Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 19.11
Bible en Swahili de l’est


Guerre contre les Ammonites et leurs alliés

1 Ikawa baada ya hayo, Nahashi, mfalme wa wana wa Amoni, akafa, akamiliki mwanawe mahali pake.
1 Samuel 12.12 2 Samuel 10.1-10.19 1 Samuel 11.1-11.2
2 Naye Daudi akasema, Nitamtendea wema Hanuni, mwana wa Nahashi, kwa kuwa babaye alinitendea mimi wema. Basi Daudi akapeleka wajumbe ili kumtuliza kwa habari za babaye. Wakaja watumishi wa Daudi katika nchi ya wana wa Amoni kwa Hanuni, ili wamtulize.
Deutéronome 23.3-23.6 Genèse 19.37-19.38 Néhémie 4.7 2 Samuel 9.1 2 Samuel 9.7
3 Lakini wakuu wa wana wa Amoni wakamwambia Hanuni, Je! Waona Daudi amheshimu babayo kwa kukupelekea wafariji? Je! Hawakukujia watumishi wake ili kuiangalia nchi, na kuiangamiza, na kuipeleleza?
1 Rois 12.8-12.11 Juges 18.8-18.10 Josué 2.1-2.3 Juges 1.23-1.24 1 Samuel 29.9
4 Basi Hanuni akawatwaa watumishi wa Daudi, akawanyoa, akawakatia nguo zao katikati, hata matakoni, akawatoa waende zao.
Jérémie 41.5 Esaïe 47.2-47.3 Lévitique 19.27 Luc 20.10-20.11 Jérémie 48.37
5 Wakaenda watu wakamwambia Daudi jinsi walivyotendewa wale watu. Naye akatuma watu kuwalaki; kwa sababu watu hao walikuwa wametahayarika sana. Mfalme akasema, Ngojeni Yeriko, hata mtakapoota ndevu zenu, ndipo mrudi.
1 Rois 16.34 Juges 16.22 Matthieu 18.31 Josué 6.24-6.26
6 Na wana wa Amoni walipoona ya kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, Hanuni na wana wa Amoni wakapeleka talanta elfu za fedha ili kujiajiria magari na wapanda farasi kutoka Mesopotamia, na kutoka Atam-maaka, na kutoka Soba.
2 Samuel 10.6 1 Chroniques 18.9 1 Chroniques 18.5 Genèse 34.30 2 Chroniques 18.3
7 Basi wakajiajiria magari thelathini na mbili elfu, na mfalme wa Maaka na watu wake; nao walikuja wakatua mbele ya Medeba. Na wana wa Amoni wakakusanyika kutoka miji yao, wakaja vitani.
Josué 13.9 Nombres 21.30 Josué 13.16 Esaïe 15.2 1 Chroniques 18.4
8 Basi Daudi aliposikia habari akamtuma Yoabu, na jeshi lote la mashujaa.
2 Samuel 23.8-23.39 1 Chroniques 11.6 1 Chroniques 11.10-11.47
9 Wakatoka wana wa Amoni, wakapanga vita langoni pa mji; na hao wafalme waliokuja walikuwa peke yao uwandani.
2 Samuel 10.8 2 Samuel 18.4 1 Rois 20.1 2 Chroniques 13.3 2 Chroniques 14.10
10 Basi Yoabu alipoona ya kwamba uso wa vita umekuwa juu yake mbele na nyuma, akachagua baadhi ya wateule wote wa Israeli, akawapanga juu ya Washami.
Josué 8.22 Juges 20.42-20.43 2 Samuel 10.9-10.14
11 Na hao watu waliosalia akawatia mikononi mwa Abishai, nduguye, nao wakajipanga juu ya wana wa Amoni.
1 Chroniques 18.12 1 Chroniques 19.9 1 Chroniques 11.20
12 Akasema, Wakiwa Washami ni hodari mno kwangu, ndipo wewe utanisaidia; lakini wana wa Amoni wakiwa ni hodari mno kwako, ndipo mimi nitakusaidia wewe.
Philippiens 1.27-1.28 Néhémie 4.20 Ecclésiaste 4.9-4.12 Galates 6.2
13 Uwe hodari, tukajitie moyo mkuu kwa ajili ya watu wetu, na kwa ajili ya miji ya Mungu wetu; naye Bwana afanye yaliyo mema machoni pake.
Esdras 10.4 Deutéronome 31.6-31.7 Josué 1.7 Juges 10.15 2 Samuel 15.26
14 Basi Yoabu, na watu waliokuwa pamoja naye, wakakaribia kupigana na Washami; nao wakakimbia mbele yake.
1 Rois 20.19-20.21 Jérémie 46.15-46.16 1 Rois 20.13 2 Chroniques 13.5-13.16 1 Rois 20.28-20.30
15 Na wana wa Amoni walipoona ya kwamba Washami wamekimbia, wakakimbia nao mbele ya Abishai, nduguye, wakaingia mjini. Ndipo Yoabu akaja Yerusalemu.
Romains 8.31 Lévitique 26.7
16 Na Washami walipojiona kuwa wameshindwa mbele ya Israeli, wakapeleka wajumbe, wakawavuta Washami walioko ng’ambo ya Mto, na Shobaki, jemadari wa jeshi la Hadadezeri, akawaongoza.
2 Samuel 10.16 Psaumes 2.1 Esaïe 8.9 Michée 4.11-4.12 Zacharie 14.1-14.3
17 Alipoambiwa Daudi; akakusanya Israeli wote, akavuka Yordani, akawajia, akapanga vita juu yao. Basi Daudi alipopanga vita juu ya Washami, wakapigana naye.
Esaïe 22.6-22.7 1 Chroniques 19.9
18 Washami wakakimbia mbele ya Israeli; naye Daudi akawaua katika Washami watu wa magari saba elfu, na askari waendao kwa miguu arobaini elfu, akamwua na Shobaki, jemadari wa jeshi.
2 Samuel 10.18 Psaumes 18.32 1 Chroniques 19.13-19.14 Psaumes 46.11 Psaumes 33.16
19 Na watumwa wa Hadadezeri walipojiona kuwa wameshindwa mbele ya Israeli, walifanya amani na Daudi, wakamtumikia; wala Washami hawakukubali kuwasaidia wana wa Amoni tena.
Genèse 14.4-14.5 Esaïe 10.8 2 Samuel 10.19 Psaumes 48.3-48.6 1 Chroniques 14.17

Cette Bible est dans le domaine public.