Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 11.19
Bible en Swahili de l’est


La tour de Babel

1 Nchi yote ilikuwa na lugha moja na usemi mmoja.
Sophonie 3.9 Esaïe 19.18 Actes 2.6
2 Ikawa watu waliposafiri pande za mashariki waliona nchi tambarare katika nchi ya Shinari; wakakaa huko.
Genèse 10.10 Daniel 1.2 Genèse 14.1 Zacharie 5.11 Esaïe 11.11
3 Wakaambiana, Haya, na tufanye matofali tukayachome moto. Walikuwa na matofali badala ya mawe, na lami badala ya chokaa.
Genèse 14.10 Exode 1.14 Exode 2.3 Genèse 11.4 Jacques 5.1
4 Wakasema, Haya, na tujijengee mji, na mnara, na kilele chake kifike mbinguni, tujifanyie jina; ili tusipate kutawanyika usoni pa nchi yote.
Deutéronome 1.28 Deutéronome 9.1 Psaumes 92.9 Daniel 4.30 Jean 5.44
5 Bwana akashuka ili auone mji na mnara waliokuwa wakiujenga wanadamu.
Genèse 18.21 Exode 19.11 Exode 3.8 Jean 3.13 Exode 19.20
6 Bwana akasema, Tazama, watu hawa ni taifa moja, na lugha yao ni moja; na haya ndiyo wanayoanza kuyafanya, wala sasa hawatazuiliwa neno wanalokusudia kulifanya.
Genèse 11.1 Luc 1.51 Genèse 9.19 Ecclésiaste 11.9 Genèse 3.22
7 Haya, na tushuke huko, tuwachafulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa wao.
Genèse 1.26 Genèse 42.23 1 Corinthiens 14.2-14.11 Deutéronome 28.49 Jérémie 5.15
8 Basi Bwana akawatawanya kutoka huko waende usoni pa nchi yote; wakaacha kuujenga ule mji.
Luc 1.51 Genèse 10.32 Genèse 10.25 Genèse 11.9 Genèse 11.4
9 Kwa sababu hiyo jina lake likaitwa Babeli; maana hapo ndipo Bwana alipoichafua lugha ya dunia yote; na kutoka huko Bwana akawatawanya waende usoni pa nchi yote.
Genèse 10.10 Genèse 10.5 Genèse 10.20 Genèse 10.25 1 Corinthiens 14.23

Histoire d’Abraham

Les ancêtres d’Abram

10 Hivi ndivyo vizazi vya Shemu; Shemu alikuwa mtu wa miaka mia akamzaa Arfaksadi miaka miwili baada ya gharika.
1 Chroniques 1.17-1.27 Genèse 10.21-10.22 Luc 3.34-3.36 Genèse 11.27
11 Shemu akaishi baada ya kumzaa Arfaksadi miaka mia tano, akazaa wana, waume na wake.
Genèse 9.7 Psaumes 127.3-127.4 Genèse 5.4-5.32 Psaumes 144.12 Genèse 1.28
12 Arfaksadi akaishi miaka thelathini na mitano, akamzaa Sela.
Luc 3.36
13 Arfaksadi akaishi baada ya kumzaa Sela miaka mia nne na mitatu, akazaa wana, waume na wake.
14 Sela akaishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
15 Sela akaishi baada ya kumzaa Eberi miaka mia nne na mitatu, akazaa wana, waume na wake.
16 Eberi akaishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
Genèse 10.25 Genèse 10.21 1 Chroniques 1.19 Nombres 24.24 Luc 3.35
17 Eberi akaishi baada ya kumzaa Pelegi miaka mia nne na thelathini, akazaa wana, waume na wake.
18 Pelegi akaishi miaka thelathini, akamzaa Reu.
Luc 3.35
19 Pelegi akaishi baada ya kumzaa Reu miaka mia mbili na kenda, akazaa wana, waume na wake.
20 Reu akaishi miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi.
Luc 3.35
21 Reu akaishi baada ya kumzaa Serugi miaka mia mbili na saba, akazaa wana, waume na wake.
22 Serugi akaishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
Josué 24.2
23 Serugi akaishi baada ya kumzaa Nahori miaka mia mbili, akazaa wana, waume na wake.
24 Nahori akaishi miaka ishirini na kenda, akamzaa Tera.
Luc 3.34 Josué 24.2
25 Nahori akaishi baada ya kumzaa Tera miaka mia na kumi na kenda, akazaa wana, waume na wake.
26 Tera akaishi miaka sabini, akamzaa Abramu, na Nahori, na Harani.
Josué 24.2 Genèse 29.4-29.5 1 Chroniques 1.26-1.27 Genèse 22.20-22.24 Genèse 12.4-12.5
27 Na hivi ndivyo vizazi vya Tera. Tera akamzaa Abramu, na Nahori, na Harani. Harani akamzaa Lutu.
Genèse 14.12 Genèse 12.4 Genèse 11.31 2 Pierre 2.7 Genèse 13.1-13.11
28 Harani akafa kabla ya baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, yaani, katika Uru wa Wakaldayo.
Genèse 15.7 Actes 7.2-7.4 Néhémie 9.7 Genèse 11.31
29 Abramu na Nahori wakajitwalia wake. Jina la mkewe Abramu aliitwa Sarai, na jina la mkewe Nahori aliitwa Milka, binti Harani, ambaye alikuwa baba wa Milka na wa Iska.
Genèse 22.20 Genèse 17.15 Genèse 24.15 Genèse 20.12
30 Na Sarai alikuwa tasa, hakuwa na mtoto.
Luc 1.36 Juges 13.2 Genèse 16.1-16.2 Genèse 25.21 1 Samuel 1.2
31 Tera akamtwaa Abramu mwanawe, na Lutu mwana wa Harani, mwana wa mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka wote katika Uru wa Wakaldayo, waende nchi ya Kanaani, wakafika mpaka Harani wakakaa huko.
Néhémie 9.7 Actes 7.2-7.4 Genèse 12.4 Genèse 15.7 Genèse 24.10
32 Siku za Tera zilikuwa miaka mia mbili na mitano; Tera akafa katika Harani.

Cette Bible est dans le domaine public.