Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 29.5

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 29

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 28 Chapitre 30

La toute-puissance de Dieu

1 Mpeni Bwana, enyi wana wa Mungu, Mpeni Bwana utukufu na nguvu; 2 Mpeni Bwana utukufu wa jina lake; Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu. 3 Sauti ya Bwana i juu ya maji; Mungu wa utukufu alipiga radi; Bwana yu juu ya maji mengi. 4 Sauti ya Bwana ina nguvu; Sauti ya Bwana ina adhama; 5 Sauti ya Bwana yaivunja mierezi; Naam, Bwana aivunja-vunja mierezi ya Lebanoni; 6 Airusha-rusha kama ndama wa ng’ombe; Lebanoni na Sirioni kama mwana-nyati. 7 Sauti ya Bwana yaipasua miali ya moto; 8 Sauti ya Bwana yalitetemesha jangwa; Bwana alitetemesha jangwa la Kadeshi. 9 Sauti ya Bwana yawazalisha ayala, Na kuifichua misitu; Na ndani ya hekalu lake Wanasema wote, Utukufu. 10 Bwana aliketi juu ya Gharika; Naam, Bwana ameketi hali ya mfalme milele. 11 Bwana atawapa watu wake nguvu; Bwana atawabariki watu wake kwa amani.

Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 29.5 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.