Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 3.20
Bible en Swahili de l’est


Apparition de Dieu à Salomon

1 Huyo Sulemani akafanya ujamaa na Farao, mfalme wa Misri, akamwoa binti yake Farao, akamleta mjini mwa Daudi, hata alipokwisha kuijenga nyumba yake, na nyumba ya Bwana, na ukuta wa kuuzunguka Yerusalemu.
1 Rois 9.24 2 Samuel 5.7 2 Chroniques 2.1-2.4 2 Chroniques 18.1 1 Rois 11.1
2 Ila watu walikuwa wakichinja dhabihu katika mahali pa juu, kwa sababu haikuwapo nyumba iliyojengwa kwa jina la Bwana, hata siku zile.
1 Rois 22.43 Deutéronome 12.2-12.5 1 Chroniques 17.4-17.6 1 Chroniques 28.3-28.6 Actes 7.47-7.49
3 Sulemani naye akampenda Bwana, akienda katika amri za Daudi babaye, ila hutoa dhabihu na kufukiza uvumba katika mahali pa juu.
Deutéronome 6.5 Psaumes 31.23 Deutéronome 30.16 1 Corinthiens 8.3 1 Rois 3.6
4 Basi mfalme akaenda Gibeoni, ili atoe dhabihu huko; kwa kuwa ndipo mahali pa juu palipo pakuu. Sulemani akatoa sadaka elfu za kuteketezwa juu ya madhabahu ile.
1 Chroniques 16.39 1 Chroniques 21.29 2 Chroniques 1.3 2 Chroniques 1.6-1.12 Josué 9.3
5 Na huko Gibeoni Bwana akamtokea Sulemani katika ndoto ya usiku; Mungu akamwambia, Omba utakalo nikupe.
1 Rois 9.2 Matthieu 1.20 Nombres 12.6 1 Rois 11.9 Jacques 1.5-1.6
6 Sulemani akasema, Umemfanyia mtumwa wako Daudi baba yangu fadhili kuu, kadiri alivyoenenda mbele zako katika kweli, na katika haki, na katika unyofu wa moyo pamoja nawe; nawe umemwekea na fadhili hii kubwa, maana umempa mwana wa kuketi kitini pake kama ilivyo leo.
1 Rois 9.4 1 Rois 1.48 1 Rois 2.4 Psaumes 15.2 2 Samuel 7.8-7.12
7 Na sasa, Ee Bwana, Mungu wangu, umenitawaza niwe mfalme mimi mtumwa wako badala ya Daudi baba yangu; nami ni mtoto mdogo tu; sijui jinsi inipasavyo kutoka wala kuingia.
1 Chroniques 29.1 Nombres 27.17 Jérémie 1.6 Psaumes 121.8 Deutéronome 31.2
8 Na mtumwa wako yu katikati ya watu wako uliowachagua, watu wengi wasioweza kuhesabiwa, wala kufahamiwa idadi yao, kwa kuwa ni wengi.
Genèse 15.5 Genèse 22.17 Genèse 13.16 Deutéronome 7.6-7.8 1 Samuel 12.22
9 Kwa hiyo nipe mimi mtumwa wako moyo wa adili niwahukumu watu wako, na kupambanua mema na mabaya; maana ni nani awezaye kuwahukumu hawa watu wako walio wengi?
Jacques 1.5 2 Samuel 14.17 Psaumes 72.1-72.2 Proverbes 2.3-2.9 Hébreux 5.14
10 Neno hili likawa jema machoni pa Bwana, ya kuwa Sulemani ameomba neno hili.
Proverbes 15.8
11 Mungu akamwambia, Kwa kuwa umeomba neno hili, wala hukujitakia maisha ya siku nyingi; wala hukutaka utajiri kwa nafsi yako; wala hukutaka roho za adui zako; bali umejitakia akili za kujua kuhukumu;
Romains 8.26 1 Rois 3.9 Matthieu 20.21-20.22 Proverbes 16.31 Psaumes 4.6
12 basi, tazama, nimefanya kama ulivyosema. Tazama, nimekupa moyo wa hekima na wa akili; hata kabla yako hapakuwa na mtu kama wewe, wala baada yako hatainuka mtu kama wewe.
1 Jean 5.14-5.15 1 Rois 5.12 Ecclésiaste 1.16 1 Rois 10.23-10.24 2 Chroniques 2.12
13 Na mambo yale usiyoyaomba nimekupa, mali na fahari, hata hapatakuwa na mtu katika wafalme kama wewe, siku zako zote.
Matthieu 6.33 Proverbes 3.16 Ephésiens 3.20 1 Rois 4.21-4.24 Psaumes 84.11-84.12
14 Nawe ukienda katika njia zangu, na kuyashika mausia yangu, na amri zangu, kama baba yako Daudi alivyokwenda, basi nitazifanya siku zako kuwa nyingi.
Psaumes 91.16 Proverbes 3.2 Proverbes 3.16 1 Rois 3.6 1 Rois 15.5
15 Naye Sulemani akaamka, na kumbe! Ni ndoto. Akaenda Yerusalemu, akasimama mbele ya sanduku la agano la Bwana, akatoa sadaka za kuteketezwa, akatoa na sadaka za amani; akawafanyia karamu watumishi wake wote.
Genèse 41.7 1 Rois 8.65 Daniel 5.1 Marc 6.21 Esther 1.3

