Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 18
Bible en Swahili de l’est


Confrontation entre Élie et les prophètes de Baal

1 Ikawa baada ya siku nyingi, neno la Bwana likamjia Eliya, katika mwaka wa tatu, kusema, Enenda, ukajionyeshe kwa Ahabu; nami nitaleta mvua juu ya nchi.
Luc 4.25 Jacques 5.17 1 Rois 17.1 Deutéronome 28.12 Lévitique 26.4
2 Basi Eliya akaenda ili ajionyeshe kwa Ahabu. Na njaa ilikuwa nzito katika Samaria.
Esaïe 51.12 Proverbes 28.1 2 Rois 6.25 Jérémie 14.2-14.6 Jérémie 14.18
3 Ahabu akamwita Obadia, aliyekuwa juu ya nyumba yake; (na huyu Obadia alikuwa mwenye kumcha Bwana sana;
Néhémie 7.2 1 Rois 16.9 Genèse 24.2 2 Rois 4.1 Genèse 41.40
4 kwa kuwa ikawa, Yezebeli alipowaua manabii wa Bwana, Obadia akatwaa manabii mia, akawaficha hamsini hamsini katika pango, akawalisha chakula na kuwapa maji).
1 Rois 18.13 Matthieu 10.40-10.42 Hébreux 11.38 Matthieu 21.35 Apocalypse 17.4-17.6
5 Ahabu akamwambia Obadia, Pita katika nchi, kwenye chemchemi zote za maji, na vijito vyote; labda tutapata majani, tuwahifadhi hai farasi na nyumbu, tusipate hasara ya hao wanyama wote.
Joël 2.22 Psaumes 104.14 Habakuk 3.17 Romains 8.20-8.22 Jérémie 14.5-14.6
6 Basi wakaigawanya nchi, ili wapite katika nchi yote; Ahabu akaenda zake njia moja peke yake, na Obadia akaenda zake njia nyingine peke yake.
Jérémie 14.3
7 Na Obadia alipokuwa njiani, kumbe! Eliya akakutana naye. Akamtambua, akaanguka kifudifudi, akanena, Je! Ni wewe, bwana wangu Eliya?
2 Rois 1.6-1.8 1 Samuel 20.41 Genèse 18.12 2 Samuel 19.18 Genèse 44.16
8 Akamjibu, Ni mimi. Enenda, umwambie bwana wako, Tazama, Eliya yupo.
1 Pierre 2.17-2.18 Romains 13.7 1 Rois 18.3
9 Akamwambia, Nimekosa nini, hata unitie mimi mtumishi wako mkononi mwa Ahabu, aniue?
1 Rois 17.18 Exode 5.21 1 Rois 18.12
10 Kama Bwana, Mungu wako, aishivyo, hakuna taifa wala ufalme ambao bwana wangu hakutuma watu wakutafute; na waliposema, Hayupo, akawaapisha ule ufalme, na taifa, ya kwamba hawakukuona.
1 Rois 17.1 Psaumes 12.7-12.8 1 Rois 17.5 Psaumes 31.20 1 Rois 2.24
11 Nawe sasa wasema, Enenda, umwambie bwana wako, Tazama, Eliya yupo.
1 Rois 18.14 1 Rois 18.8
12 Na itakuwa, mara mimi nikiondoka kwako, roho ya Bwana atakuchukua uende nisikojua; nami nitakapokwenda kumwambia Ahabu, naye asipokuona, ataniua, lakini mimi mtumishi wako namcha Bwana tangu ujana wangu.
2 Rois 2.16 Actes 8.39 Ezéchiel 8.3 2 Rois 2.11 2 Corinthiens 12.2-12.3
13 Je! Bwana wangu hakuambiwa nilivyofanya hapo Yezebeli alipowaua manabii wa Bwana? Jinsi nilivyowaficha manabii wa Bwana, watu mia, hamsini hamsini katika pango, nikawalisha chakula na kuwapa maji?
1 Rois 18.4 Matthieu 25.35 Genèse 20.4-20.5 1 Thessaloniciens 2.9-2.10 Matthieu 10.41-10.42
14 Nawe sasa wasema, Enenda umwambie bwana wako, Tazama, Eliya yupo; basi, ataniua.
Matthieu 10.28
15 Eliya akasema, Kama Bwana wa majeshi aishivyo ambaye ninasimama mbele zake, hakika nitajionyesha kwake leo.
1 Rois 17.1 1 Rois 18.10 Psaumes 103.21 Luc 2.13-2.14 Psaumes 148.2-148.3
16 Basi, Obadia akaenda zake amwone Ahabu, akamwambia; naye Ahabu akaenda kumlaki Eliya.
17 Ikawa, Ahabu alipomwona Eliya, Ahabu akamwambia, Je! Ni wewe, Ewe mtaabishaji wa Israeli?
1 Rois 21.20 Josué 7.25 Actes 16.20 Actes 17.6 Jérémie 38.4
18 Naye akajibu, Si mimi niliyewataabisha Israeli; bali ni wewe, na nyumba ya baba yako, kwa kuwa mmeziacha amri za Bwana; nawe umewafuata mabaali.
