Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 10.18
Bible en Swahili de l’est


Le méchant et son sort

1 Ee Bwana, kwa nini wasimama mbali? Kwani kujificha nyakati za shida?
Psaumes 22.1 Job 23.9 Psaumes 27.9 Psaumes 44.24 Psaumes 30.7
2 Kwa kiburi chake asiye haki mnyonge anafuatiwa kwa ukali; Na wanaswe kwa hila zizo hizo walizoziwaza.
Psaumes 7.16 Esaïe 14.16 Psaumes 36.11 Exode 18.11 Esaïe 10.12-10.13
3 Maana mdhalimu hujisifia tamaa ya nafsi yake, Na mwenye choyo humkana Bwana na kumdharau.
Psaumes 94.4 Psaumes 49.6 Lévitique 26.30 1 Timothée 6.9-6.10 Psaumes 73.8-73.9
4 Mdhalimu kwa kiburi cha uso wake Asema, Hatapatiliza. Jumla ya mawazo yake ni, Hakuna Mungu;
Psaumes 53.1 Ephésiens 2.12 Deutéronome 8.14 Esaïe 65.2 Actes 8.22
5 Njia zake ni thabiti kila wakati. Hukumu zako ziko juu asizione, Adui zake wote awafyonya.
Psaumes 12.5 Esaïe 26.11 Esaïe 5.12 Esaïe 10.1 1 Rois 20.13
6 Asema moyoni mwake, Sitaondoshwa, Kizazi baada ya kizazi sitakuwamo taabuni.
Matthieu 24.48 Ecclésiaste 8.11 Apocalypse 18.7 1 Thessaloniciens 5.3 Esaïe 47.7
7 Kinywa chake kimejaa laana, Na hila na dhuluma. Chini ya ulimi wake kuna madhara na uovu,
Psaumes 7.14 Job 20.12 Psaumes 140.3 Psaumes 36.3 Psaumes 62.4
8 Hukaa katika maoteo ya vijiji. Mahali pa siri humwua asiye na hatia, Macho yake humvizia mtu duni.
Habakuk 3.14 Proverbes 1.11-1.12 Jérémie 22.17 Psaumes 17.11 Luc 10.1
9 Huotea faraghani kama simba pangoni, Huotea amkamate mtu mnyonge. Naam, humkamata mtu mnyonge, Akimkokota wavuni mwake.
Psaumes 17.12 Psaumes 59.3 Michée 7.2 Job 5.15-5.16 Lamentations 3.10
10 Hujikunyata na kuinama; Watu duni huanguka kwa nguvu zake.
1 Samuel 2.36 1 Samuel 18.21-18.26 1 Samuel 23.21-23.22 2 Samuel 15.5
11 Asema moyoni mwake, Mungu amesahau, Auficha uso wake, haoni kamwe.
Psaumes 94.7 Ezéchiel 9.9 Psaumes 73.11 Ezéchiel 8.12 Luc 7.39
12 Bwana, uondoke, Ee Mungu, uuinue mkono wako, Usiwasahau wanyonge.
Psaumes 9.12 Michée 5.9 Psaumes 3.7 Esaïe 26.11 Psaumes 17.7
13 Kwani mdhalimu kumdharau Mungu. Akisema moyoni mwake, Hutapatiliza?
2 Samuel 12.9-12.10 Luc 11.50-11.51 Psaumes 74.18 2 Chroniques 24.22 Genèse 42.22
14 Umeona, maana unaangalia madhara na jeuri, Uyatwae mkononi mwako. Mtu duni hukuachia nafsi yake, Maana umekuwa msaidizi wa yatima.
Psaumes 68.5 Psaumes 146.9 Osée 14.3 Deutéronome 10.18 Psaumes 55.22
15 Uuvunje mkono wake mdhalimu, Na mbaya, uipatilize dhuluma yake, hata usiione.
Psaumes 37.17 Ezéchiel 30.21-30.22 Sophonie 1.12 Job 38.15 Psaumes 7.9
16 Bwana ndiye Mfalme milele na milele; Mataifa wamepotea kutoka nchi yake.
Psaumes 29.10 1 Timothée 1.17 Psaumes 145.13 Lamentations 5.19 Daniel 4.34
17 Bwana, umeisikia tamaa ya wanyonge, Utaitengeneza mioyo yao, utalitega sikio lako.
1 Chroniques 29.18 Psaumes 9.18 1 Pierre 3.12 2 Chroniques 34.27 Jacques 1.16-1.17
18 Ili kumhukumu yatima naye aliyeonewa, Binadamu aliye udongo asizidi kudhulumu.
Psaumes 82.3 Psaumes 17.14 Esaïe 11.4 Psaumes 9.9 Luc 18.7-18.8

Cette Bible est dans le domaine public.