Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 102.21
Bible en Swahili de l’est


Prière dans la détresse

1 Ee Bwana, usikie kuomba kwangu, Kilio changu kikufikie.
Psaumes 61.2 Exode 2.23 Psaumes 18.6 Lamentations 3.44 Psaumes 55.1-55.5
2 Usinifiche uso wako siku ya shida yangu, Unitegee sikio lako, siku niitapo unijibu upesi.
Psaumes 69.17 Psaumes 27.9 Psaumes 71.2 1 Corinthiens 10.13 Psaumes 143.7
3 Maana siku zangu zinatoweka kama moshi, Na mifupa yangu inateketea kama kinga.
Jacques 4.14 Lamentations 1.13 Job 30.30 Psaumes 37.20 Psaumes 31.10
4 Moyo wangu umepigwa kama majani na kukauka, Naam, ninasahau kula chakula changu.
Psaumes 37.2 Esaïe 40.7 Esdras 10.6 Actes 9.9 Psaumes 143.3-143.4
5 Kwa ajili ya sauti ya kuugua kwangu Mifupa yangu imegandamana na nyama yangu.
Job 19.20 Proverbes 17.22 Lamentations 4.8 Psaumes 6.8 Psaumes 38.8-38.10
6 Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani, Na kufanana na bundi wa mahameni.
Sophonie 2.14 Esaïe 38.14 Job 30.29-30.30 Michée 1.8 Esaïe 34.11-34.15
7 Nakesha, tena nimekuwa kama shomoro Aliye peke yake juu ya nyumba.
Psaumes 77.4 Psaumes 38.11 Psaumes 130.6 Marc 14.33-14.37 Deutéronome 28.66-28.67
8 Adui zangu wananilaumu mchana kutwa; Wanaonichukia kana kwamba wana wazimu Huapa kwa kunitaja mimi.
Actes 26.11 Luc 6.11 Psaumes 31.11-31.13 Psaumes 89.51 Psaumes 69.20
9 Maana nimekula majivu kama chakula, Na kukichanganya kinywaji changu na machozi.
Psaumes 42.3 Psaumes 80.5 Michée 7.17 Esaïe 44.20 Michée 1.10
10 Kwa sababu ya ghadhabu yako na hasira yako; Maana umeniinua na kunitupilia mbali.
Psaumes 38.3 Lamentations 1.18 Lamentations 5.16 Psaumes 39.11 Psaumes 73.18-73.20
11 Siku zangu zi kama kivuli kilichotandaa, Nami ninanyauka kama majani.
Job 14.2 Psaumes 109.23 Psaumes 144.4 Psaumes 102.3-102.4 Psaumes 39.5-39.6
12 Bali Wewe, Bwana utaketi ukimiliki milele, Na kumbukumbu lako kizazi hata kizazi.
Psaumes 135.13 Psaumes 9.7 Exode 3.15 Lamentations 5.19 Apocalypse 1.17-1.18
13 Wewe mwenyewe utasimama, Na kuirehemu Sayuni, Kwa maana ndio wakati wa kuihurumia, Naam, majira yaliyoamriwa yamewadia.
Galates 4.4 Psaumes 44.26 Esaïe 40.2 2 Pierre 3.8 2 Pierre 3.12
14 Maana watumishi wako wameyaridhia mawe yake, Na kuyaonea huruma mavumbi yake.
Néhémie 4.2 Néhémie 2.17 Psaumes 137.5-137.6 Daniel 9.16 Néhémie 4.6
15 Kisha mataifa wataliogopa jina la Bwana, Na wafalme wote wa dunia utukufu wako;
1 Rois 8.43 Psaumes 138.4 Psaumes 68.31-68.32 Esaïe 60.3-60.22 Esaïe 55.5
16 Bwana atakapokuwa ameijenga Sayuni, Atakapoonekana katika utukufu wake,
Esaïe 60.1-60.2 Psaumes 147.2 Esaïe 66.18 Jérémie 31.4 Esaïe 60.7
17 Atakapoyaelekea maombi yake aliye mkiwa, Asiyadharau maombi yao.
Néhémie 1.6 Psaumes 22.24 Jérémie 29.11-29.14 Daniel 9.3-9.21 Psaumes 9.18
18 Kizazi kitakachokuja kitaandikiwa hayo, Na watu watakaoumbwa watamsifu Bwana.
Romains 15.4 1 Corinthiens 10.11 Psaumes 22.30-22.31 Esaïe 43.21 Psaumes 78.4-78.6
19 Maana ametazama toka patakatifu pake pa juu, Toka mbinguni Bwana ameiangalia nchi,
Deutéronome 26.15 Psaumes 14.2 Hébreux 9.23-9.24 2 Chroniques 16.9 Psaumes 33.13-33.14
20 Ili akusikie kuugua kwake aliyefungwa, Na kuwafungua walioandikiwa kufa.
Psaumes 79.11 Psaumes 146.7 Esaïe 61.1-61.3 Esaïe 14.17 Actes 12.6-12.11
21 Watu walitangaze jina la Bwana katika Sayuni, Na sifa zake katika Yerusalemu,
Psaumes 22.22 1 Pierre 2.9 Ephésiens 3.21 Psaumes 9.13-9.14 Ephésiens 2.4-2.7
22 Pindi mataifa watapokusanyika pamoja, Falme nazo ili kumtumikia Bwana.
Zacharie 8.20-8.23 Matthieu 24.14 Psaumes 72.8-72.11 Esaïe 49.22-49.23 Psaumes 22.27
23 Amezipunguza nguvu zangu njiani; Amezifupisha siku zangu.
2 Timothée 3.1-3.17 Apocalypse 11.2-11.19 Apocalypse 12.13-12.17 1 Timothée 4.1-4.3 Job 21.21
24 Nitasema, Ee Mungu wangu, usiniondoe katikati ya siku zangu; Miaka yako ni tangu kizazi hata kizazi.
Habakuk 1.12 Psaumes 39.13 Psaumes 102.12 Apocalypse 1.8 Psaumes 90.1-90.2
25 Hapo mwanzo uliutia msingi wa nchi, Na mbingu ni kazi ya mikono yako.
Genèse 1.1 Hébreux 1.10-1.12 Genèse 2.1 Job 38.4-38.7 Jérémie 32.17
26 Hizi zitaharibika, bali Wewe utadumu Naam, hizi zitachakaa kama nguo; Na kama mavazi utazibadilisha, Nazo zitabadilika.
Esaïe 34.4 Esaïe 51.6 Apocalypse 20.11 Matthieu 24.35 Romains 8.20
27 Lakini Wewe U Yeye yule; Na miaka yako haitakoma.
Malachie 3.6 Jacques 1.17 Hébreux 13.8 Apocalypse 1.17-1.18 Jean 8.58
28 Wana wa watumishi wako watakaa, Na wazao wao wataimarishwa mbele zako.
Psaumes 45.16-45.17 Psaumes 69.35-69.36 Esaïe 65.22 Esaïe 53.10 Psaumes 89.4

Cette Bible est dans le domaine public.