Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 13
Bible en Swahili de l’est


1 Tazama, jicho langu limeyaona hayo yote, Sikio langu limeyasikia na kuelewa nayo.
Job 42.3-42.6 Job 15.17-15.18 Job 5.27 1 Jean 1.3 Job 4.12
2 Hayo myajuayo ninyi, na mimi pia nayajua; Mimi si duni kuliko ninyi.
Job 12.3 Job 37.2 Job 35.16 Job 15.8-15.9 Job 40.4-40.5
3 Hakika ningenena naye huyo Mwenyezi, Nami nataka kuhojiana na Mungu.
Esaïe 41.21 Job 31.35 Job 9.3 Job 13.22 Job 23.3-23.7
4 Lakini ninyi hubuni maneno ya uongo, Ninyi nyote ni matabibu wasiofaa.
Psaumes 119.69 Job 16.2 Jérémie 8.22 Jérémie 46.11 Job 5.1-5.5
5 Laiti mngenyamaza kabisa! Hilo lingekuwa hekima kwenu.
Proverbes 17.28 Ecclésiaste 5.3 Job 13.13 Jacques 1.19 Job 21.2-21.3
6 Sikieni sasa basi hoja zangu, Mkayasikie mashindano ya midomo yangu.
Job 33.1-33.3 Juges 9.7 Proverbes 8.6-8.7 Job 34.2 Job 21.2-21.3
7 Je! Mtanena yasiyo ya haki kwa ajili ya Mungu, Na kusema kwa udanganyifu kwa ajili yake?
Job 36.4 2 Corinthiens 4.2 Job 17.5 Job 4.7 Job 11.2-11.4
8 Je! Mtamwonyesha yeye upendeleo? Mtamtetea Mungu?
Proverbes 24.23 Malachie 2.9 Job 32.21 Job 34.19 Exode 23.2-23.3
9 Je! Itafaa yeye kuwatafuta ninyi? Au, kama kumdanganya mtu, je! Mtamdanganya yeye?
Jérémie 17.10 Galates 6.7-6.8 Job 17.2 Job 34.36 Esaïe 28.22
10 Hakika atawakemea ninyi, Mkiwapendelea watu kwa siri.
Job 42.7-42.8 Jacques 2.9 Psaumes 50.21-50.22 Psaumes 82.2
11 Je! Huo ukuu wake hautawatia hofu, Na utisho wake hautawaangukia?
Psaumes 119.120 Job 31.23 Jérémie 5.22 Exode 15.16 Job 13.21
12 Matamko yenu ya hekima ni mithali ya majivu, Ngome zenu ni ngome za udongo.
Esaïe 26.14 Job 4.19 Job 18.17 Psaumes 109.15 Psaumes 34.16
13 Nyamazeni, niacheni, ili nipate kunena, Na hayo yatakayonijilia na yaje.
Job 7.11 Job 13.5 Job 6.9-6.10 Job 10.1 Job 7.15-7.16
14 Nitaitwaa nyama ya mwili wangu katika meno yangu, Na kuutwaa uhai wangu mkononi mwangu!
Juges 12.3 1 Samuel 19.5 Ecclésiaste 4.5 Psaumes 119.109 1 Samuel 28.21
15 Tazama, ataniua; sina tumaini; ila hata hivyonitaithibitisha njia yangu mbele yake.
Job 27.5 Proverbes 14.32 Job 23.10 Psaumes 23.4 Romains 8.38-8.39
16 Hili nalo litakuwa ni wokovu wangu; Kwani asiyemcha Mungu hatakaribia mbele yake.
Esaïe 12.1-12.2 Actes 13.47 Psaumes 118.14 Job 27.8-27.10 Psaumes 27.1
17 Sikieni sana maneno yangu, Maelezo yangu na yaingie masikioni mwenu.
Job 13.6 Job 21.2 Job 33.1
18 Angalieni sasa, nimekwisha kulitengeneza neno langu, Najua ya kuwa ni mwenye haki mimi.
Job 23.4 Job 9.2-9.3 Job 40.7-40.8 2 Corinthiens 1.12 Job 9.20
19 Yuko nani atakayeshindana nami? Maana sasa nitanyamaa kimya na kutoa roho.
Esaïe 50.7-50.8 Romains 8.33 Job 33.32 Jérémie 20.9 Job 7.11
20 Lakini msinifanyie mambo mawili, hayo tu, Ndipo nami sitajificha usoni pako;
Job 9.34-9.35 Genèse 3.8-3.10 Apocalypse 6.15-6.16 Psaumes 139.12
21 Uondoe mkono wako usinilemee; Na utisho wako usinitie hofu.
Job 9.34 Psaumes 39.10 Job 33.7 Job 22.15-22.17 Psaumes 119.120
22 Basi uite wakati huo, nami nitaitika; Au, niache ninene mimi, nawe unijibu.
Job 14.15 Job 9.16 Job 9.32 Job 38.3 Job 42.3-42.6
23 Maovu yangu na dhambi zangu ni ngapi? Nijulishe kosa langu na dhambi yangu.
Psaumes 44.20-44.21 Job 36.8-36.9 Job 22.5 Psaumes 139.23
24 Mbona umeuficha uso wako, Na kunihesabu kuwa ni adui yako?
Job 19.11 Lamentations 2.5 Psaumes 13.1 Job 33.10 Esaïe 8.17
25 Je! Utalitaabisha jani lipeperushwalo? Au, je! Utayafuatia hayo mabua makavu?
Job 21.18 Lévitique 26.36 Esaïe 17.13 Job 14.3 Matthieu 12.20
26 Kwani umeandika maneno ya uchungu juu yangu, Na kunirithisha maovu ya ujana wangu;
Psaumes 25.7 Jérémie 31.19 Job 3.20 Proverbes 5.11-5.13 Ruth 1.20
27 Waitia miguu yangu katika mkatale, na kuyaaua mapito yangu yote; Wajiandikia alama kuzizunguka nyayo za miguu yangu;
Job 33.11 Job 14.16 Actes 16.24 Proverbes 7.22 Job 16.9
28 Nijapokuwa ni kama kitu kilichooza, kinachosinyaa, Mfano wa nguo iliyoliwa na nondo.
Psaumes 39.11 Job 4.19 Job 30.29-30.30 Job 30.17-30.19 Nombres 12.12

Cette Bible est dans le domaine public.