Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 21.19
Bible en Swahili de l’est


Achab et la vigne de Naboth

1 Ikawa baada ya hayo, Nabothi Myezreeli alikuwa na shamba la mizabibu katika Yezreeli, karibu na nyumba ya kifalme ya Ahabu mfalme wa Samaria.
1 Rois 18.45-18.46 2 Chroniques 28.22 Juges 6.33 1 Samuel 29.1 1 Rois 20.35-20.43
2 Ahabu akasema na Nabothi, akamwambia, Nipe shamba lako la mizabibu nilifanye shamba la mboga, maana ni karibu na nyumba yangu; nami nitakupa badala yake shamba la mizabibu lililo zuri zaidi; au ukipenda, nitakupa fedha sawasawa na thamani yake.
1 Samuel 8.14 Cantique 4.15 Genèse 3.6 Deutéronome 5.21 Exode 20.17
3 Nabothi akamwambia Ahabu, Bwana apishe mbali nikupe wewe urithi wa baba zangu.
Lévitique 25.23 Nombres 36.7 Ezéchiel 46.18 Romains 6.2 Galates 6.14
4 Basi Ahabu akaenda nyumbani kwake, ana moyo mzito, tena amekasirika, kwa sababu ya neno lile aliloambiwa na Nabothi Myezreeli, akisema, Sitakupa urithi wa baba zangu. Akajilaza kitandani pake, akageuza uso wake, akakataa kula.
1 Rois 20.43 Jacques 1.14 Esaïe 57.20-57.21 Ecclésiaste 6.9 Nombres 22.13-22.14
5 Lakini Yezebeli mkewe akamwendea, akamwambia, Kwa nini roho yako ina huzuni hata usile chakula?
Esther 4.5 1 Rois 16.31 Néhémie 2.2 1 Rois 18.4 1 Rois 19.2
6 Akamwambia, Kwa sababu nimesema na Nabothi Myezreeli, nikamwambia, Unipe shamba lako la mizabibu kwa fedha, au, ukipenda, nitakupa shamba la mizabibu lingine badala yake. Akajibu, Sitakupa shamba langu la mizabibu.
1 Timothée 6.9-6.10 1 Rois 21.2-21.4 Jacques 4.2-4.7 Proverbes 14.30 Esther 6.12
7 Yezebeli mkewe akamwambia, Je! Sasa wewe unaumiliki ufalme wa Israeli? Ondoka, ule chakula, moyo wako ufurahi; mimi nitakupa shamba la mizabibu la Nabothi Myezreeli.
1 Samuel 8.4 Ecclésiaste 4.1 1 Samuel 8.14 2 Samuel 13.4 Michée 7.3
8 Basi, akaandika nyaraka kwa jina la Ahabu, akazitia muhuri yake, akazipeleka zile nyaraka kwa wazee, na kwa watu wenye nguvu waliokuwa katika mji wake, waliokaa pamoja na Nabothi.
1 Rois 20.7 2 Samuel 11.14-11.15 Néhémie 6.5 Esdras 4.7-4.8 Deutéronome 21.1-21.9
9 Akaandika katika zile nyaraka, akasema, Pigeni mbiu ya watu kufunga, mkamweke Nabothi juu mbele ya watu,
Esaïe 58.4 Matthieu 2.8 Luc 20.47 Jean 18.28 Matthieu 23.13
10 mkainue watu wawili, watu wasiofaa, ili wamshitaki, na kumshuhudia, kunena, Umemtukana Mungu na mfalme. Kisha mchukueni nje, mkampige kwa mawe, ili afe.
Actes 6.11 Exode 22.28 Lévitique 24.15-24.16 Deutéronome 13.13 Actes 6.13
11 Wale wazee wa mji wake, na walio wenye nguvu waliokaa mjini mwake, wakafanya kama Yezebeli alivyowaagiza, kama ilivyoandikwa katika nyaraka alizowapelekea.
Exode 1.21 2 Chroniques 24.21 2 Rois 10.6-10.7 Daniel 3.18-3.25 Exode 23.1-23.2
12 Wakapiga mbiu ya watu kufunga, wakamweka Nabothi juu mbele ya watu.
Esaïe 58.4 1 Rois 21.8-21.10
13 Na hao watu wawili, watu wasiofaa, wakaingia, wakaketi mbele yake; wale watu wasiofaa wakamshuhudia Nabothi mbele ya watu, wakasema, Nabothi amemtukana Mungu na mfalme. Ndipo wakamchukua nje ya mji, wakampiga kwa mawe hata akafa.
2 Rois 9.26 Job 2.9 Proverbes 25.18 Deutéronome 13.10 Proverbes 19.5
