Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 29.11

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 29

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 28 Chapitre 30

La toute-puissance de Dieu

1 Mpeni Bwana, enyi wana wa Mungu, Mpeni Bwana utukufu na nguvu;
2 Mpeni Bwana utukufu wa jina lake; Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu.
3 Sauti ya Bwana i juu ya maji; Mungu wa utukufu alipiga radi; Bwana yu juu ya maji mengi.
4 Sauti ya Bwana ina nguvu; Sauti ya Bwana ina adhama;
5 Sauti ya Bwana yaivunja mierezi; Naam, Bwana aivunja-vunja mierezi ya Lebanoni;
6 Airusha-rusha kama ndama wa ng’ombe; Lebanoni na Sirioni kama mwana-nyati.
7 Sauti ya Bwana yaipasua miali ya moto;
8 Sauti ya Bwana yalitetemesha jangwa; Bwana alitetemesha jangwa la Kadeshi.
9 Sauti ya Bwana yawazalisha ayala, Na kuifichua misitu; Na ndani ya hekalu lake Wanasema wote, Utukufu.
10 Bwana aliketi juu ya Gharika; Naam, Bwana ameketi hali ya mfalme milele.
11 Bwana atawapa watu wake nguvu; Bwana atawabariki watu wake kwa amani.

Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 29.11 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.