Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 83.12

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 83

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 82 Chapitre 84

Prière contre les ennemis d’Israël

1 Ee Mungu, usistarehe, Ee Mungu, usinyamae, wala usitulie.
2 Maana adui zako wanafanya ghasia, Nao wakuchukiao wameviinua vichwa vyao.
3 Juu ya watu wako wanafanya hila, Na kushauriana juu yao uliowaficha.
4 Wamesema, Njoni, tuwakatilie mbali wasiwe taifa, Na jina la Israeli halitakumbukwa tena.
5 Maana wanashauriana kwa moyo mmoja, Juu yako wanafanyana agano.
6 Hema za Edomu, na Waishmaeli, Na Moabu, na Wahagari,
7 Gebali, na Amoni, na Amaleki, Na Filisti, nao wanaokaa Tiro,
8 Ashuri naye amepatana nao, Wamewasaidia wana wa Lutu.
9 Uwatende kama Midiani, kama Sisera, Kama Yabini, penye kijito Kishoni.
10 Ambao waliangamizwa Endori; Wakawa samadi juu ya nchi.
11 Uwafanye wakuu wao kama Orebu na Zeebu, Na masheki yao wote kama Zeba na Zalmuna.
12 Ambao Walisema, Na tutamalaki makao ya Mungu.
13 Ee Mungu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, Mithili ya makapi mbele ya upepo,
14 Kama moto uteketezao msitu, Kama miali ya moto iiwashayo milima,
15 Ndivyo utakavyowafuatia kwa tufani yako, Na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
16 Uwajaze nyuso zao fedheha; Wakalitafute jina lako, Bwana.
17 Waaibike, wafadhaike milele, Naam, watahayarike na kupotea.
18 Wajue ya kuwa Wewe, uitwaye jina lako YEHOVA, Ndiwe peke yako Uliye juu, juu ya nchi yote.

Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 83.12 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.