Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 81.5

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 81

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 80 Chapitre 82

Invitation à écouter le Seigneur

1 Mwimbieni Mungu, nguvu zetu, nyimbo za furaha, Mshangilieni Mungu wa Yakobo.
2 Pazeni zaburi, pigeni matari, Kinubi chenye sauti nzuri, na kinanda.
3 Pigeni panda mwandamo wa mwezi, Wakati wa mbalamwezi, sikukuu yetu.
4 Kwa maana ni sheria kwa Israeli, Ni hukumu ya Mungu wa Yakobo.
5 Aliamuru iwe ushuhuda katika Yusufu, Alipoondoka juu ya nchi ya Misri; Maneno yake nisiyemjua naliyasikia.
6 Nimelitenga bega lake na mzigo, Mikono yake ikaachana na kikapu.
7 Katika shida uliniita nikakuokoa; Nalikuitikia katika sitara ya radi; Nalikujaribu penye maji ya Meriba.
8 Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya, Ee Israeli, kama ukitaka kunisikiliza;
9 Usiwe na mungu mgeni ndani yako; Wala usimsujudie mungu mwingine.
10 Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, Niliyekupandisha toka nchi ya Misri; Fumbua sana kinywa chako nami nitakijaza.
11 Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu, Wala Israeli hawakunitaka.
12 Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao, Waenende katika mashauri yao.
13 Laiti watu wangu wangenisikiliza, Na Israeli angeenenda katika njia zangu;
14 Ningewadhili adui zao kwa upesi, Na juu ya watesi wao ningegeuza mkono wangu;
15 Wamchukiao Bwana wangenyenyekea mbele zake, Bali wakati wao ungedumu milele.
16 Naam, ningewalisha kwa unono wa ngano, Ningewashibisha kwa asali itokayo mwambani.

Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 81.5 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.