Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 102
Bible en Swahili de l’est


1 Ee Bwana, usikie kuomba kwangu, Kilio changu kikufikie. Psaumes 61.2 Exode 2.23 Psaumes 18.6 Psaumes 55.1-55.5 1 Samuel 9.16
2 Usinifiche uso wako siku ya shida yangu, Unitegee sikio lako, siku niitapo unijibu upesi. Psaumes 69.17 Psaumes 27.9 1 Corinthiens 10.13 Psaumes 143.7 Job 7.21
3 Maana siku zangu zinatoweka kama moshi, Na mifupa yangu inateketea kama kinga. Jacques 4.14 Lamentations 1.13 Job 30.30 Psaumes 37.20 Psaumes 31.10
4 Moyo wangu umepigwa kama majani na kukauka, Naam, ninasahau kula chakula changu. Psaumes 37.2 Esaïe 40.7 Esdras 10.6 Job 6.4 Psaumes 102.11
5 Kwa ajili ya sauti ya kuugua kwangu Mifupa yangu imegandamana na nyama yangu. Job 19.20 Lamentations 4.8 Psaumes 6.8 Proverbes 17.22 Psaumes 38.8-38.10
6 Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani, Na kufanana na bundi wa mahameni. Sophonie 2.14 Job 30.29-30.30 Michée 1.8 Esaïe 34.11-34.15 Apocalypse 18.2
7 Nakesha, tena nimekuwa kama shomoro Aliye peke yake juu ya nyumba. Psaumes 77.4 Psaumes 38.11 Marc 14.33-14.37 Deutéronome 28.66-28.67 Job 7.13-7.16
8 Adui zangu wananilaumu mchana kutwa; Wanaonichukia kana kwamba wana wazimu Huapa kwa kunitaja mimi. Actes 26.11 Psaumes 31.11-31.13 Psaumes 89.51 Psaumes 69.20 Actes 23.12-23.35
9 Maana nimekula majivu kama chakula, Na kukichanganya kinywaji changu na machozi. Psaumes 42.3 Psaumes 80.5 Esaïe 44.20 Michée 1.10 Lamentations 3.15-3.16
10 Kwa sababu ya ghadhabu yako na hasira yako; Maana umeniinua na kunitupilia mbali. Psaumes 38.3 Lamentations 1.18 Lamentations 5.16 Psaumes 39.11 Psaumes 73.18-73.20
11 Siku zangu zi kama kivuli kilichotandaa, Nami ninanyauka kama majani. Job 14.2 Psaumes 109.23 Psaumes 144.4 Psaumes 39.5-39.6 Jacques 4.14
12 Bali Wewe, Bwana utaketi ukimiliki milele, Na kumbukumbu lako kizazi hata kizazi. Psaumes 135.13 Psaumes 9.7 Exode 3.15 Lamentations 5.19 Psaumes 102.24-102.27
13 Wewe mwenyewe utasimama, Na kuirehemu Sayuni, Kwa maana ndio wakati wa kuihurumia, Naam, majira yaliyoamriwa yamewadia. Galates 4.4 Psaumes 44.26 Esaïe 40.2 2 Pierre 3.8 2 Pierre 3.12
14 Maana watumishi wako wameyaridhia mawe yake, Na kuyaonea huruma mavumbi yake. Néhémie 4.2 Psaumes 137.5-137.6 Daniel 9.16 Néhémie 4.6 Esdras 7.27
15 Kisha mataifa wataliogopa jina la Bwana, Na wafalme wote wa dunia utukufu wako; 1 Rois 8.43 Psaumes 138.4 Esaïe 60.3-60.22 Esaïe 55.5 Apocalypse 11.15
16 Bwana atakapokuwa ameijenga Sayuni, Atakapoonekana katika utukufu wake, Esaïe 60.1-60.2 Psaumes 147.2 Jérémie 31.4 Esaïe 60.7 Esaïe 14.26
17 Atakapoyaelekea maombi yake aliye mkiwa, Asiyadharau maombi yao. Néhémie 1.6 Psaumes 22.24 Jérémie 29.11-29.14 Daniel 9.3-9.21 Psaumes 9.18
18 Kizazi kitakachokuja kitaandikiwa hayo, Na watu watakaoumbwa watamsifu Bwana. Romains 15.4 1 Corinthiens 10.11 Psaumes 22.30-22.31 Esaïe 43.21 2 Corinthiens 5.17-5.18
19 Maana ametazama toka patakatifu pake pa juu, Toka mbinguni Bwana ameiangalia nchi, Deutéronome 26.15 Psaumes 14.2 Hébreux 9.23-9.24 2 Chroniques 16.9 Psaumes 33.13-33.14
20 Ili akusikie kuugua kwake aliyefungwa, Na kuwafungua walioandikiwa kufa. Psaumes 79.11 Psaumes 146.7 Esaïe 14.17 Actes 12.6-12.11 2 Chroniques 33.11-33.13
21 Watu walitangaze jina la Bwana katika Sayuni, Na sifa zake katika Yerusalemu, Psaumes 22.22 Ephésiens 3.21 Psaumes 9.13-9.14 Ephésiens 2.4-2.7 Psaumes 79.13
22 Pindi mataifa watapokusanyika pamoja, Falme nazo ili kumtumikia Bwana. Zacharie 8.20-8.23 Matthieu 24.14 Psaumes 72.8-72.11 Esaïe 49.22-49.23 Osée 1.9-1.11
23 Amezipunguza nguvu zangu njiani; Amezifupisha siku zangu. Apocalypse 11.2-11.19 Apocalypse 12.13-12.17 1 Timothée 4.1-4.3 Job 21.21 Psaumes 89.38-89.47
24 Nitasema, Ee Mungu wangu, usiniondoe katikati ya siku zangu; Miaka yako ni tangu kizazi hata kizazi. Habakuk 1.12 Psaumes 39.13 Psaumes 102.12 Apocalypse 1.8 Psaumes 90.1-90.2
25 Hapo mwanzo uliutia msingi wa nchi, Na mbingu ni kazi ya mikono yako. Genèse 1.1 Hébreux 1.10-1.12 Genèse 2.1 Jérémie 32.17 Proverbes 8.23-8.36
26 Hizi zitaharibika, bali Wewe utadumu Naam, hizi zitachakaa kama nguo; Na kama mavazi utazibadilisha, Nazo zitabadilika. Esaïe 51.6 Esaïe 34.4 Apocalypse 20.11 Matthieu 24.35 Romains 8.20
27 Lakini Wewe U Yeye yule; Na miaka yako haitakoma. Jacques 1.17 Malachie 3.6 Hébreux 13.8 Apocalypse 1.17-1.18 Jean 8.58
28 Wana wa watumishi wako watakaa, Na wazao wao wataimarishwa mbele zako. Psaumes 45.16-45.17 Psaumes 69.35-69.36 Esaïe 53.10 Psaumes 89.4 Psaumes 90.16-90.17

Cette Bible est dans le domaine public.