Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 40.19
Bible en Swahili de l’est


Incapacité de Job à répondre

1 Bwana akafuliza kumjibu Ayubu, na kusema,
Job 38.1 Job 40.6
2 Je! Mwenye hoja atashindana na Mwenyezi? Mwenye kujadiliana na Mungu, na ajibu yeye.
Job 33.13 Esaïe 45.9-45.11 Job 9.3 Job 19.6-19.11 Job 27.2
3 Ndipo Ayubu akamjibu Mungu, na kusema,
4 Tazama, mimi si kitu kabisa, nikujibu nini? Naweka mkono wangu kinywani pangu.
Job 29.9 Job 21.5 Job 42.6 Esdras 9.6 Genèse 32.10
5 Nimenena mara moja, nami sitajibu; Naam, nimenena mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.
Job 33.14 Psaumes 62.11 2 Rois 6.10 Job 9.15 Jérémie 31.18-31.19

Les animaux monstrueux

6 Ndipo Bwana akamjibu Ayubu katika upepo wa kisulisuli, na kusema,
Job 38.1 Psaumes 50.3-50.4 Hébreux 12.18-12.20 2 Pierre 3.10-3.12
7 Jifunge viuno kama mwanamume, Mimi nitakuuliza neno, nawe niambie.
Job 38.3 Job 42.4 Job 13.22 Job 23.3-23.4
8 Je! Hata hukumu yangu utaibatilisha? Utanitia mimi hatiani, upate kuhesabiwa haki?
Job 32.2 Job 10.3 Job 34.5-34.6 Romains 3.4 Hébreux 7.18
9 Au je! Wewe una mkono kama Mungu? Waweza kutoa ngurumo kwa sauti kama yeye?
Psaumes 89.13 Job 37.4-37.5 Esaïe 45.9 Psaumes 39.3-39.9 Psaumes 89.10
10 Haya! Jivike sasa fahari na ukuu; Jipambe heshima na enzi.
Psaumes 93.1 Esaïe 59.17 Psaumes 149.4 Esaïe 4.2 Psaumes 45.3-45.4
11 Mwaga mafuriko ya hasira zako, Ukamtazame kila mtu mwenye kiburi, ukamdhili.
Daniel 4.37 Esaïe 2.11-2.12 Esaïe 2.17 Nahum 1.6 Actes 12.22-12.23
12 Mtazame kila mtu mwenye kiburi ukamshushe, Ukawakanyage waovu hapo wasimamapo.
Esaïe 63.3 Malachie 4.3 Psaumes 60.12 1 Samuel 2.7 Actes 1.25
13 Wafiche mavumbini pamoja, Wafunge nyuso zao mahali palipositirika.
Esaïe 2.10 Esther 7.8 Job 36.13 Job 14.13 Psaumes 49.14
14 Ndipo mimi nami nitazikiri habari zako, Ya kuwa mkono wako wa kuume waweza kukuokoa.
Psaumes 44.6 Ephésiens 2.4-2.9 Psaumes 44.3 Romains 5.6 Esaïe 40.29
15 Mwangalie huyo kiboko, niliyemwumba pamoja nawe; Yeye hula nyasi kama vile ng’ombe,
Job 40.20 Psaumes 104.14 Job 39.8 Genèse 1.24-1.26
16 Tazama basi, nguvu zake ni katika viuno vyake, Na uwezo wake u katika mishipa ya tumbo lake.
17 Yeye hutikisa mkia wake mfano wa mwerezi; Mishipa ya mapaja yake yanaungamana pamoja.
Job 41.23
18 Mifupa yake ni kama mirija ya shaba; Mbavu zake ni kama vipande vya chuma.
Esaïe 48.4 Job 7.12
19 Yeye ni mkuu wa njia za Mungu; Yeye aliyemfanya alimpa upanga wake.
Psaumes 7.12 Job 26.13 Esaïe 27.1 Job 41.33 Psaumes 104.24
20 Hakika milima humtolea chakula; Hapo wachezapo wanyama wote wa barani.
Psaumes 104.14 Psaumes 104.26 Psaumes 147.8-147.9 Job 40.15
21 Hulala chini ya miti yenye vivuli, Mafichoni penye mianzi, na matopeni.
Esaïe 35.7 Esaïe 19.6-19.7
22 Hiyo miti yenye vivuli humfunika kwa vivuli vyao; Mierebi ya vijito humzunguka.
Esaïe 15.7 Ezéchiel 17.5 Lévitique 23.40
23 Tazama, mto ukifurika, yeye hatetemeki; Hujiona yu salama, ijapokuwa Yordani hufurika hata kinywani pake.
Genèse 13.10 Psaumes 55.8 Esaïe 28.16 Esaïe 37.25 Josué 3.15
24 Je! Mtu ye yote atamnasa akiwa yu macho, Au, kumtoboa pua yake kwa mtego?
Job 41.1-41.2

Cette Bible est dans le domaine public.