2 Chroniques 15.2 1 Rois 9.9 1 Rois 16.31 Actes 24.13 Actes 24.20
19 Basi sasa upeleke watu, unikusanyie jamii ya Israeli katika mlima wa Karmeli, na wale manabii wa Baali mia nne na hamsini, na wale manabii wa Ashera mia nne, walao chakula mezani pa Yezebeli.
Josué 19.26 1 Rois 16.33 2 Rois 2.25 Apocalypse 2.20 1 Rois 15.13
20 Basi, Ahabu akapeleka watu kwa wana wa Israeli wote, akawakusanya manabii pamoja katika mlima wa Karmeli.
1 Rois 22.9
21 Naye Eliya akawakaribia watu wote, akanena, Mtasita-sita katikati ya mawazo mawili hata lini? Bwana akiwa ndiye Mungu, mfuateni; bali ikiwa Baali ni Mungu, haya! Mfuateni yeye. Wale watu hawakumjibu neno.
Josué 24.15 Matthieu 6.24 2 Corinthiens 6.14-6.16 1 Samuel 7.3 2 Rois 17.41
22 Ndipo Eliya akawaambia watu, Mimi nimesalia, mimi peke yangu, nabii wa Bwana; lakini manabii wa Baali ni watu mia nne na hamsini.
1 Rois 19.10 1 Rois 19.14 1 Rois 18.19-18.20 1 Rois 20.38 1 Rois 22.6-22.8
23 Kwa hiyo na watutolee ng’ombe wawili; wao na wajichagulie ng’ombe mmoja, wamkate-kate na kumweka juu ya kuni, wasitie moto chini; nami nitamtengeza huyo ng’ombe wa pili, na kumweka juu ya kuni, wala sitatia moto chini.
24 Nanyi ombeni kwa jina la mungu wenu, nami nitaomba kwa jina la Bwana; na Mungu yule ajibuye kwa moto, na awe ndiye Mungu. Watu wote wakajibu wakasema, Maneno haya ni mazuri.
1 Rois 18.38 1 Chroniques 21.26 2 Samuel 14.19 2 Chroniques 7.3 Lévitique 9.24
25 Eliya akawaambia manabii wa Baali, Jichagulieni ng’ombe mmoja, mkamtengeze kwanza; maana ninyi ndio wengi; mkaliitie jina la mungu wenu, wala msitie moto chini.
26 Wakamtwaa yule ng’ombe waliyepewa, wakamtengeza, wakaliitia jina la Baali tangu asubuhi hata adhuhuri, wakisema, Ee Baali, utusikie. Lakini hapakuwa na sauti, wala aliyejibu. Nao wakaruka-ruka juu ya madhabahu waliyoifanya.
Jérémie 10.5 1 Corinthiens 12.2 1 Corinthiens 8.4 Esaïe 44.17 Sophonie 1.9
27 Ikawa, wakati wa adhuhuri, Eliya akawafanyia dhihaka, akasema, Mwiteni kwa sauti kuu; maana ni mungu huyo; labda anazungumza, au ana shughuli, au anasafiri, au labda amelala, sharti aamshwe.
Psaumes 44.23 Esaïe 41.23 Psaumes 121.4 Psaumes 78.65-78.66 Ecclésiaste 11.9
28 Wakapiga kelele, wakajikata-kata kwa visu na vyembe kama ilivyo desturi yao, hata damu ikawachuruzika.
Lévitique 19.28 Deutéronome 14.1 Marc 5.5 Marc 9.22 Michée 6.7
29 Ikawa, wakati wa adhuhuri ulipopita, walitabiri hata wakati wa kutoa dhabihu ya jioni; lakini hapakuwa na sauti, wala aliyejibu, wala aliyeangalia.
1 Rois 18.26 Exode 29.41 1 Corinthiens 11.4-11.5 2 Timothée 3.8-3.9 Galates 4.8
30 Kisha Eliya akawaambia watu wote, Nikaribieni mimi. Watu wote wakamkaribia. Akaitengeneza madhabahu ya Bwana iliyovunjika.
2 Chroniques 33.16 1 Rois 19.10 1 Rois 19.14 Romains 11.3
31 Eliya akatwaa mawe kumi na mawili, kwa hesabu ya kabila za wana wa Yakobo, aliyejiliwa na neno la Bwana na kuambiwa, Jina lako litakuwa Israeli.
