Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 8.3
Bible en Swahili de l’est


Guerres et victoires de David

1 Ikawa baadaye, Daudi akawapiga Wafilisti, akawashinda; Daudi akautwaa Gathi na vijiji vyake mikononi mwa hao Wafilisti.
1 Chroniques 18.1-18.17 2 Samuel 2.24 2 Samuel 21.15-21.22 2 Samuel 7.9
2 Akapiga Moabu, akawapima kwa kamba hali wamelazwa chini; akapima kamba mbili za kuuawa, na kamba moja nzima ya kuhifadhi hai. Wamoabi wakawa watumwa wa Daudi, wakaleta zawadi.
Nombres 24.17 2 Samuel 8.6 1 Samuel 10.27 Psaumes 60.8 1 Samuel 14.47
3 Tena Daudi akampiga Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, alipokwenda kujipatia tena mamlaka yake huko Mtoni.
1 Samuel 14.47 2 Samuel 10.19 2 Samuel 10.16 2 Samuel 10.6 1 Chroniques 18.3
4 Daudi akampokonya wapanda farasi elfu na mia saba na askari waliokwenda kwa miguu ishirini elfu; Daudi akawakata mshipa farasi wote wa magari, ila farasi wa magari mia akawasaza.
Josué 11.6 Josué 11.9 1 Rois 10.26 1 Chroniques 18.4 Psaumes 20.7
5 Na Washami wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadezeri, mfalme wa Soba, Daudi akawapiga wa Washami watu ishirini na mbili elfu.
1 Rois 11.23-11.25 Esaïe 8.9-8.10 1 Chroniques 18.5-18.6 Job 9.13 2 Samuel 8.3
6 Daudi akaweka ngome katika Shamu ya Dameski, na hao Washami wakawa watumwa wa Daudi, wakaleta zawadi. Naye Bwana akampa Daudi kushinda kila alikokwenda.
2 Samuel 8.14 2 Samuel 7.9 1 Samuel 14.6 1 Samuel 14.1 Psaumes 5.11-5.12
7 Tena Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizovaliwa na watumwa wa Hadadezeri, akazileta Yerusalemu.
1 Rois 10.16-10.17 1 Chroniques 18.7 2 Chroniques 9.15-9.16 1 Rois 14.26-14.27
8 Tena toka Tebhathi na toka Berothai, miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi mno.
1 Chroniques 18.8 1 Chroniques 22.14 1 Chroniques 29.7 Ezéchiel 47.16 2 Chroniques 4.1-4.18
9 Na Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia ya kwamba Daudi amewapiga jeshi lote la Hadadezeri,
1 Rois 8.65 2 Chroniques 8.4 1 Chroniques 18.9 Amos 6.2
10 Tou akamtuma kwa Daudi Hadoramu mwanawe kusalimia, na kumbarikia, kwa sababu amepigana na Hadadezeri, na kumpiga; kwa maana Hadadezeri alikuwa amepigana vita juu ya Tou. Na mkononi mwake akaleta vyombo vya fedha, na vyombo vya dhahabu, na vyombo vya shaba;
1 Rois 1.47 Genèse 43.27 Esaïe 39.1 Psaumes 129.8 1 Chroniques 18.10
11 hivi pia mfalme Daudi akavifanya wakfu kwa Bwana, pamoja na hiyo fedha, na dhahabu alizofanya wakfu za mataifa yote aliowashinda;
1 Rois 7.51 1 Chroniques 18.11 1 Chroniques 22.14-22.16 Michée 4.13 1 Chroniques 29.2
12 za Edomu, na za Moabu, na za wana wa Amoni, na za Wafilisti, na za Amaleki, na za nyara za Hadadezeri, mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
2 Samuel 10.14 2 Samuel 8.2 1 Chroniques 18.11 1 Samuel 30.20 2 Samuel 10.11
13 Basi Daudi akajipatia jina, aliporudi kutoka kuwapiga Waedomi katika Bonde la Chumvi, watu kumi na nane elfu.
2 Rois 14.7 2 Samuel 7.9 1 Chroniques 18.12 2 Chroniques 25.11 Psaumes 60.1
14 Akaweka askari wenye kulinda ngome katika Edomu; katikati ya Edomu yote akaweka ngome, na Waedomi wote wakawa watumwa wa Daudi. Naye Bwana akampa Daudi kushinda kila alikokwenda.
Genèse 27.29 Genèse 25.23 2 Samuel 8.6 Genèse 27.37-27.40 1 Chroniques 18.13
15 Daudi akatawala juu ya Israeli wote; naye Daudi akawafanyia hukumu na haki watu wake wote.
Amos 5.15 1 Chroniques 18.14 Psaumes 101.1-101.8 2 Samuel 5.5 Jérémie 23.5-23.6
16 Huyo Yoabu, mwana wa Seruya alikuwa juu ya jeshi; na Yehoshafati, mwana wa Ahiludi, mwenye kuandika tarehe;
1 Rois 4.3 1 Chroniques 11.6 2 Samuel 19.13 2 Samuel 20.23-20.24 1 Chroniques 18.15-18.17
17 na Sadoki, mwana wa Ahitubu, na Ahimeleki, mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; na Shausha mwandishi;
1 Chroniques 18.16 1 Chroniques 6.8 1 Chroniques 24.3-24.4 1 Chroniques 16.39 1 Chroniques 6.53
18 na Benaya, mwana wa Yehoyada, alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi wakawa makuhani.
1 Samuel 30.14 2 Samuel 20.23 2 Samuel 20.7 2 Samuel 15.18 1 Chroniques 18.17

Cette Bible est dans le domaine public.