Guerres et victoires de David
 1 Ikawa baadaye, Daudi akawapiga Wafilisti, akawashinda; Daudi akautwaa Gathi na vijiji vyake mikononi mwa hao Wafilisti.
1 Chroniques 18.1-18.17  2 Samuel 2.24  2 Samuel 21.15-21.22  2 Samuel 7.9  
 2 Akapiga Moabu, akawapima kwa kamba hali wamelazwa chini; akapima kamba mbili za kuuawa, na kamba moja nzima ya kuhifadhi hai. Wamoabi wakawa watumwa wa Daudi, wakaleta zawadi.
Nombres 24.17  2 Samuel 8.6  1 Samuel 10.27  Psaumes 60.8  1 Samuel 14.47  
 3 Tena Daudi akampiga Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, alipokwenda kujipatia tena mamlaka yake huko Mtoni.
1 Samuel 14.47  2 Samuel 10.19  2 Samuel 10.16  2 Samuel 10.6  1 Chroniques 18.3  
 4 Daudi akampokonya wapanda farasi elfu na mia saba na askari waliokwenda kwa miguu ishirini elfu; Daudi akawakata mshipa farasi wote wa magari, ila farasi wa magari mia akawasaza.
Josué 11.6  Josué 11.9  1 Rois 10.26  1 Chroniques 18.4  Psaumes 20.7  
 5 Na Washami wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadezeri, mfalme wa Soba, Daudi akawapiga wa Washami watu ishirini na mbili elfu.
1 Rois 11.23-11.25  Esaïe 8.9-8.10  1 Chroniques 18.5-18.6  Job 9.13  2 Samuel 8.3  
 6 Daudi akaweka ngome katika Shamu ya Dameski, na hao Washami wakawa watumwa wa Daudi, wakaleta zawadi. Naye Bwana akampa Daudi kushinda kila alikokwenda.2 Samuel 8.14  2 Samuel 7.9  1 Samuel 14.6  1 Samuel 14.1  Psaumes 5.11-5.12  
 7 Tena Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizovaliwa na watumwa wa Hadadezeri, akazileta Yerusalemu.
1 Rois 10.16-10.17  1 Chroniques 18.7  2 Chroniques 9.15-9.16  1 Rois 14.26-14.27  
 8 Tena toka Tebhathi na toka Berothai, miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi mno.
1 Chroniques 18.8  1 Chroniques 22.14  1 Chroniques 29.7  Ezéchiel 47.16  2 Chroniques 4.1-4.18  
 9 Na Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia ya kwamba Daudi amewapiga jeshi lote la Hadadezeri,
1 Rois 8.65  2 Chroniques 8.4  1 Chroniques 18.9  Amos 6.2  
 10 Tou akamtuma kwa Daudi Hadoramu mwanawe kusalimia, na kumbarikia, kwa sababu amepigana na Hadadezeri, na kumpiga; kwa maana Hadadezeri alikuwa amepigana vita juu ya Tou. Na mkononi mwake akaleta vyombo vya fedha, na vyombo vya dhahabu, na vyombo vya shaba;
1 Rois 1.47  Genèse 43.27  Esaïe 39.1  Psaumes 129.8  1 Chroniques 18.10  
 11 hivi pia mfalme Daudi akavifanya wakfu kwa Bwana, pamoja na hiyo fedha, na dhahabu alizofanya wakfu za mataifa yote aliowashinda;
1 Rois 7.51  1 Chroniques 18.11  1 Chroniques 22.14-22.16  Michée 4.13  1 Chroniques 29.2  
 12 za Edomu, na za Moabu, na za wana wa Amoni, na za Wafilisti, na za Amaleki, na za nyara za Hadadezeri, mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
2 Samuel 10.14  2 Samuel 8.2  1 Chroniques 18.11  1 Samuel 30.20  2 Samuel 10.11  
 13 Basi Daudi akajipatia jina, aliporudi kutoka kuwapiga Waedomi katika Bonde la Chumvi, watu kumi na nane elfu.
2 Rois 14.7  2 Samuel 7.9  1 Chroniques 18.12  2 Chroniques 25.11  Psaumes 60.1  
 14 Akaweka askari wenye kulinda ngome katika Edomu; katikati ya Edomu yote akaweka ngome, na Waedomi wote wakawa watumwa wa Daudi. Naye Bwana akampa Daudi kushinda kila alikokwenda.
Genèse 27.29  Genèse 25.23  2 Samuel 8.6  Genèse 27.37-27.40  1 Chroniques 18.13  
 15 Daudi akatawala juu ya Israeli wote; naye Daudi akawafanyia hukumu na haki watu wake wote.
Amos 5.15  1 Chroniques 18.14  Psaumes 101.1-101.8  2 Samuel 5.5  Jérémie 23.5-23.6  
 16 Huyo Yoabu, mwana wa Seruya alikuwa juu ya jeshi; na Yehoshafati, mwana wa Ahiludi, mwenye kuandika tarehe;
1 Rois 4.3  1 Chroniques 11.6  2 Samuel 19.13  2 Samuel 20.23-20.24  1 Chroniques 18.15-18.17  
 17 na Sadoki, mwana wa Ahitubu, na Ahimeleki, mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; na Shausha mwandishi;
1 Chroniques 18.16  1 Chroniques 6.8  1 Chroniques 24.3-24.4  1 Chroniques 16.39  1 Chroniques 6.53  
 18 na Benaya, mwana wa Yehoyada, alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi wakawa makuhani.
1 Samuel 30.14  2 Samuel 20.23  2 Samuel 20.7  2 Samuel 15.18  1 Chroniques 18.17