Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 40.11
Bible en Swahili de l’est


Incapacité de Job à répondre

1 Bwana akafuliza kumjibu Ayubu, na kusema,
Job 38.1 Job 40.6
2 Je! Mwenye hoja atashindana na Mwenyezi? Mwenye kujadiliana na Mungu, na ajibu yeye.
Job 33.13 Job 9.3 Esaïe 45.9-45.11 Job 14.16-14.17 Job 7.19-7.21
3 Ndipo Ayubu akamjibu Mungu, na kusema,
4 Tazama, mimi si kitu kabisa, nikujibu nini? Naweka mkono wangu kinywani pangu.
Job 29.9 Job 21.5 Job 42.6 Genèse 32.10 Proverbes 30.32
5 Nimenena mara moja, nami sitajibu; Naam, nimenena mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.
Job 33.14 Psaumes 62.11 Job 9.15 Jérémie 31.18-31.19 Job 9.3

Les animaux monstrueux

6 Ndipo Bwana akamjibu Ayubu katika upepo wa kisulisuli, na kusema,
Job 38.1 Hébreux 12.18-12.20 2 Pierre 3.10-3.12 Psaumes 50.3-50.4
7 Jifunge viuno kama mwanamume, Mimi nitakuuliza neno, nawe niambie.
Job 38.3 Job 42.4 Job 23.3-23.4 Job 13.22
8 Je! Hata hukumu yangu utaibatilisha? Utanitia mimi hatiani, upate kuhesabiwa haki?
Job 32.2 Job 10.3 Job 34.5-34.6 Romains 3.4 Psaumes 51.4
9 Au je! Wewe una mkono kama Mungu? Waweza kutoa ngurumo kwa sauti kama yeye?
Psaumes 89.13 Job 37.4-37.5 Psaumes 39.3-39.9 Psaumes 89.10 Job 33.12-33.13
10 Haya! Jivike sasa fahari na ukuu; Jipambe heshima na enzi.
Psaumes 93.1 Esaïe 59.17 Psaumes 149.4 Exode 28.2 Matthieu 6.13
11 Mwaga mafuriko ya hasira zako, Ukamtazame kila mtu mwenye kiburi, ukamdhili.
Daniel 4.37 Esaïe 2.11-2.12 Esaïe 2.17 Nahum 1.6 Romains 2.8-2.9
12 Mtazame kila mtu mwenye kiburi ukamshushe, Ukawakanyage waovu hapo wasimamapo.
Esaïe 63.3 Malachie 4.3 1 Samuel 2.7 Actes 1.25 Ecclésiaste 11.3
13 Wafiche mavumbini pamoja, Wafunge nyuso zao mahali palipositirika.
Esaïe 2.10 Esther 7.8 Job 36.13 Job 14.13 Psaumes 49.14
14 Ndipo mimi nami nitazikiri habari zako, Ya kuwa mkono wako wa kuume waweza kukuokoa.
Ephésiens 2.4-2.9 Psaumes 44.3 Romains 5.6 Esaïe 40.29 Psaumes 44.6
15 Mwangalie huyo kiboko, niliyemwumba pamoja nawe; Yeye hula nyasi kama vile ng’ombe,
Psaumes 104.14 Job 39.8 Genèse 1.24-1.26 Job 40.20
16 Tazama basi, nguvu zake ni katika viuno vyake, Na uwezo wake u katika mishipa ya tumbo lake.
17 Yeye hutikisa mkia wake mfano wa mwerezi; Mishipa ya mapaja yake yanaungamana pamoja.
Job 41.23
18 Mifupa yake ni kama mirija ya shaba; Mbavu zake ni kama vipande vya chuma.
Job 7.12 Esaïe 48.4
19 Yeye ni mkuu wa njia za Mungu; Yeye aliyemfanya alimpa upanga wake.
Job 26.13 Esaïe 27.1 Job 41.33 Psaumes 104.24 Psaumes 7.12
20 Hakika milima humtolea chakula; Hapo wachezapo wanyama wote wa barani.
Psaumes 104.26 Psaumes 104.14 Psaumes 147.8-147.9 Job 40.15
21 Hulala chini ya miti yenye vivuli, Mafichoni penye mianzi, na matopeni.
Esaïe 19.6-19.7 Esaïe 35.7
22 Hiyo miti yenye vivuli humfunika kwa vivuli vyao; Mierebi ya vijito humzunguka.
Ezéchiel 17.5 Lévitique 23.40 Esaïe 15.7
23 Tazama, mto ukifurika, yeye hatetemeki; Hujiona yu salama, ijapokuwa Yordani hufurika hata kinywani pake.
Genèse 13.10 Psaumes 55.8 Esaïe 28.16 Esaïe 37.25 Josué 3.15
24 Je! Mtu ye yote atamnasa akiwa yu macho, Au, kumtoboa pua yake kwa mtego?
Job 41.1-41.2

Cette Bible est dans le domaine public.