Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Apocalypse 12.14
Bible en Swahili de l’est


Sept signes

La femme, le dragon et l’enfant

1 Na ishara kuu ilionekana mbinguni; mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota kumi na mbili.
Apocalypse 11.19 Apocalypse 12.3 Luc 21.11 Esaïe 60.1-60.4 Actes 2.19
2 Naye alikuwa ana mimba, akilia, hali ana utungu na kuumwa katika kuzaa.
Apocalypse 12.4 Galates 4.19 Esaïe 66.7-66.9 Jean 16.21 Esaïe 53.11
3 Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama, joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake vilemba saba.
Apocalypse 17.12 Apocalypse 12.9 Apocalypse 20.2 Apocalypse 12.1 Daniel 7.20
4 Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi. Na yule joka akasimama mbele ya yule mwanamke aliye tayari kuzaa, ili azaapo, amle mtoto wake.
Jean 8.44 Apocalypse 8.7 Apocalypse 12.9 Apocalypse 17.18 Apocalypse 9.10
5 Naye akazaa mtoto mwanamume, yeye atakayewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Na mtoto wake akanyakuliwa hata kwa Mungu, na kwa kiti chake cha enzi.
Apocalypse 2.26-2.27 Apocalypse 19.15 Apocalypse 12.2 Psaumes 2.9-2.10 Michée 5.3
6 Yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambapo ana mahali palipotengenezwa na Mungu, ili wamlishe huko muda wa siku elfu na mia mbili na sitini.
Apocalypse 11.2-11.3 1 Rois 17.3-17.6 Apocalypse 12.14 Apocalypse 12.4 Apocalypse 13.5
7 Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;
Jude 1.9 Daniel 12.1 Daniel 10.21 2 Pierre 2.4 Daniel 10.13
8 nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni.
Romains 8.31-8.39 Job 7.10 Jérémie 1.19 Job 27.21-27.23 Jude 1.6
9 Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.
Jean 12.31 Luc 10.18 2 Corinthiens 4.4 Jean 8.44 Apocalypse 20.8
10 Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.
Apocalypse 11.15 Luc 22.31 1 Chroniques 29.11 Job 2.5 Job 1.9
11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.
Luc 14.26 2 Corinthiens 10.3-10.5 Jean 16.33 Hébreux 2.14-2.15 Romains 16.20
12 Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.
Apocalypse 10.6 Apocalypse 18.20 Apocalypse 8.13 Esaïe 49.13 Apocalypse 11.14
13 Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.
Genèse 3.15 Jean 16.33 Apocalypse 12.3-12.5 Psaumes 37.12-37.14
14 Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.
Exode 19.4 Apocalypse 12.6 Daniel 12.7 Daniel 7.25 Esaïe 40.31
15 Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule.
Esaïe 59.19 Esaïe 28.2 Psaumes 18.4 Psaumes 93.3-93.4 Psaumes 65.7
16 Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake.
2 Rois 8.9 Exode 12.35-12.36 1 Rois 17.6
17 Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari.
Apocalypse 14.12 Genèse 3.15 Apocalypse 11.7 Apocalypse 1.2 Apocalypse 6.9

Cette Bible est dans le domaine public.