Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 14.24
Bible en Swahili de l’est


Retour d’Absalom

1 Basi Yoabu, mwana wa Seruya, akatambua ya kuwa moyo wa mfalme unamwelekea Absalomu.
2 Samuel 13.39 2 Samuel 2.18 1 Chroniques 2.16 Proverbes 29.26 2 Samuel 19.4
2 Yoabu akatuma watu waende Tekoa, akaleta kutoka huko mwanamke mwenye akili, akamwambia, Nakusihi, ujifanye kama unakaa matanga, ukavae nguo za kufiwa, nakusihi, wala usijitie mafuta, ila ukafanane na mwanamke aliyeomboleza siku nyingi kwa ajili yake aliyefariki;
2 Chroniques 11.6 Amos 1.1 Ruth 3.3 Jérémie 6.1 2 Samuel 12.20
3 kisha uingie kwa mfalme ukamwambie maneno haya. Hivyo Yoabu akamtia maneno kinywani.
2 Samuel 14.19 Exode 4.15 Esaïe 59.21 Jérémie 1.9 Deutéronome 18.18
4 Naye yule mwanamke wa Tekoa aliponena na mfalme, akaanguka kifulifuli chini, akamsujudia, akasema, Nisaidie, Ee mfalme.
2 Rois 6.26-6.28 2 Samuel 1.2 1 Samuel 25.23 Job 29.12-29.14 Luc 18.3-18.5
5 Mfalme akamwuliza, Una nini? Naye akajibu, Hakika ni mjane mimi, niliyefiwa na mume wangu.
2 Samuel 12.1-12.3 Juges 9.8-9.15
6 Nami mjakazi wako nalikuwa na wana wawili, na hao wawili wakashindana uwandani, wala hapakuwa na mtu wa kuwaamua, lakini mmoja akampiga mwenzake, akamwua.
Genèse 4.8 Deutéronome 22.26-22.27 Exode 2.13
7 Na tazama, jamaa yote wameniinukia mimi mjakazi wako, wakasema, Mtoe yule aliyempiga nduguye, ili tupate kumwua yeye kwa maisha ya nduguye aliyemwua, hata na kumfisha mrithi pia; ndivyo watakavyolizima kaa langu lililobaki, wasimwachie mume wangu jina wala masalio usoni pa nchi.
Nombres 35.19 Matthieu 21.38 2 Samuel 12.17 Genèse 4.14 Deutéronome 25.6
8 Mfalme akamwambia huyo mwanamke, Nenda nyumbani kwako, nami nitakufanyia agizo.
Proverbes 18.13 Job 29.16 2 Samuel 12.5-12.6 2 Samuel 16.4 Esaïe 11.3-11.4
9 Ndipo huyo mwanamke wa Tekoa akamwambia mfalme, Na uwe juu yangu, Ee bwana wangu mfalme, na juu ya nyumba ya baba yangu uovu huu; wala kwa mfalme na kwa kiti chake cha enzi pasiwepo hatia.
1 Samuel 25.24 1 Rois 2.33 Matthieu 27.25 2 Samuel 3.28-3.29 Nombres 35.33
10 Mfalme akasema, Ye yote atakaye kuambia neno, mlete kwangu, naye hatakugusa tena.
11 Ndipo akajibu, Nakusihi, mfalme na amkumbuke Bwana, Mungu wako, ili mlipiza kisasi cha damu asizidi kuharibu, wasije kumharibu mwanangu. Naye akasema, Aishivyo Bwana, hautaanguka chini hata unywele mmoja wa mwanao.
1 Samuel 14.45 Nombres 35.19 Matthieu 10.30 Nombres 35.21 Actes 27.34
12 Mwanamke akasema, Mwache mjakazi wako, nakusihi, niseme neno moja kwa bwana wangu mfalme. Akasema, Haya nena.
1 Samuel 25.24 Jérémie 12.1 Genèse 44.18 Actes 26.1 Genèse 18.27
13 Mwanamke akasema, Kwa nini basi wewe umewafikiria mambo kama hayo watu wa Mungu? Kwani kwa kunena neno hili mfalme ni kama mwenye hatia, kwa kuwa mfalme hamleti kwao tena yule mfukuzwa wake.
2 Samuel 12.7 2 Samuel 13.37-13.38 Juges 20.2 1 Rois 20.40-20.42 2 Samuel 7.8
14 Kwa kuwa hatuna budi kufa, nasi tu kama maji yaliyomwagika chini, yasiyowezekana kuzoleka tena; wala Mungu haondoi maisha ila hufikiri shauri, kwamba yeye aliyefukuzwa asiwe mkimbizi kwake.
Nombres 35.28 Nombres 35.25 Nombres 35.15 Hébreux 9.27 Job 30.23
15 Hata sasa nilivyokuja mimi kunena neno hili na bwana wangu mfalme, ni kwa sababu watu wamenitisha; nami, mjakazi wako, nikasema, Mimi nitanena sasa kwa mfalme; labda itakuwa mfalme atanifanyia haja yangu mimi mtumwa wake.
16 Kwa kuwa mfalme atasikia, ili amwokoe mtumwa wake mkononi mwa yule mtu atakaye kuniharibu mimi na mwanangu pia katika urithi wa Mungu.
1 Samuel 26.19
17 Ndipo mimi mjakazi wako nikasema, Neno la bwana wangu mfalme na liwe la kustarehesha; kwa kuwa kama malaika wa Mungu ndivyo alivyo bwana wangu mfalme, kuyapambanua yaliyo mema na yaliyo mabaya; naye Bwana, Mungu wako na awe pamoja nawe.
