Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 32.29
Bible en Swahili de l’est


Tentative d’invasion par Sanchérib

1 :Ikawa, baada ya mambo hayo, na uaminifu huo, Senakeribu, mfalme wa Ashuru, akaja, akaingia katika Yuda, akafanya marago juu ya miji yenye maboma, akadhania kwamba ataipata iwe yake.
2 Rois 18.13-18.37 2 Rois 17.6 Esaïe 36.1-37.38 Esaïe 8.6-8.8 2 Chroniques 20.1-20.2
2 Basi Hezekia, alipoona ya kuwa Senakeribu amekuja, na kuazimia kupigana na Yerusalemu,
Luc 9.53 Luc 9.51 2 Rois 12.17
3 akafanya shauri na wakuu wake, na mashujaa wake, kuzuia maji ya chemchemi zilizokuwa nje ya mji; nao wakamsaidia.
Proverbes 24.6 Romains 11.34 Esaïe 22.8-22.11 2 Rois 18.20 2 Rois 20.20
4 Wakakusanyika watu wengi, wakazizuia chemchemi zote, na kijito kilichopita kati ya nchi, wakisema, Kwa nini, wakifika wafalme wa Ashuru, waone maji mengi?
2 Chroniques 32.30 1 Rois 19.21 2 Chroniques 32.1 2 Rois 18.13 1 Rois 3.9
5 Akapiga moyo konde, akaujenga ukuta wote uliobomoka, akauinua sawa na minara, na ukuta wa pili nje, akaongeza nguvu ya Milo, katika mji wa Daudi, akafanya silaha na ngao tele.
2 Chroniques 25.23 1 Rois 9.24 2 Samuel 5.9 Esaïe 22.9-22.10 2 Rois 25.4
6 Akaweka maakida wa vita juu ya watu, akawakusanya kwake uwandani penye lango la mji, akawafurahisha mioyo; akisema,
2 Chroniques 30.22 Esaïe 40.2 Esdras 10.9 1 Chroniques 27.3-27.34 2 Chroniques 17.14-17.19
7 Iweni hodari, na wa moyo mkuu, msiogope, wala msifadhaike kwa sababu ya mfalme wa Ashuru, wala kwa majeshi yote walio pamoja naye; kwa maana yupo mkuu pamoja nasi kuliko aliye pamoja naye;
2 Rois 6.16 2 Chroniques 20.15 Esaïe 35.4 2 Rois 18.30 2 Timothée 2.1
8 kwake upo mkono wa mwili; ila kwetu yupo Bwana, Mungu wetu, kutusaidia, na kutupigania mapigano yetu. Na watu wakayategemea maneno ya Hezekia, mfalme wa Yuda.
Jérémie 17.5 2 Chroniques 20.17 2 Chroniques 13.12 2 Chroniques 20.15 Actes 18.10
9 Na baada ya hayo Senakeribu mfalme wa Ashuru, akatuma watumishi wake waende Yerusalemu, (naye alikuwapo mbele ya Lakishi, na uwezo wake wote pamoja naye,) kwa Hezekia, mfalme wa Yuda, na kwa Yuda wote waliokuwako Yerusalemu, kusema,
2 Rois 18.17 Josué 10.31 Michée 1.13 Josué 15.39 Esaïe 36.2
10 Senakeribu, mfalme wa Ashuru, asema hivi, Mwatumainia nini hata mkae mkihusuriwa katika Yerusalemu?
Esaïe 36.4 2 Rois 18.19
11 Siye Hezekia anayewashawishi, mtolewe kufa kwa njaa na kwa kiu, akisema, Bwana, Mungu wetu, atatuokoa na mkono wa mfalme wa Ashuru?
2 Rois 18.27 Psaumes 22.8 Psaumes 71.11 Psaumes 11.1-11.3 2 Chroniques 32.15
12 Si yeye Hezekia huyo aliyeondoa mahali pake pa juu, na madhabahu zake, akawaamuru Yuda na Yerusalemu, akisema, Abuduni mbele ya madhabahu moja, na juu yake mtafukiza uvumba?