Le sage jugement de Salomon

16 Ndipo wanawake wawili, makahaba, walimwendea mfalme, wakasimama mbele yake.
Lévitique 19.29 Deutéronome 23.17 Juges 11.1 Nombres 27.2 Exode 18.16
17 Na mwanamke mmoja akasema, Ee bwana wangu, mimi na mwanamke huyu tunakaa katika nyumba moja; nami nalizaa nilipokuwa pamoja naye nyumbani.
Romains 13.7 Genèse 43.20
18 Kisha, siku ya tatu baada ya kuzaa kwangu, ikawa mwanamke huyu naye akazaa; na sisi tulikuwa pamoja; hapakuwa na mtu mwingine pamoja nasi nyumbani, isipokuwa sisi wawili tu.
19 Na mtoto wa mwanamke huyu akafa usiku, maana alimlalia.
20 Akaondoka kati ya usiku, akamwondoa mtoto wangu ubavuni pangu, mimi mjakazi wako nilipokuwa usingizini, akamweka kifuani pake, na mtoto wake mwenyewe, aliyekuwa amekufa, akamweka kifuani pangu.
Matthieu 13.25 Jean 3.20 Job 24.13-24.17 Psaumes 139.11
21 Nilipoondoka asubuhi nimnyonyeshe mtoto wangu, kumbe? Amekufa. Hata asubuhi nilipomtazama sana, kumbe! Siye mtoto wangu niliyemzaa.
Lamentations 4.3-4.4 1 Samuel 1.23 Genèse 21.7
22 Ndipo yule mwanamke wa pili akasema, Sivyo hivyo; bali mtoto wangu ndiye aliye hai, na mtoto wako ndiye aliyekufa. Na mwenzake akasema, Sivyo hivyo; bali mtoto wako ndiye aliyekufa, na mtoto wangu ndiye aliye hai. Ndivyo walivyosema mbele ya mfalme.
23 Ndipo mfalme akasema, Huyu anasema, Mtoto wangu yu hai, na mtoto wako amekufa. Na huyu anasema, Sivyo hivyo; bali mtoto aliyekufa ni wako, na mtoto aliye hai ni wangu.
24 Mfalme akasema, Nileteeni upanga. Wakaleta upanga mbele ya mfalme.
25 Mfalme akasema, Mkate mtoto aliye hai vipande viwili, kampe huyu nusu, na huyu nusu.
Proverbes 25.8
26 Ndipo mwanamke yule, ambaye mtoto aliye hai ni wake, akamwambia mfalme kwa maana moyoni mwake alimwonea mtoto wake huruma, akasema, Ee bwana wangu, mpe huyu mtoto aliye hai, wala usimwue kamwe. Lakini yule mwingine akasema, Asiwe wangu wala wako; na akatwe.
Jérémie 31.20 Esaïe 49.15 Genèse 43.30 Osée 11.8 Philippiens 2.1
27 Ndipo mfalme akajibu, akasema, Mpe huyu wa kwanza mtoto aliye hai, maana yeye ndiye mama yake.
28 Na Israeli wote wakapata habari za hukumu ile aliyoihukumu mfalme wakamwogopa mfalme; maana waliona ya kuwa hekima ya Mungu ilikuwa ndani yake, ili afanye hukumu.
Colossiens 2.3 Esdras 7.25 1 Rois 3.9-3.12 1 Corinthiens 1.30 Exode 14.31

Cette Bible est dans le domaine public.