Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 102.10
Bible en Swahili de l’est


Prière dans la détresse

1 Ee Bwana, usikie kuomba kwangu, Kilio changu kikufikie.
Psaumes 61.2 Exode 2.23 Psaumes 18.6 Lamentations 3.8 Juges 10.16
2 Usinifiche uso wako siku ya shida yangu, Unitegee sikio lako, siku niitapo unijibu upesi.
Psaumes 69.17 Psaumes 27.9 Job 7.21 Actes 12.5-12.25 Job 34.29
3 Maana siku zangu zinatoweka kama moshi, Na mifupa yangu inateketea kama kinga.
Jacques 4.14 Psaumes 37.20 Lamentations 1.13 Job 30.30 Psaumes 31.10
4 Moyo wangu umepigwa kama majani na kukauka, Naam, ninasahau kula chakula changu.
Psaumes 37.2 Esaïe 40.7 Esdras 10.6 Psaumes 102.11 Job 10.1
5 Kwa ajili ya sauti ya kuugua kwangu Mifupa yangu imegandamana na nyama yangu.
Job 19.20 Psaumes 6.8 Proverbes 17.22 Lamentations 4.8 Psaumes 32.3-32.4
6 Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani, Na kufanana na bundi wa mahameni.
Sophonie 2.14 Michée 1.8 Esaïe 34.11-34.15 Apocalypse 18.2 Esaïe 38.14
7 Nakesha, tena nimekuwa kama shomoro Aliye peke yake juu ya nyumba.
Psaumes 77.4 Psaumes 38.11 Deutéronome 28.66-28.67 Job 7.13-7.16 Lamentations 3.28-3.30
8 Adui zangu wananilaumu mchana kutwa; Wanaonichukia kana kwamba wana wazimu Huapa kwa kunitaja mimi.
Actes 26.11 Psaumes 69.20 Actes 23.12-23.35 Jérémie 29.22 Psaumes 69.9-69.10
9 Maana nimekula majivu kama chakula, Na kukichanganya kinywaji changu na machozi.
Psaumes 42.3 Psaumes 80.5 Lamentations 3.15-3.16 Lamentations 3.48-3.49 Job 3.24
10 Kwa sababu ya ghadhabu yako na hasira yako; Maana umeniinua na kunitupilia mbali.
Psaumes 38.3 Psaumes 39.11 Psaumes 73.18-73.20 Daniel 9.8-9.14 Psaumes 38.18
11 Siku zangu zi kama kivuli kilichotandaa, Nami ninanyauka kama majani.
Job 14.2 Psaumes 109.23 Psaumes 144.4 Jacques 4.14 Jacques 1.10
12 Bali Wewe, Bwana utaketi ukimiliki milele, Na kumbukumbu lako kizazi hata kizazi.
Psaumes 9.7 Psaumes 135.13 Exode 3.15 Lamentations 5.19 Psaumes 90.1-90.2
13 Wewe mwenyewe utasimama, Na kuirehemu Sayuni, Kwa maana ndio wakati wa kuihurumia, Naam, majira yaliyoamriwa yamewadia.
Galates 4.4 Psaumes 44.26 Esaïe 40.2 2 Pierre 3.12 Esdras 1.1-1.11
14 Maana watumishi wako wameyaridhia mawe yake, Na kuyaonea huruma mavumbi yake.
Néhémie 4.2 Néhémie 4.6 Esdras 7.27 Esdras 1.5 Esdras 3.1-3.3
15 Kisha mataifa wataliogopa jina la Bwana, Na wafalme wote wa dunia utukufu wako;
1 Rois 8.43 Psaumes 138.4 Apocalypse 11.15 Psaumes 86.9 Psaumes 72.11
16 Bwana atakapokuwa ameijenga Sayuni, Atakapoonekana katika utukufu wake,
Esaïe 60.1-60.2 Psaumes 147.2 Esaïe 14.26 Michée 2.9 Psaumes 51.18
17 Atakapoyaelekea maombi yake aliye mkiwa, Asiyadharau maombi yao.
Néhémie 1.6 Psaumes 22.24 Jérémie 29.11-29.14 Daniel 9.3-9.21 Psaumes 9.18
18 Kizazi kitakachokuja kitaandikiwa hayo, Na watu watakaoumbwa watamsifu Bwana.
Romains 15.4 1 Corinthiens 10.11 Psaumes 22.30-22.31 Esaïe 43.21 Psaumes 71.18
19 Maana ametazama toka patakatifu pake pa juu, Toka mbinguni Bwana ameiangalia nchi,
Deutéronome 26.15 Psaumes 14.2 Psaumes 33.13-33.14 Job 22.12 Hébreux 8.1-8.2
20 Ili akusikie kuugua kwake aliyefungwa, Na kuwafungua walioandikiwa kufa.
Psaumes 79.11 Psaumes 146.7 2 Chroniques 33.11-33.13 Job 24.12 Zacharie 9.9-9.12
21 Watu walitangaze jina la Bwana katika Sayuni, Na sifa zake katika Yerusalemu,
Psaumes 22.22 Ephésiens 2.4-2.7 Psaumes 79.13 Esaïe 51.11 Psaumes 51.14-51.15
22 Pindi mataifa watapokusanyika pamoja, Falme nazo ili kumtumikia Bwana.
Zacharie 8.20-8.23 Psaumes 72.8-72.11 Esaïe 49.22-49.23 Matthieu 24.14 Osée 1.9-1.11
23 Amezipunguza nguvu zangu njiani; Amezifupisha siku zangu.
1 Timothée 4.1-4.3 Job 21.21 Psaumes 89.38-89.47 2 Thessaloniciens 2.3-2.12 2 Timothée 3.1-3.17
24 Nitasema, Ee Mungu wangu, usiniondoe katikati ya siku zangu; Miaka yako ni tangu kizazi hata kizazi.
Habakuk 1.12 Psaumes 102.12 Psaumes 39.13 Psaumes 90.1-90.2 Job 36.26
25 Hapo mwanzo uliutia msingi wa nchi, Na mbingu ni kazi ya mikono yako.
Genèse 1.1 Hébreux 1.10-1.12 Genèse 2.1 Proverbes 8.23-8.36 Exode 20.11
26 Hizi zitaharibika, bali Wewe utadumu Naam, hizi zitachakaa kama nguo; Na kama mavazi utazibadilisha, Nazo zitabadilika.
Esaïe 34.4 Esaïe 51.6 Apocalypse 20.11 Matthieu 24.35 Romains 8.20
27 Lakini Wewe U Yeye yule; Na miaka yako haitakoma.
Jacques 1.17 Malachie 3.6 Hébreux 13.8 Apocalypse 1.8 Job 36.26
28 Wana wa watumishi wako watakaa, Na wazao wao wataimarishwa mbele zako.
Psaumes 45.16-45.17 Psaumes 69.35-69.36 Psaumes 90.16-90.17 Esaïe 59.20-59.21 Psaumes 22.30-22.31

Cette Bible est dans le domaine public.