2 Chroniques 31.1 2 Rois 18.22 Esaïe 36.7 2 Rois 18.4 Deutéronome 12.26-12.27
13 Je! Ninyi hamjui mimi na baba zangu tuliyowafanyia watu wote wa nchi? Je! Miungu ya mataifa wa nchi iliweza kuokoa kwa lo lote nchi zao na mkono wangu?
2 Rois 18.33-18.35 Esaïe 10.9-10.10 2 Rois 19.17-19.19 Jérémie 10.16 Daniel 4.37
14 Ni yupi miongoni mwa miungu ya mataifa wale walioharibiwa kabisa na baba zangu, aliyeweza kuwaokoa watu wake na mkono wangu, hata Mungu wenu aweze kuwaokoa ninyi na mkono wangu?
Exode 14.3 Exode 15.9-15.11 Esaïe 42.8 Esaïe 10.11-10.12
15 Basi sasa asiwadanganye Hezekia, wala asiwashawishi kwa hayo, wala msimwamini; kwa kuwa hapana mungu wa taifa lo lote, wala wa ufalme wo wote, aliyeweza kuwaokoa watu wake na mkono wangu, au na mkono wa baba zangu; sembuse Mungu wenu atawaokoaje ninyi na mkono wangu?
Daniel 3.15 Exode 5.2 Esaïe 36.18 2 Rois 19.10 2 Rois 18.29
16 Na watumishi wake wakazidi kusema juu ya Bwana Mungu, na juu ya Hezekia, mtumishi wake.
Psaumes 73.9 Jean 15.21 Job 15.25-15.26
17 Tena akaandika waraka, kumtukana Bwana, Mungu wa Israeli, na kumwambia, akisema, Kama vile miungu ya mataifa wa nchi isivyowaokoa watu wao na mkono wangu, vivyo hivyo Mungu wa Hezekia hatawaokoa watu wake na mkono wangu.
Esaïe 37.14 2 Rois 19.12 Esaïe 37.28-37.29 Apocalypse 13.6 2 Rois 19.28
18 Wakawalilia kwa sauti kuu, kwa lugha ya Kiyahudi, watu wa Yerusalemu waliokuwako ukutani ili kuwaogofisha, na kuwafadhaisha; hata wapate kuutwaa mji.
1 Samuel 17.10 2 Rois 18.26-18.28 1 Samuel 17.26 Esaïe 36.13 Néhémie 6.9
19 Wakamnenea Mungu wa Yerusalemu, kana kwamba kuitaja miungu ya mataifa wa nchi, iliyo kazi ya mikono ya watu.
2 Rois 19.18 Esaïe 2.8 Deutéronome 4.28 Jérémie 10.9 Deutéronome 27.15
20 Na kwa ajili ya hayo Hezekia mfalme, na Isaya nabii, mwana wa Amozi, wakaomba, wakalia hata mbinguni.
2 Chroniques 14.11 2 Chroniques 20.6-20.12 Esaïe 37.1-37.4 Esaïe 37.14-37.20 Psaumes 91.14-91.15
21 Naye Bwana akatuma malaika aliyewakatia mbali mashujaa wote, na majemadari, na maakida, matuoni mwa mfalme wa Ashuru. Basi akarudia nchi yake mwenye haya ya uso. Naye alipoingia nyumbani mwa mungu wake, wale waliotoka viunoni mwake mwenyewe wakamwangamiza humo kwa upanga.
Esaïe 33.10-33.12 Psaumes 18.50 Daniel 3.28 Actes 12.23 2 Rois 19.35-19.37
22 Ndivyo Bwana alivyomwokoa Hezekia, na wenyeji wa Yerusalemu, na mkono wa Senakeribu, mfalme wa Ashuru, na mikononi mwa wote, akawaongoza pande zote.
Psaumes 71.20-71.21 Esaïe 58.11 Esaïe 31.4-31.5 Psaumes 73.24 Psaumes 18.48-18.50
23 Watu wengi walimletea Bwana zawadi huko Yerusalemu, na vitu vya thamani kwa Hezekia, mfalme wa Yuda; hata yeye akatukuka tangu wakati ule machoni pa mataifa yote.
2 Chroniques 17.5 2 Chroniques 9.24 2 Chroniques 1.1 Matthieu 2.11 1 Rois 10.10

