.20 Psaumes 25.4-25.5 Psaumes 119.12 Psaumes 23.3 Hébreux 13.21
11 Ee Bwana, unihuishe kwa ajili ya jina lako, Kwa haki yako unitoe roho yangu taabuni;
Psaumes 31.1 Psaumes 119.25 Psaumes 71.2 Apocalypse 7.14-7.17 Psaumes 138.7
12 Kwa fadhili zako utawakatilia mbali adui zangu; Na kuwaangamiza wote wanitesao nafsi, Kwa maana mimi ni mtumishi wako.
Psaumes 116.16 Psaumes 54.5 1 Samuel 26.10 Psaumes 52.5 1 Samuel 25.29

Cette Bible est dans le domaine public.