2 Rois 17.34 Genèse 32.28 Genèse 35.10 Josué 4.3-4.4 Josué 4.20
32 Naye akaijenga madhabahu kwa mawe hayo katika jina la Bwana; akafanya mfereji, kama wa vipimo viwili vya mbegu, ukiizunguka madhabahu.
Colossiens 3.17 1 Samuel 7.17 Juges 6.26 Exode 20.24-20.25 1 Corinthiens 10.31
33 Kisha akazipanga zile kuni, akamkata yule ng’ombe vipande vipande, akaviweka juu ya kuni. Akasema, Jazeni mapipa manne maji, mkayamwage juu ya sadaka ya kuteketezwa, na juu ya kuni.
Genèse 22.9 Lévitique 1.6-1.8 Juges 6.20 Jean 11.39-11.40 Daniel 3.25
34 Akasema, Fanyeni mara ya pili. Wakafanya mara ya pili. Akasema, Fanyeni mara ya tatu. Wakafanya mara ya tatu.
2 Corinthiens 4.2 2 Corinthiens 8.21
35 Yale maji yakaizunguka madhabahu; akaujaza mfereji maji.
1 Rois 18.32 1 Rois 18.38
36 Ikawa, wakati wa kutoa dhabihu ya jioni, Eliya nabii akakaribia, akasema, Ee Bwana, Mungu wa Ibrahimu, na wa Isaka, na wa Israeli, na ijulikane leo ya kuwa wewe ndiwe Mungu katika Israeli, na ya kuwa mimi ni mtumishi wako, na ya kuwa nimefanya mambo haya yote kwa neno lako.
Exode 3.6 1 Rois 18.29 1 Rois 8.43 Nombres 16.28-16.30 2 Rois 19.19
37 Unisikie, Ee Bwana, unisikie, ili watu hawa wajue ya kuwa wewe, Bwana, ndiwe Mungu, na ya kuwa wewe umewageuza moyo wakurudie.
Malachie 4.5-4.6 Luc 11.8 Genèse 32.28 Genèse 32.26 Esaïe 37.17-37.20
38 Ndipo moto wa Bwana ukashuka, ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa, na kuni, na mawe, na mavumbi, ukayaramba yale maji yaliyokuwamo katika mfereji.
Lévitique 9.24 Job 1.16 2 Chroniques 7.1 Juges 6.21 1 Chroniques 21.26
39 Na watu wote walipoona, wakaanguka kifudifudi; wakasema, Bwana ndiye Mungu, Bwana ndiye Mungu.
1 Rois 18.24 1 Rois 18.21 Actes 4.16 1 Chroniques 21.16 Actes 2.37
40 Eliya akawaambia, Wakamateni hao manabii wa Baali, asiokoke hata mmoja. Wakawakamata; na Eliya akawachukua mpaka kijito cha Kishoni, akawaua huko.
Deutéronome 13.5 Deutéronome 18.20 Juges 5.21 Juges 4.7 Zacharie 13.2-13.3
41 Naye Eliya akamwambia Ahabu, Haya! Inuka, ule, unywe; kwani pana sauti ya mvua tele.
1 Rois 17.1 1 Rois 18.1 Actes 27.34 Ecclésiaste 9.7
42 Basi Ahabu akainuka ili ale na kunywa. Naye Eliya akapanda juu mpaka kilele cha Karmeli; akasujudu kifudifudi, akainama uso mpaka magotini.
Josué 7.6 Esaïe 6.2 Actes 10.9 Genèse 24.52 Daniel 9.7
43 Akamwambia mtumishi wake, Kwea sasa, utazame upande wa bahari. Akakwea, akatazama, na kusema, Hakuna kitu. Naye akanena, Enenda tena mara saba.
Habakuk 2.3 Luc 18.7 Psaumes 5.3 Luc 18.1 Ephésiens 6.18
44 Ikawa mara ya saba akasema, Tazama, wingu linatoka katika bahari, nalo ni dogo kama mkono wa mtu. Akanena, Enenda, umwambie Ahabu, Tandika, ushuke, mvua isikuzuie.
Luc 12.54 Michée 1.13 Job 8.7 Zacharie 4.10 1 Samuel 6.10
45 Ikawa, muda si muda, mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, ikanyesha mvua nyingi. Ahabu akapanda garini, akaenda zake Yezreeli.
Josué 17.16 1 Rois 21.23 1 Rois 21.1 Nombres 25.8 2 Samuel 21.14
46 Mkono wa Bwana ulikuwa juu ya Eliya; akajikaza viuno, akapiga mbio mbele ya Ahabu mpaka kuiingia Yezreeli.
2 Rois 4.29 2 Rois 3.15 2 Rois 9.1 Ezéchiel 3.14 Jérémie 1.17

Cette Bible est dans le domaine public.