Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 11
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 1 de Tsophar

1 Ndipo Sofari Mnaamathi akajibu, na kusema,
Job 2.11 Job 20.1
2 Je! Huu wingi wa maneno usijibiwe? Na mtu aliyejaa maneno, je! Ahesabiwe kuwa na haki?
Job 18.2 Proverbes 10.19 Psaumes 140.11 Job 16.3 Job 8.2
3 Je! Majivuno yako yawanyamazishe watu wawe kimya? Nawe hapo ufanyapo dhihaka, je! Hapana mtu atakayekutahayarisha?
Job 17.2 Psaumes 35.16 Job 34.7 Job 24.25 Job 15.2-15.3
4 Kwa kuwa wewe wasema, Mafunzo yangu ni safi, Nami ni safi machoni pako.
Job 10.7 Job 6.10 Job 14.4 Job 7.20 Job 6.29-6.30
5 Lakini, laiti Mungu angenena, Na kuifunua midomo yake juu yako;
Job 38.1-38.2 Job 23.3-23.7 Job 42.7 Job 40.1-40.5 Job 40.8
6 Tena akuonyeshe hizo siri za hekima, Ya kuwa hufanikiwa katika kuyatimiza makusudi yake! Ujue basi ya kuwa Mungu akuachilia katika uovu wako.
Esdras 9.13 Psaumes 103.10 Job 15.5 Job 15.11 Job 9.4
7 Je! Wewe waweza kuuvumbua ukuu wa Mungu? Waweza kuufikilia upeo wa huyo Mwenyezi?
Romains 11.33 Ecclésiaste 3.11 Job 5.9 Psaumes 145.3 Job 37.23
8 Ni juu mno kama mbingu; waweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kuliko kuzimuni; waweza kujua nini wewe?
Job 22.12 Amos 9.2 Esaïe 55.9 Job 35.5 Job 26.6
9 Cheo chake ni kirefu kuliko dunia, Ni kipana zaidi ya bahari.
Psaumes 139.9-139.10 Psaumes 65.5-65.8 Job 28.24-28.25
10 Yeye akipita, na kufunga watu, Na kuwaita hukumuni, ni nani basi awezaye kumzuia?
Job 9.12-9.13 Apocalypse 3.7 Job 12.14 Daniel 4.35 Job 9.4
11 Kwani yeye awajua watu baradhuli; Huona na uovu pia, hata asipoufikiri.
Hébreux 4.13 Psaumes 10.14 Job 34.21-34.23 Jérémie 17.9-17.10 Jean 2.24-2.25
12 Lakini mpumbavu aweza kupata ufahamu, Ingawa mwanadamu huzaliwa kama mtoto wa punda-mwitu.
Job 39.5-39.8 Psaumes 73.22 Ecclésiaste 3.18 Jérémie 2.24 Psaumes 51.5
13 Wewe ukiuweka moyo wako kwa uelekevu, Na kumnyoshea mikono yako;
Psaumes 88.9 Psaumes 78.8 1 Samuel 7.3 Psaumes 143.6 2 Chroniques 19.3
14 Ikiwa una uovu mkononi mwako, uweke mbali nawe, Wala usikubali upuzi kukaa hemani mwako;
Job 22.23 Esaïe 1.15 Zacharie 5.3-5.4 Jacques 4.8 Psaumes 101.2
15 Hakika ndipo utakapopata kuinua uso pasipo ila; Naam, utathibitika, wala hutakuwa na hofu;
Job 22.26 2 Corinthiens 1.12 Psaumes 119.6-119.7 Proverbes 14.26 1 Timothée 2.8
16 Kwa kuwa utasahau mashaka yako; Utayakumbuka kama maji yaliyokwisha pita;
Esaïe 65.16 Ecclésiaste 5.20 Genèse 41.51 Esaïe 54.4 Esaïe 54.9
17 Na maisha yako yatakuwa meupe kuliko adhuhuri; Lijapokuwa ni giza, litakuwa kama alfajiri.
Psaumes 37.6 Esaïe 58.8-58.10 Job 42.11-42.17 Luc 2.26-2.32 Proverbes 4.18
18 Nawe utakuwa salama, kwa sababu kuna matumaini; Naam, utatafuta-tafuta kando yako, na kupumzika katika salama.
Psaumes 3.5 Psaumes 4.8 Proverbes 3.24-3.26 Lévitique 26.5-26.6 Proverbes 14.32
19 Tena utalala, wala hapana atakayekutia hofu; Naam, wengi watakutafuta uso wako.
Psaumes 45.12 Esaïe 60.14 Job 42.8-42.9 Apocalypse 3.9 Genèse 26.26-26.31
20 Lakini macho ya waovu yataingia kiwi, Nao hawatakuwa na njia ya kukimbilia, Na matumaini yao yatakuwa ni kutoa roho.
Deutéronome 28.65 Job 31.16 Job 17.5 Lamentations 4.17 Proverbes 20.20

Cette Bible est dans le domaine public.