Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 24.25
Bible en Swahili de l’est


Répartition des prêtres en classes

1 Na zamu za wana wa Haruni ni hizi. Wana wa Haruni; Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamari.
Exode 6.23 Nombres 3.2 1 Chroniques 23.6 Nombres 26.60 1 Chroniques 6.3
2 Lakini hao Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, wala hawakuwa na watoto; kwa hiyo Eleazari na Ithamari wakafanya ukuhani.
Lévitique 10.2 Nombres 3.4 Nombres 26.61 Exode 24.9 Exode 24.1
3 Akawagawanya Daudi, na Sadoki wa wana wa Eleazari, na Ahimeleki wa wana wa Ithamari, katika utumishi kwa kadiri ya usimamizi wao.
2 Samuel 8.17 1 Chroniques 24.31 1 Chroniques 12.27-12.28 1 Chroniques 16.39 1 Chroniques 24.6
4 Wakaonekana wakuu wengi wa wana wa Eleazari kuliko wa wana wa Ithamari; wakagawanyika hivi; wa wana wa Eleazari kulikuwa na kumi na sita, waliokuwa wakuu wa mbari za baba zao; na wa wana wa Ithamari, sawasawa na mbari za baba zao, wanane.
1 Chroniques 15.6-15.12 Nombres 25.11-25.13 1 Chroniques 23.24
5 Ndivyo walivyogawanyika kwa kura, wao kwa wao; kwani kulikuwa na wakuu wa patakatifu, na wakuu wa Mungu, wa wana wa Eleazari, na wa wana wa Ithamari pia.
1 Chroniques 24.31 Actes 1.26 Matthieu 27.1 Matthieu 26.3 Néhémie 11.11
6 Naye Shemaya, mwana wa Nethaneli, mwandishi, aliyekuwa wa Walawi, akawaandika mbele ya mfalme, na mbele ya wakuu, na Sadoki kuhani, na Ahimeleki, mwana wa Abiathari, na wakuu wa mbari za baba za makuhani, na za Walawi; ikatwaliwa ya Eleazari mbari moja ya baba, na moja ikatwaliwa ya Ithamari.
1 Chroniques 18.16 Matthieu 8.19 1 Rois 4.3 Matthieu 13.52 2 Chroniques 34.13
7 Kura ya kwanza ikamtokea Yehoiaribu, na ya pili Yedaya;
Esdras 2.36 1 Chroniques 9.10 Néhémie 11.10 Néhémie 7.39 Néhémie 12.19
8 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu;
Esdras 2.39 Néhémie 12.15 Néhémie 7.35 Esdras 10.21
9 ya tano Malkia, ya sita Miyamini;
Néhémie 12.17
10 ya saba Hakosi, ya nane Abia;
Luc 1.5 Néhémie 12.4 Néhémie 12.17
11 ya kenda Yeshua, ya kumi Shekania;
Néhémie 12.10 Esdras 2.36 Néhémie 7.39
12 ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu;
Néhémie 12.10
13 ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu;
14 ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri;
Esdras 2.37 Néhémie 7.40 Esdras 10.20
15 ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi;
16 ya kumi na kenda Pethahia, ya ishirini Ezekieli;
17 ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli;
18 ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
19 Huu ndio usimamizi wao katika huduma yao, waingie nyumbani mwa Bwana kwa kadiri ya agizo lao, kwa mkono wa Haruni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyomwamuru.
1 Chroniques 9.25 1 Corinthiens 14.40 2 Chroniques 23.8 2 Chroniques 23.4 1 Chroniques 24.1

Chefs des Lévites

20 Na wa wana wa Lawi, waliosalia; wa wana wa Amramu, Shebueli; wa wana wa Shebueli, Yedeya.
1 Chroniques 26.24 1 Chroniques 23.16 1 Chroniques 6.18 1 Chroniques 23.12-23.14
21 Wa Rehabia; wa wana wa Rehabia, Ishia mkuu wao.
1 Chroniques 23.17 1 Chroniques 26.25
22 Wa Waishari, Shelomothi; wa wana wa Shelomothi, Yahathi.
1 Chroniques 23.18 Nombres 3.19 1 Chroniques 26.26 Nombres 3.27 Exode 6.21
23 Na wana wa Hebroni; Yeria mkuu wao, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, Yekameamu wa nne.
1 Chroniques 23.19 1 Chroniques 26.31
24 Wana wa Uzieli, Mika; wa wana wa Mika, Shamiri.
1 Chroniques 23.20
25 Nduguye Mika, Ishia; wa wana wa Ishia, Zekaria.
1 Chroniques 15.18 1 Chroniques 15.20 1 Chroniques 23.20
26 Wana wa Merari; Mali na Mushi; wana wa Yaazia; Beno.
1 Chroniques 23.21
27 Wana wa Merari; wa Yaazia; Beno, na Shohamu, na Zakuri, na Ibri.
Exode 6.19 1 Chroniques 23.21 1 Chroniques 6.19 Nombres 3.20
28 Wa Mali; Eleazari, asiyekuwa na wana.
1 Chroniques 23.22
29 Wa Kishi; wana wa Kishi; Yerameeli.
30 Na wana wa Mushi; Mali, na Ederi, na Yeremothi. Hao ndio wana wa Walawi, kwa kufuata mbari za baba zao.
1 Chroniques 23.23 1 Chroniques 6.47
31 Hao nao wakatupiwa kura vile vile, kama ndugu zao wana wa Haruni, machoni pa Daudi mfalme, na Sadoki, na Ahimeleki, na wakuu wa mbari za baba za makuhani na za Walawi; mbari za baba za mkuu, vile vile kama za nduguye mdogo.
1 Chroniques 24.5-24.6 1 Chroniques 25.8 1 Chroniques 26.13 Nombres 26.56

Cette Bible est dans le domaine public.