Maladie et guérison d’Ézéchias

24 Katika siku hizo Hezekia akaugua akawa katika hatari ya kufa; akamwomba Bwana; naye akasema naye, akampa ishara.
Esaïe 38.1-38.8 2 Rois 20.1-20.11 Esaïe 38.21-38.22
25 Walakini kadiri alivyofadhiliwa Hezekia hakumrudishia vivyo; kwa kuwa moyo wake ulitukuka; kwa hiyo ikawako hasira juu yake, na juu ya Yuda na Yerusalemu.
2 Chroniques 26.16 2 Chroniques 24.18 2 Chroniques 32.31 2 Rois 14.10 1 Chroniques 21.12-21.17
26 Hata hivyo Hezekia akajinyenyekeza kwa ajili ya huku kutukuka kwa moyo wake, yeye na wenyeji wa Yerusalemu, hata haikuwajia hasira ya Bwana siku za Hezekia.
Jérémie 26.18-26.19 Jacques 4.10 2 Chroniques 33.12 2 Chroniques 34.27-34.28 2 Chroniques 33.23
27 Naye Hezekia akawa na mali nyingi mno na heshima; akajifanyizia hazina za fedha, na za dhahabu, na za vito, na za manukato, na za ngao, na za namna zote za vyombo vya thamani;
2 Chroniques 1.12 Proverbes 10.22 2 Chroniques 9.27 1 Chroniques 27.25-27.31 2 Chroniques 17.5
28 ghala pia za mazao ya nafaka na mvinyo na mafuta; na malisho ya wanyama wa namna zote, na makundi mazizini.
1 Rois 4.26 2 Chroniques 26.10 2 Samuel 7.8
29 Tena akajifanyizia miji, na mali za kondoo na ng’ombe kwa wingi; maana Mungu alimtajirisha sana sana.
1 Chroniques 29.12 2 Chroniques 25.9 2 Chroniques 26.10 Deutéronome 8.18 Genèse 13.2-13.6
30 Naye huyo Hezekia ndiye aliyezuia chemchemi ya juu ya maji ya Gihoni, akayaleta chini moja kwa moja upande wa magharibi wa mji wa Daudi. Akafanikiwa Hezekia katika kazi zake zote.
1 Rois 1.33 1 Rois 1.45 Esaïe 22.9-22.11 Psaumes 1.1-1.3 2 Chroniques 32.4
31 Walakini kwa habari ya wajumbe wa wakuu wa Babeli, waliotuma kwake kuuliza ajabu iliyofanywa katika nchi, Mungu akamwacha, ili amjaribu, ili kwamba ayajue yote yaliyokuwamo moyoni mwake.
Deutéronome 8.2 Genèse 22.1 2 Chroniques 32.24 Deutéronome 8.16 2 Rois 20.8-20.13
32 Basi mambo yote ya Hezekia yaliyosalia, na matendo yake mema, tazama, yameandikwa katika maono ya Isaya nabii, mwana wa Amozi, katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
2 Rois 18.1-18.20 Esaïe 36.1-36.22 2 Chroniques 31.20-31.21
33 Hezekia akalala na babaze, wakamzika mahali pa kupandia makaburi ya wana wa Daudi; nao Yuda wote na wenyeji wa Yerusalemu wakamfanyia heshima alipokufa. Na Manase mwanawe akatawala mahali pake.
Proverbes 10.7 Genèse 50.10-50.11 2 Chroniques 16.14 1 Samuel 25.1 Deutéronome 34.8

Cette Bible est dans le domaine public.