Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 35.9
Bible en Swahili de l’est


Appel à rechercher Dieu

1 Tena Elihu akajibu na kusema,
2 Je! Wewe wadhani kwamba haya ni haki yako, Au je! Wasema, Haki yangu ni zaidi kuliko ya Mungu,
Matthieu 12.36-12.37 Job 10.7 Job 9.17 Job 19.6-19.7 Job 34.5
3 Maana wasema, Kutakuwa na faida gani kwako wewe? Tena, Nitapata faida gani, kuliko nikifanya dhambi?
Job 34.9 Job 9.21-9.22 Psaumes 73.13 Job 21.15 Job 31.2
4 Mimi nitakujibu, Na hawa wenzio pamoja nawe.
Job 34.8 Proverbes 13.20
5 Ziangalie mbingu ukaone; Na mawingu yaangalie, yaliyo juu kuliko wewe.
Job 22.12 Esaïe 55.9 Nahum 1.3 Psaumes 8.3-8.4 Job 37.22-37.23
6 Ikiwa umefanya dhambi, umefanya nini juu yake? Yakiwa makosa yako yameongezeka, wamfanyia nini yeye?
Proverbes 8.36 Jérémie 7.19 Proverbes 9.12
7 Ikiwa u mwenye haki, wampa kitu gani? Au yeye hupokea nini mkononi mwako?
Job 22.2-22.3 Romains 11.35 Proverbes 9.12 Luc 17.10 Psaumes 16.2
8 Uovu wako waweza kumwumiza mtu kama wewe; Na haki yako yaweza kumfaa mwanadamu.
Genèse 12.2 Genèse 19.29 Jonas 1.12 Hébreux 11.7 Josué 7.1-7.5
9 Kwa sababu ya wingi wa jeuri wao hulia; Walilia msaada kwa sababu ya mkono wa wakuu.
Exode 2.23 Job 34.28 Luc 18.3-18.7 Psaumes 55.2-55.3 Psaumes 10.15
10 Wala hapana asemaye, Yuko wapi Mungu Muumba wangu, Awapaye nyimbo wakati wa usiku;
Psaumes 42.8 Psaumes 149.5 Actes 16.25 Esaïe 51.13 Psaumes 77.6
11 Atufundishaye zaidi ya hayawani wa nchi, Na kutufanya wenye hekima kuliko ndege za angani?
Psaumes 94.12 Job 36.22 Genèse 1.26 Job 32.8 Genèse 2.7
12 Hulia huko, lakini hapana ajibuye, Kwa sababu ya kiburi cha watu waovu.
Proverbes 1.28 Jean 9.31 Psaumes 123.3-123.4 Esaïe 14.14-14.17 Psaumes 73.6-73.8
13 Hakika Mungu hatasikia ubatili, Wala Mwenyezi hatauangalia.
Proverbes 15.29 Jérémie 11.11 Esaïe 1.15 Jacques 4.3 Proverbes 15.8
14 Sembuse usemapo wewe ya kuwa humwangalii, Hiyo daawa i mbele yake, nawe wamngojea!
Job 9.11 Job 9.19 Psaumes 62.8 Psaumes 37.5-37.6 Esaïe 54.17
15 Lakini sasa, kwa sababu yeye hakukujilia katika hasira zake, Wala hauangalii sana unyeti;
Psaumes 89.32 Osée 11.8-11.9 Apocalypse 3.19 Job 30.15-30.31 Psaumes 88.11-88.16
16 Ndiposa Ayubu hufunua kinywa chake kwa ubatili; Huongeza maneno pasipo maarifa.
Job 38.2 Job 34.35-34.37 Job 3.1 Job 33.2 Job 33.8-33.12

Cette Bible est dans le domaine public.