Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Jean 2.3
Bible en Swahili de l’est


1 Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki,
Romains 8.34 1 Timothée 2.5 2 Corinthiens 5.21 1 Jean 1.8-1.10 Jean 8.11
2 naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.
1 Jean 4.10 1 Jean 4.14 Jean 11.51-11.52 Jean 4.42 1 Pierre 2.24
3 Na katika hili twajua ya kuwa tumemjua yeye, ikiwa tunashika amri zake.
Jean 14.15 Jean 15.10 1 Jean 5.3 1 Jean 4.13 1 Jean 3.22-3.24
4 Yeye asemaye, Nimemjua, wala hazishiki amri zake, ni mwongo, wala kweli haimo ndani yake.
1 Jean 1.6 1 Jean 1.8 Jacques 2.14-2.16 Tite 1.16 1 Jean 4.20
5 Lakini yeye alishikaye neno lake, katika huyo upendo wa Mungu umekamilika kweli kweli. Katika hili twajua ya kuwa tumo ndani yake.
Jean 14.23 1 Jean 4.12-4.13 1 Jean 3.24 Jean 14.21 1 Jean 4.15-4.16
6 Yeye asemaye ya kuwa anakaa ndani yake, imempasa kuenenda mwenyewe vile vile kama yeye alivyoenenda.
1 Pierre 2.21 Jean 13.15 Matthieu 11.29 1 Corinthiens 11.1 1 Jean 2.28
7 Wapenzi, siwaandikii amri mpya, ila amri ya zamani mliyokuwa nayo tangu mwanzo. Na hiyo amri ya zamani ni neno lile mlilolisikia.
1 Jean 3.11 Lévitique 19.18 2 Jean 1.5-1.6 Matthieu 22.37-22.40 Romains 13.8-13.10
8 Tena nawaandikia amri mpya, neno lililo kweli ndani yake na ndani yenu; kwa kuwa giza linapita na ile nuru ya kweli imekwisha kung’aa.
Romains 13.12 Ephésiens 5.8 Jean 1.9 Jean 13.34 Jean 8.12
9 Yeye asemaye kwamba yumo nuruni, naye amchukia ndugu yake, yumo gizani hata sasa.
1 Jean 4.20 1 Jean 2.4 1 Corinthiens 13.1-13.3 1 Jean 2.11 1 Jean 1.6
10 Yeye ampendaye ndugu yake, akaa katika nuru, wala ndani yake hamna kikwazo.
Osée 6.3 Matthieu 18.7 2 Pierre 1.10 1 Jean 3.14 Romains 9.32-9.33
11 Bali yeye amchukiaye ndugu yake, yu katika giza, tena anakwenda katika giza, wala hajui aendako, kwa sababu giza imempofusha macho.
Jean 12.35 1 Jean 2.9 2 Corinthiens 4.4 1 Jean 1.6 Apocalypse 3.17
12 Nawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu mmesamehewa dhambi zenu, kwa ajili ya jina lake.
Actes 10.43 Actes 13.38 Psaumes 106.8 Luc 24.47 1 Jean 1.7
13 Nawaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mmemshinda yule mwovu. Nimewaandikia ninyi, watoto, kwa sababu mmemjua Baba.
1 Jean 2.14 Jean 14.7 1 Jean 1.1 1 Jean 4.4 Luc 10.22
14 Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.
1 Jean 2.13 Ephésiens 6.10 Jean 5.38 Psaumes 119.11 Jean 15.7
15 Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.
Jacques 4.4 Romains 12.2 Matthieu 6.24 1 Jean 3.17 Colossiens 3.1-3.2
16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.
Genèse 3.6 Romains 13.14 Psaumes 119.36-119.37 Ephésiens 2.3 Matthieu 5.28
17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.
1 Corinthiens 7.31 Romains 12.2 Marc 3.35 Matthieu 24.35 1 Pierre 4.2

Le retour du Seigneur et les antichrists

18 Watoto, ni wakati wa mwisho; na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja, hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho.
1 Jean 4.3 1 Jean 2.22 2 Jean 1.7 Matthieu 24.5 Matthieu 24.24
19 Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu. Maana kama wangalikuwa wa kwetu, wangalikaa pamoja nasi. Lakini walitoka ili wafunuliwe kwamba si wote walio wa kwetu.
1 Corinthiens 11.19 Actes 20.30 Deutéronome 13.13 Jean 4.14 Jean 15.2
20 Nanyi mmepakwa mafuta na Yeye aliye Mtakatifu nanyi mnajua nyote.
1 Jean 2.27 Marc 1.24 Jean 14.26 Proverbes 28.5 Psaumes 45.7
21 Sikuwaandikia ninyi kwa sababu hamwijui iliyo kweli, bali kwa sababu mwaijua, tena kwamba hapana uongo wo wote utokao katika hiyo kweli.
2 Pierre 1.12 Jude 1.5 Proverbes 9.8-9.9 Romains 15.14-15.15 Proverbes 1.5
22 Ni nani aliye mwongo ila yeye akanaye ya kuwa Yesu ni Kristo? Huyo ndiye mpinga Kristo, yeye amkanaye Baba na Mwana.
2 Jean 1.7 1 Jean 4.3 1 Jean 2.18 Jude 1.4 1 Jean 4.20
23 Kila amkanaye Mwana, hanaye Baba; amkiriye Mwana anaye Baba pia.
1 Jean 4.15 Jean 8.19 Jean 5.23 Luc 10.22 1 Jean 5.1
24 Ninyi basi, hilo mlilolisikia tangu mwanzo na likae ndani yenu. Ikiwa hilo mlilolisikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana, na ndani ya Baba.
Jean 14.23 1 Jean 1.3 Apocalypse 3.11 1 Jean 2.7 1 Jean 4.16
25 Na hii ndiyo ahadi aliyotuahidia, yaani, uzima wa milele.
1 Jean 1.2 Tite 1.2 Tite 3.7 Romains 2.7 Luc 18.30
26 Nimewaandikia haya katika habari za watu wale wanaotaka kuwapoteza.
2 Jean 1.7 1 Jean 3.7 Colossiens 2.8 2 Pierre 2.1-2.3 1 Timothée 4.1
27 Nanyi, mafuta yale mliyoyapata kwake yanakaa ndani yenu, wala hamna haja ya mtu kuwafundisha; lakini kama mafuta yake yanavyowafundisha habari za mambo yote, tena ni kweli wala si uongo, na kama yalivyowafundisha, kaeni ndani yake.
Jean 14.26 1 Jean 2.20-2.21 Jean 15.4-15.7 1 Corinthiens 2.13 Colossiens 2.6
28 Na sasa, watoto wadogo, kaeni ndani yake, ili kusudi, atakapofunuliwa, mwe na ujasiri, wala msiaibike mbele zake katika kuja kwake.
1 Jean 3.2 1 Jean 4.17 1 Jean 2.1 Colossiens 3.4 1 Jean 3.21
29 Kama mkijua ya kuwa yeye ni mwenye haki, jueni ya kuwa kila atendaye haki amezaliwa na yeye.
1 Jean 5.1 1 Jean 3.7 1 Jean 4.7 Jean 1.13 Jérémie 13.23

Cette Bible est dans le domaine public.