2 Samuel 19.27 1 Samuel 29.9 2 Samuel 14.20 1 Rois 3.9 Hébreux 5.14
18 Ndipo mfalme akajibu, akamwambia yule mwanamke, usinifiche, nakusihi, neno lo lote nitakalokuuliza. Na mwanamke akasema, Na anene sasa bwana wangu mfalme.
Jérémie 38.14 Jérémie 38.25 1 Samuel 3.17-3.18
19 Mfalme akasema, Je! Si mkono wa Yoabu ulio pamoja nawe katika haya yote? Mwanamke akajibu, akasema, Kama iishivyo roho yako, bwana wangu, mfalme, hapana mtu awezaye kugeuka kwa kuume, au kwa kushoto, kukana neno lo lote alilolisema bwana wangu mfalme; kwani mtumwa wako Yoabu ndiye aliyeniamuru, na kuyaweka maneno haya yote kinywani mwa mjakazi wako;
2 Samuel 14.3 1 Samuel 1.26 2 Samuel 3.27 Deutéronome 5.32 Exode 4.15
20 mtumwa wako Yoabu ameyatenda haya ili kubadili uso wa jambo hili; na bwana wangu anayo akili, kama akili ya malaika wa Mungu, hata ajue mambo yote ya duniani.
2 Samuel 14.17 2 Samuel 19.27 Job 32.21-32.22 Genèse 3.5 2 Samuel 5.23
21 Basi mfalme akamwambia Yoabu, Angalia sasa, nimekata shauri hili; nenda, ukamrudishe tena yule kijana Absalomu.
2 Samuel 14.11 Marc 6.26 1 Samuel 14.39
22 Naye Yoabu akaanguka kifulifuli hata nchi, akasujudu, akambariki mfalme, Yoabu akasema, Leo mimi mtumwa wako najua ya kwamba nimepata neema machoni pako, bwana wangu mfalme, kwa kuwa mfalme amemfanyia mtumwa wake haja yake.
Genèse 6.8 Néhémie 11.2 Proverbes 31.28 Job 31.20 Exode 33.16-33.17
23 Basi Yoabu akaondoka, akaenda Geshuri, akamleta Absalomu Yerusalemu.
2 Samuel 3.3 2 Samuel 13.37-13.38
24 Naye mfalme akasema, Ageukie nyumbani kwake, asinione uso wangu. Basi Absalomu akarejea nyumbani kwake, asimwone uso mfalme.
Apocalypse 22.4 Genèse 43.3 2 Samuel 14.28 2 Samuel 3.13 Exode 10.28
25 Basi katika Israeli wote hapakuwa na mtu hata mmoja mwenye kusifiwa kwa uzuri wake kama huyo Absalomu; tangu nyayo za miguu yake hata utosi wa kichwa chake hapakuwa na ila kwake.
Job 2.7 Esaïe 1.6 Deutéronome 28.35 Ephésiens 5.27 Proverbes 31.30
26 Naye aliponyoa kichwa, (basi mwisho wa kila mwaka hunyoa; na kwa sababu nywele zilikuwa nzito kwake, kwa hiyo akanyoa;) hupima nywele za kichwa chake shekeli mia mbili kwa uzani wa mfalme.
Ezéchiel 44.20 2 Samuel 18.9 Genèse 23.16 Esaïe 3.24 Ezéchiel 45.9-45.14
27 Kisha wakazaliwa kwake Absalomu wana watatu na binti mmoja, ambaye jina lake aliitwa Tamari; naye alikuwa mwanamke mzuri wa uso.
2 Samuel 18.18 2 Samuel 13.1 Esaïe 14.22 Jérémie 22.30 Job 18.16-18.19
28 Absalomu akakaa miaka miwili mizima katika Yerusalemu; asimwone uso mfalme.
29 Ndipo Absalomu akatuma kumwita Yoabu, ampeleke kwa mfalme, lakini yeye akakataa kumjia; akatuma tena mara ya pili, lakini akakataa kuja.
2 Samuel 14.30-14.31 Esther 1.12 Matthieu 22.3
30 Kwa hiyo akawaambia watumishi wake, Tazameni, shamba la Yoabu liko karibu na shamba langu, naye ana shayiri huko; nendeni mkalitie moto. Basi watumishi wa Absalomu wakalitia moto lile shamba.
Juges 15.4-15.5 2 Rois 9.33 1 Rois 21.9-21.14 2 Samuel 13.28-13.29 2 Rois 10.6-10.7
31 Ndipo akaondoka Yoabu, akamwendea Absalomu nyumbani kwake, akamwambia, Kwa nini watumishi wako wamelitia moto shamba langu?
32 Absalomu akamjibu Yoabu, Angalia, nilituma kwako, kusema, Njoo kwangu, ili nikupeleke kwa mfalme kunena, Mbona nimekuja kutoka Geshuri? Ingekuwa heri kwangu kama ningekuwako huko hata sasa; basi sasa na nimtazame uso mfalme; na ukiwapo uovu kwangu, na aniue.
Proverbes 28.13 1 Samuel 20.8 Matthieu 25.44 Exode 16.3 Romains 3.19
33 Basi Yoabu akamwendea mfalme, akamwambia hayo, naye alipomwita Absalomu, yeye akaja kwa mfalme, akainama kifulifuli hata nchi mbele ya mfalme; naye mfalme akambusu Absalomu.
Luc 15.20 Genèse 33.4 Genèse 27.26 Genèse 45.15

Cette Bible est dans le domaine public.