Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Apocalypse 4.2
Bible en Swahili de l’est


Sept sceaux

Le trône de Dieu

1 Baada ya hayo naliona, na tazama, mlango ukafunguka mbinguni, na sauti ile ya kwanza niliyoisikia kama sauti ya baragumu ikinena nami, ikisema, Panda hata huku, nami nitakuonyesha mambo ambayo hayana budi kuwako baada ya hayo.
Apocalypse 1.10 Apocalypse 11.12 Apocalypse 22.6 Apocalypse 1.19 Apocalypse 16.17
2 Na mara nalikuwa katika Roho; na tazama, kiti cha enzi kimewekwa mbinguni na mmoja ameketi juu ya kile kiti;
Daniel 7.9 Esaïe 6.1 1 Rois 22.19 Apocalypse 1.10 Apocalypse 4.9
3 na yeye aliyeketi alionekana mithili ya jiwe la yaspi na akiki, na upinde wa mvua ulikizunguka kile kiti cha enzi, ukionekana mithili ya zumaridi.
Ezéchiel 1.28 Apocalypse 21.11 Apocalypse 10.1 Ezéchiel 28.13 Genèse 9.13-9.16
4 Na viti ishirini na vinne vilikizunguka kile kiti cha enzi, na juu ya vile viti naliona wazee ishirini na wanne, wameketi, wamevikwa mavazi meupe; na juu ya vichwa vyao walikuwa na taji za dhahabu.
Apocalypse 11.16 Matthieu 19.28 Apocalypse 4.10 Apocalypse 20.4 Luc 22.30
5 Na katika kile kiti cha enzi kunatoka umeme na sauti na ngurumo. Na taa saba za moto zilikiwaka mbele ya kile kiti cha enzi, ndizo Roho saba za Mungu.
Apocalypse 1.4 Exode 19.16 Apocalypse 8.5 Zacharie 4.2 Apocalypse 11.19
6 Na mbele ya kile kiti cha enzi kulikuwa na mfano wa bahari ya kioo, kama bilauri; na katikati ya kile kiti cha enzi, na pande zote za kile kiti, walikuwako wenye uhai wanne, wamejaa macho mbele na nyuma.
Apocalypse 15.2 Apocalypse 5.6 Ezéchiel 10.12 Apocalypse 19.4 Apocalypse 5.14-6.1
7 Na huyo mwenye uhai wa kwanza alikuwa mfano wa simba; na mwenye uhai wa pili alikuwa mfano wa ndama; na mwenye uhai wa tatu alikuwa na uso kama uso wa mwanadamu; na mwenye uhai wa nne alikuwa mfano wa tai arukaye.
Ezéchiel 1.10 Ezéchiel 10.14 Ezéchiel 1.8 Nombres 23.24 Nombres 24.9
8 Na hawa wenye uhai wanne, kila mmoja alikuwa na mabawa sita; na pande zote na ndani wamejaa macho, wala hawapumziki mchana wala usiku, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, Bwana Mungu Mwenyezi, aliyekuwako na aliyeko na atakayekuja.
Esaïe 6.2-6.13 Apocalypse 4.6 Ezéchiel 10.21-10.22 Apocalypse 1.8 Apocalypse 1.4
9 Na hao wenye uhai wanapompa yeye aketiye juu ya kiti cha enzi utukufu, na heshima, na shukrani, yeye aliye hai hata milele na milele,
Apocalypse 15.7 Apocalypse 5.13-5.14 Apocalypse 7.11-7.12 Apocalypse 10.6 Psaumes 48.14
10 ndipo hao wazee ishirini na wanne huanguka mbele zake yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi, nao humsujudia yeye aliye hai hata milele na milele, nao huzitupa taji zao mbele ya kile kiti cha enzi, wakisema,
Apocalypse 4.4 Apocalypse 5.14 Apocalypse 5.8 Apocalypse 19.4 Apocalypse 7.11
11 Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa.
Colossiens 1.16-1.17 Apocalypse 5.12 Genèse 1.1 Esaïe 40.28 Apocalypse 10.6

Cette Bible est dans le domaine public.