Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 42.2
Bible en Swahili de l’est


Aveu par Job de son ignorance

1 Ndipo Ayubu akamjibu Bwana, na kusema.
2 Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote, Na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika.
Matthieu 19.26 Genèse 18.14 Ephésiens 1.11 Jean 2.24-2.25 Marc 10.27
3 Ni nani huyu afichaye mashauri bila maarifa? Kwa maana, nimesema maneno nisiyoyafahamu, Mambo ya ajabu ya kunishinda mimi, nisiyoyajua.
Psaumes 40.5 Psaumes 131.1 Psaumes 139.6 Job 38.2 Proverbes 30.2-30.4
4 Sikiliza, nakusihi, nami nitanena; Nitakuuliza neno, nawe niambie.
Job 38.3 Job 40.7 Genèse 18.30-18.32 Genèse 18.27
5 Nilikuwa nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa masikio; Bali sasa jicho langu linakuona.
Romains 10.17 Jean 1.18 Esaïe 6.1 Esaïe 6.5 Jean 12.41
6 Kwa sababu hiyo najichukia nafsi yangu, na kutubu Katika mavumbi na majivu.
Esdras 9.6 Job 2.8 Job 30.19 Job 40.3-40.4 Daniel 9.3

Retour de Job à la prospérité

7 Basi ikawa, baada ya Bwana kumwambia Ayubu maneno hayo, Bwana akamwambia huyo Elifazi Mtemani, Hasira zangu zinawaka juu yako, na juu ya hao rafiki zako wawili; kwa kuwa ninyi hamkunena yaliyo sawa katika habari zangu, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu.
Job 2.11 Psaumes 51.4 Job 4.1 Job 8.1 Job 11.1
8 Basi sasa, jitwalieni ng’ombe waume saba, na kondoo waume saba, mkamwendee mtumishi wangu Ayubu, mjisongezee sadaka ya kuteketezwa; na huyo mtumishi wangu Ayubu atawaombea ninyi; kwa kuwa nitamridhia yeye, nisiwatende sawasawa na upumbavu wenu; kwani ninyi hamkunena maneno yaliyonyoka katika habari zangu, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu.
Nombres 23.1 1 Chroniques 15.26 Job 1.5 Nombres 23.29 Ezéchiel 14.14
9 Basi Elifazi, Mtemani, na Bildadi, Mshuhi, na Sofari, Mnaamathi, wakaenda, wakafanya kama vile Bwana alivyowaamuru; naye Bwana akamridhia Ayubu.
Ecclésiaste 9.7 Actes 10.33 Job 22.27 Jean 2.5 Hébreux 11.8
10 Kisha Bwana akaugeuza uteka wa Ayubu, hapo alipowaombea rafiki zake; Bwana naye akampa Ayubu mara mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza.
Job 8.6-8.7 Psaumes 14.7 Esaïe 40.2 Deutéronome 30.3 Esaïe 61.7
11 Ndipo wakamwendea nduguze wote, waume kwa wake, nao wote waliojuana naye hapo zamani, wakala chakula pamoja naye katika nyumba yake; nao wakamlilia na kumtuza moyo katika habari za huo uovu wote Bwana aliouleta juu yake; kila mtu akampa kipande cha fedha, na pete ya dhahabu kila mmoja.
Job 2.11 Job 19.13-19.14 Genèse 24.22 Genèse 37.35 1 Corinthiens 12.26
12 Basi hivyo Bwana akaubarikia huo mwisho wa Ayubu zaidi ya mwanzo wake; naye alikuwa na kondoo kumi na nne elfu, na ngamia elfu sita, na jozi za ng’ombe elfu, na punda wake elfu.
Job 8.7 Job 1.3 Jacques 5.11 Psaumes 144.13-144.15 Proverbes 10.22
13 Tena alikuwa na wana waume saba, na binti watatu.
Job 1.2 Esaïe 49.20 Psaumes 107.41 Psaumes 127.3
14 Akamwita huyo wa kwanza jina lake Yemima; na wa pili akamwita jina lake Kesia; na wa tatu akamwita jina lake Keren-hapuhu.
15 Katika nchi hiyo yote hawakuwapo wanawake waliokuwa wazuri kama hao wana wa Ayubu; na baba yao akawapa urithi kati ya ndugu zao wana waume.
Nombres 27.7 Josué 18.4 Actes 7.20 Josué 15.18-15.19 Psaumes 144.12
16 Kisha baada ya mambo hayo Ayubu akaishi miaka mia na arobaini, naye akawaona wanawe, na wana wa wanawe, hata vizazi vinne.
Genèse 50.23 Psaumes 128.6 Josué 24.29 Deutéronome 34.7 Genèse 11.32
17 Basi Ayubu akafa, mzee sana mwenye kujawa na siku.
Genèse 25.8 Genèse 15.15 Job 5.26 Deutéronome 6.2 Psaumes 91.16

Cette Bible est dans le domaine public.