14 Wakampelekea Yezebeli habari, wakasema, Nabothi amepigwa kwa mawe, amekufa.
Ecclésiaste 5.8 2 Samuel 11.14-11.24 Ecclésiaste 8.14
15 Ikawa Yezebeli aliposikia ya kwamba Nabothi amepigwa kwa mawe na kufa, Yezebeli akamwambia Ahabu, Inuka, ulitamalaki shamba la mizabibu la Nabothi Myezreeli, alilokataa kukupa kwa fedha, maana Nabothi hako hai, lakini amekufa.
Proverbes 1.10-1.16 Proverbes 4.17 1 Rois 21.7
16 Ikawa Ahabu aliposikia ya kwamba Nabothi amekufa, akaondoka, alitelemkie shamba la mizabibu la Nabothi Myezreeli, ili alitamalaki.
2 Samuel 11.25-11.27 Psaumes 50.18 2 Samuel 23.15-23.17 Abdias 1.12-1.14 2 Samuel 4.9-4.12
17 Neno la Bwana likamjia Eliya Mtishbi, kusema,
Psaumes 9.12 Esaïe 26.21 2 Rois 1.15-1.16 2 Rois 5.26
18 Ondoka, ushuke, ukutane na Ahabu mfalme wa Israeli, akaaye katika Samaria; yuko katika shamba la mizabibu la Nabothi, ndiko alikoshukia ili alitamalaki.
1 Rois 13.32 2 Chroniques 22.9
19 Ukamwambie, ukisema, Bwana asema hivi, Je! Umeua, ukatamalaki? Nawe utamwambia, kusema, Bwana asema hivi, Mahali pale mbwa walipoiramba damu ya Nabothi, mbwa watairamba na damu yako, naam, damu yako.
1 Rois 22.38 2 Samuel 12.9 Genèse 3.11 2 Rois 9.25-9.26 Juges 1.7
20 Ahabu akamwambia Eliya, Je! Umenipata, ewe adui yangu? Akamwambia, Nimekupata, kwa sababu umejiuza utende yaliyo mabaya machoni pa Bwana.
1 Rois 18.17 Romains 7.14 1 Rois 21.25 2 Rois 17.17 Apocalypse 11.10
21 Angalia, nitaleta mabaya juu yako; nami nitakuangamiza kabisa, nitamkatia Ahabu kila mume, aliyefungwa na aliyeachwa katika Israeli.
1 Rois 14.10 1 Samuel 25.34 Exode 20.5-20.6 2 Rois 10.17 2 Rois 9.7-9.9
22 Kisha nitaifanya nyumba yako iwe kama nyumba ya Yeroboamu mwana wa Nebati, na kama nyumba ya Baasha mwana wa Ahiya, kwa ajili ya chukizo ulilonichukiza, hata kunighadhibisha, ukawakosesha Israeli.
1 Rois 16.3 1 Rois 16.11 1 Rois 14.16 1 Rois 16.26 1 Rois 15.34
23 Tena Bwana alinena habari za Yezebeli, akisema, Mbwa watamla Yezebeli katika kiwanja cha Yezreeli.
2 Rois 9.10 2 Rois 9.30-9.37 1 Rois 21.25
24 Mtu wa nyumba ya Ahabu afaye mjini, mbwa watamla, na yeye afaye mashambani ndege wa angani watamla.
1 Rois 16.4 1 Rois 14.11 Jérémie 15.3 Apocalypse 19.18 Esaïe 14.19
25 (Lakini hapakuwa na mtu kama Ahabu, aliyejiuza atende maovu machoni pa Bwana ambaye Yezebeli mkewe alimchochea.
1 Rois 21.20 1 Rois 16.30-16.33 Actes 6.12 1 Rois 18.4 Romains 6.19
26 Akachukiza mno, kwa kuzifuata sanamu sawasawa na yote waliyoyafanya Waamori, Bwana aliowafukuza mbele ya wana wa Israeli.)
2 Rois 21.11 Genèse 15.16 Lévitique 18.25-18.30 Ezéchiel 16.47 Lévitique 20.22-20.23
27 Ikawa, Ahabu alipoyasikia maneno hayo, akayararua mavazi yake, akavaa magunia mwilini mwake, akafunga, akajilaza juu ya magunia, akaenda kwa upole.
2 Rois 6.30 Genèse 37.34 2 Samuel 3.31 Joël 1.13 2 Rois 18.37
28 Neno la Bwana likaja kwa Eliya Mtishbi, kusema,
29 Huoni jinsi Ahabu alivyojidhili mbele yangu? Basi kwa sababu amejidhili mbele yangu, sitayaleta yale mabaya katika siku zake; ila katika siku za mwanawe nitayaleta mabaya hayo juu ya nyumba yake.
2 Rois 9.25-9.26 Luc 7.44 Romains 2.4 Psaumes 18.44 Jérémie 7.17

Cette Bible est dans le domaine public.