Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Néhémie 4.14
Bible en Swahili de l’est


1 Lakini ikawa, Sanbalati aliposikia ya kwamba tulikuwa tukiujenga ukuta, akaghadhibika, akaingiwa na uchungu sana, akawadhihaki Wayahudi.
Néhémie 2.10 Néhémie 2.19 Matthieu 27.29 Hébreux 11.36 Psaumes 35.15-35.16
2 Akanena mbele ya nduguze na mbele ya jeshi la Samaria, akisema, Wayahudi hawa wanyonge wanafanyaje? Je! Watajifanyizia boma? Watatoa dhabihu? Au watamaliza katika siku moja? Je! Watayafufua mawe katika chungu hizi za kifusi, nayo yameteketezwa kwa moto?
Esdras 4.9-4.10 Néhémie 4.10 1 Samuel 14.11-14.12 Néhémie 12.27 Néhémie 12.43
3 Basi Tobia, Mwamoni, alikuwa karibu naye, akasema, Hata hiki wanachokijenga, angepanda mbweha, angeubomoa ukuta wao wa mawe.
Néhémie 2.10 1 Rois 20.10 Néhémie 6.1 2 Rois 18.23 Lamentations 5.18
4 Sikia, Ee Mungu wetu; maana tunadharauliwa; ukawarudishie mashutumu yao juu ya vichwa vyao, ukawatoe watekwe katika nchi ya uhamisho;
Psaumes 123.3-123.4 Psaumes 79.12 1 Samuel 17.26 Proverbes 3.34 Osée 12.14
5 wala usiusitiri uovu wao, wala isifutwe dhambi yao, mbele zako; kwa maana wamekukasirisha mbele ya hao wanaojenga.
Psaumes 109.14 Jérémie 18.23 Psaumes 69.27-69.28 Esaïe 43.25 Psaumes 51.1
6 Basi tukaujenga ukuta; nao ukuta wote ukaungamanishwa kiasi cha nusu ya kimo chake; maana watu walikuwa na moyo wa kufanya kazi.
Néhémie 6.15 Hébreux 13.21 Philippiens 2.13 Psaumes 110.3 1 Chroniques 29.17-29.18
7 Lakini ikawa, Sanbalati, na Tobia, na Waarabu, na Waamoni, na Waashdodi, waliposikia ya kuwa kazi ya kuzitengeneza kuta za Yerusalemu inaendelea, na ya kuwa mahali palipobomoka panaanza kuzibwa, basi wakaghadhibika mno;
Actes 4.17-4.18 Apocalypse 12.17 Néhémie 2.10 Néhémie 4.1 Amos 1.13
8 wakafanya shauri wote pamoja kuja kupigana na Yerusalemu, na kufanya machafuko humo.
Psaumes 83.3-83.11 Actes 23.12-23.13 Jérémie 20.10 Esaïe 8.9-8.10 Psaumes 2.1-2.3
9 Bali sisi tulimwomba dua Mungu wetu, tena tukaweka walinzi, mchana na usiku, kwa sababu yao, ili kuwapinga.
1 Pierre 5.8 Néhémie 4.11 Actes 4.24-4.30 Luc 21.36 Genèse 32.28
10 Wakasema Yuda, Nguvu zao wachukuao mizigo zimedhoofika, na kifusi tele zipo; tusiweze kuujenga ukuta.
Nombres 32.9 Ezéchiel 29.18 Nombres 13.31 Psaumes 11.1-11.2 Aggée 1.2
11 Nao adui zetu wakasema, Hawatajua wala kuona, hata tutakapokuja kati yao, na kuwaua, na kuikomesha kazi hiyo.
Actes 23.12 1 Thessaloniciens 5.2 2 Samuel 17.2 Actes 23.21 Juges 20.29-20.48
12 Kisha ikawa, Wayahudi walipokuja, wale waliokaa karibu nao, wakatuambia mara kumi, Kutoka kila mahali mtakaporejea watatushambulia.
Job 19.3 Genèse 31.7 Nombres 14.22 Genèse 31.41
13 Basi, nikaweka watu, mahali pa chini pa nafasi iliyokuwa nyuma ya ukuta, mahali palipokuwa wazi, kwa kadiri ya jamaa zao, nikawaweka wenye panga zao, na mikuki yao, na pinde zao.
Néhémie 4.17-4.18 Cantique 3.7-3.8 Psaumes 112.5 1 Corinthiens 14.20 Genèse 32.13-32.20
14 Nikatazama, nikaondoka, nikawaambia wakuu, na mashehe, na watu wengine waliobaki, Msiwaogope; mkumbukeni Bwana, aliye mkuu mwenye kuogofya, mkawapiganie ndugu zenu, na wana wenu, na binti zenu, na wake zenu, na nyumba zenu.
Nombres 14.9 2 Samuel 10.12 Esaïe 41.10-41.14 Deutéronome 1.29-1.30 Néhémie 1.5
15 Kisha ikawa, adui zetu waliposikia ya kuwa tumekwisha kupata habari, na ya kuwa Mungu amelibatilisha shauri lao, ndipo sisi sote tukarudi ukutani, kila mtu kwa kazi yake.
Romains 12.11 2 Samuel 17.14 Esaïe 44.25 Job 5.12-5.13 Psaumes 33.10-33.11
16 Ikawa tokea wakati huo, nusu ya watumishi wangu walitumika katika kazi hiyo, na nusu yao wakaishika mikuki, na ngao, na pinde, na darii; na maakida walikuwa nyuma ya nyumba yote ya Yuda.
Néhémie 5.15-5.16 Psaumes 101.6 Néhémie 4.23
17 Watu wale walioujenga ukuta, na wale waliochukua mizigo, walijitweka wenyewe, kila mtu alifanya kazi kwa mkono mmoja, na kwa mkono wake wa pili alishika silaha yake;
1 Corinthiens 16.9 1 Corinthiens 9.12 2 Timothée 2.3 Daniel 9.25 Philippiens 1.28
18 nao wajenzi, kila mtu alikuwa na upanga wake, umefungwa ubavuni mwake, ndivyo alivyojenga. Na yeye aliyepiga baragumu alikuwa karibu na mimi.
2 Chroniques 13.12-13.17 Nombres 10.9
19 Nikawaambia wakuu, na mashehe na watu wengine; Kazi hii ni nyingi, tena kubwa, nasi tumetawanyika juu ya ukuta, kila mtu mbali na mwenzake;
20 basi mahali po pote mtakaposikia sauti ya baragumu, enendeni huko, mkatujie; Mungu wetu atatupigania.
Deutéronome 1.30 Deutéronome 20.4 Exode 14.14 Josué 23.10 Deutéronome 3.22
21 Hivyo tukajitia katika kazi hiyo; na nusu yao waliishika mikuki, tangu alfajiri hata nyota zikatokea.
Galates 6.9 Colossiens 1.29 1 Corinthiens 15.58 1 Corinthiens 15.10
22 Kadhalika, wakati ule ule, nikawaambia watu, Kila mtu na akae ndani ya Yerusalemu pamoja na mtumishi wake, wapate kuwa walinzi wetu wakati wa usiku, na kufanya kazi wakati wa mchana.
Néhémie 11.1-11.2
23 Basi mimi, na ndugu zangu, na watumishi wangu, na watu wa ulinzi walionifuata, hatukuvua nguo zetu hata mmoja; kila mtu alikwenda kuteka maji akichukua silaha yake.
Néhémie 5.16 Juges 9.48 1 Corinthiens 15.10 Néhémie 7.2 Juges 5.11

Cette Bible est dans le domaine public.