Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 10.8
Bible en Swahili de l’est


Le méchant et son sort

1 Ee Bwana, kwa nini wasimama mbali? Kwani kujificha nyakati za shida?
Psaumes 22.1 Job 23.9 Psaumes 27.9 Psaumes 44.24 Psaumes 30.7
2 Kwa kiburi chake asiye haki mnyonge anafuatiwa kwa ukali; Na wanaswe kwa hila zizo hizo walizoziwaza.
Psaumes 7.16 Jérémie 43.2 Esaïe 14.16 Psaumes 36.11 Exode 18.11
3 Maana mdhalimu hujisifia tamaa ya nafsi yake, Na mwenye choyo humkana Bwana na kumdharau.
Psaumes 94.4 Psaumes 49.6 1 Samuel 23.21 Romains 1.32 Lévitique 26.30
4 Mdhalimu kwa kiburi cha uso wake Asema, Hatapatiliza. Jumla ya mawazo yake ni, Hakuna Mungu;
Psaumes 53.1 Marc 7.21 Psaumes 14.1-14.2 Ephésiens 2.12 Deutéronome 8.14
5 Njia zake ni thabiti kila wakati. Hukumu zako ziko juu asizione, Adui zake wote awafyonya.
Psaumes 12.5 Esaïe 26.11 Esaïe 42.25 Esaïe 5.12 Esaïe 10.1
6 Asema moyoni mwake, Sitaondoshwa, Kizazi baada ya kizazi sitakuwamo taabuni.
Matthieu 24.48 Ecclésiaste 8.11 Apocalypse 18.7 Psaumes 15.5 1 Thessaloniciens 5.3
7 Kinywa chake kimejaa laana, Na hila na dhuluma. Chini ya ulimi wake kuna madhara na uovu,
Psaumes 7.14 Job 20.12 Psaumes 140.3 Psaumes 36.3 Psaumes 5.9
8 Hukaa katika maoteo ya vijiji. Mahali pa siri humwua asiye na hatia, Macho yake humvizia mtu duni.
Habakuk 3.14 Proverbes 1.11-1.12 Jérémie 22.17 Psaumes 17.11 Luc 10.1
9 Huotea faraghani kama simba pangoni, Huotea amkamate mtu mnyonge. Naam, humkamata mtu mnyonge, Akimkokota wavuni mwake.
Psaumes 17.12 Psaumes 59.3 Michée 7.2 Amos 5.11-5.12 Esaïe 32.7
10 Hujikunyata na kuinama; Watu duni huanguka kwa nguvu zake.
1 Samuel 2.36 1 Samuel 18.21-18.26 1 Samuel 23.21-23.22 2 Samuel 15.5
11 Asema moyoni mwake, Mungu amesahau, Auficha uso wake, haoni kamwe.
Psaumes 94.7 Ezéchiel 9.9 Psaumes 73.11 Ezéchiel 8.12 Job 22.13-22.14
12 Bwana, uondoke, Ee Mungu, uuinue mkono wako, Usiwasahau wanyonge.
Psaumes 9.12 Michée 5.9 Psaumes 3.7 Psaumes 7.6 Esaïe 26.11
13 Kwani mdhalimu kumdharau Mungu. Akisema moyoni mwake, Hutapatiliza?
Luc 10.16 2 Samuel 12.9-12.10 Luc 11.50-11.51 Psaumes 74.18 2 Chroniques 24.22
14 Umeona, maana unaangalia madhara na jeuri, Uyatwae mkononi mwako. Mtu duni hukuachia nafsi yake, Maana umekuwa msaidizi wa yatima.
Psaumes 68.5 Psaumes 146.9 1 Pierre 4.19 Osée 14.3 Deutéronome 10.18
15 Uuvunje mkono wake mdhalimu, Na mbaya, uipatilize dhuluma yake, hata usiione.
Psaumes 37.17 Psaumes 7.9 Ezéchiel 30.21-30.22 Sophonie 1.12 Job 38.15
16 Bwana ndiye Mfalme milele na milele; Mataifa wamepotea kutoka nchi yake.
Psaumes 29.10 Deutéronome 8.20 1 Timothée 1.17 Psaumes 145.13 Lamentations 5.19
17 Bwana, umeisikia tamaa ya wanyonge, Utaitengeneza mioyo yao, utalitega sikio lako.
1 Chroniques 29.18 Psaumes 9.18 1 Pierre 3.12 2 Chroniques 34.27 Jacques 1.16-1.17
18 Ili kumhukumu yatima naye aliyeonewa, Binadamu aliye udongo asizidi kudhulumu.
Psaumes 82.3 Psaumes 17.14 Esaïe 11.4 Psaumes 9.9 Luc 16.25

Cette Bible est dans le domaine public.